Jumapili, 3 Aprili 2016

UMUHIMU WA IMANI.


UJUMBE WA LEO 

  UMUHIMU WA IMANI.
Umuhimu wa imani katika maisha  ya mkristo ni lazima , kwasababu maisha ya kila mwenye mwili yanategemea imani,na hili jambo liko wazi kila mwenye mwili Mungu amempa kiasi cha
imani , ndio maana unaweza ukamkuta mtu hana hata ukaribu na Mungu lakini anasema tumuombe Mungu tutafanikiwa , hicho ni kiasi cha imani alichopewa na Mungu moja kwa moja.

Ili mkristo anayemtegemea  Mungu  aweze kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine kiroho inategemeana na bidii aliyonayo katika kuikuza imani yake.

(Kushindwa kwangu mimi kunatokana na mambo ya kiroho kuyatazama kimwili lakini ukweli  unajulikana , mambo ya kiroho hujulikana kwa jinsi ya rohoni.)

Imani inapofika katika kiwango cha juu mamlaka niliyonayo huwa hai na hapo ndio sehemu ya kutumia kinywa changu vizuri ,kwasababu kila nitakachokitamka kitatimia ,sasa wakristo wengi wanapokuwa katika kiwango hicho hujisahau na kutamka udhaifu.

(Nikitaka maisha yabadilike nibadilishe ukiri wangu.)

Mathayo 18:18-20

(Mathayo 18:18 ni picha halisi ambayo Biblia inamzungumzia mtu  anayeishi sambamba na Neno la Mungu au mwenye kulitendea kazi Neno la Mungu, mtu wa aina hii mamlaka ya kinywa chake itakuwa hai , kwahiyo lolote atakalotamka  muda wowote lazima lithibitike , kwasababu Yeremia1:2 kuna kitu pia Biblia imezungumzia.

(Hata kama nina ugumu wa maisha kiasi gani haitakiwi nipoteze  muunganiko  na Neno la Mungu , kwasababu thamani ya maisha ya mkristo kwenye uso wa Mungu inatokana na bidii aliyonayo katika Neno la Mungu) .

Neno la Mungu ndilo lenye uwezo wa kuibadilisha tabia yangu isiyompendeza Mungu, kwasababu lina uwezo wa kunijua hata kama mimi ninalisoma.

Jinsi ninavyopunguza bidii ya kulisogelea Neno la Mungu ndivyo ninavyoongeza uvamizi kwenye ulimwengu wa roho.

Yeremia 1:11-12.

Roho ya maono inakuwa dhahiri katika maisha ya mtu  jinsi anavyozidi kuzama katika  kina cha Neno la Mungu , ndio maana watu wengi adui hatupi nafasi ya kutosha  wa kulilingana Neno la Mungu.

Imani inayotokana na Neno la Mungu ni imani yenye uwezo wa kukabiliana na jaribu la aina yoyote  bila kukata tamaa  na ikapata ushindi , kwasababu ni imani ambayo inakuwa imeatamiwa na upendo halisi wa Kimungu.





Hakuna maoni: