Jumapili, 26 Oktoba 2014

NAMNA YA KUMILIKI BARAKA ZA MUNGU.



26/10/2014
UJUMBE WA LEO
NAMNA YA KUMILIKI BARAKA ZA MUNGU
Ukweli Mungu anatubariki, lakini kwasababu ya upofu wa kiroho hatuzioni Baraka hizo zikidhibitika.

Hii ni hatari sana kwa wakristo wengi wanafahamu Baraka za Mungu ni pesatu,lakini Baraka za Munguzimegawanyika katika  sehemu kuu tatu
A)Kuna Baraka za Kiafya.
B)Kuna Baraka za Kiuchumi (Pesa)
C)Kuna Baraka za Uzima wa milele (Wokovu)


Baraka za Mungu haziambatani na maisha ya wakristo wa leo kwasababu wakristo wa leo wamevaliwa na roho ya Kaini, vilevile roho ya Anania na Safira,roho ya Kaini, roho ya Anania na Safira huaribu mzunguko mzima wa Baraka ya  mkristo anayechuma na Mungu ,ndio maana asilimia kubwa ya wakristo waliokoka ni masikini vilevile hawana mpenyo katika maisha .

Roho ya Kaini tunaisoma kuanzia Mwanzo 4:1-15 roho ya Anania  na Safira tunaisoma  katika Matendo ya Mitume 5:1…….

( Wakristo wengi hawazitendei haki karama zilizoko ndani mwao ndio mwanzo wa maisha yao kuharibika , hili linanidhibitishia utoaji ni karama vilevile ni imani)

Kwenye uso wa Mungu Kaini aliponzwa na mambo yafuatayo:-
i)Tamaa ya mali.
ii)Wivu, hizi ndizo roho zilizoponza utumishi wa Kaini mpaka akawa muasi kwenye uso wa Mungu,mpaka sasa ni roho zinazoyagawanya makanisa ya Mun gu kwasababu wana wa Kaini wamezidi kuwa wengi katika makanisa ya Bwana.

( Hakuna Baraka ya Mungu inayoweza kuingia kwenye maisha ya mtu anayetoa sadaka iliyo kilema )

Roho ya Kaini ikiyavamia maisha ya mwamini aliyeokoka huathiri maisha yake katika maeneo yafuatayo :- i) Eneo la kwanza itaharibu Baraka inayotokana na Mungu katika maisha yake.
ii) Eneo la pili itaharibu mzunguko wa Baraka za wale wanaomsaidia.
iii) Husababisha na kulazimisha roho ya umasikini katika maisha ya mtu huyo,vilevile katika uzao wake.
MFANO;Katika hali ya kibinadamu
                  Baba na Mama katika familia wakiwa ni wachoyo hata mtoto watakayemzaa  atakuwa ni mchoyo, kwasababu motto anarithi kutoka kwa Baba na Mama.

Roho ya Kaini huathiri sana Baraka ya mkristo anayechuma na Mungu.

Ili niweze kuepuka roho ya Kaini inatakiwa niruhusu roho yangu kuelimishwa na Neno la Mungu,tena katika mazingira yafuatayo:-
i)                    Kufundishwa Neno la Mungu (Biblia)
ii)                   Kutoa muda wa kusikiliza Neno la Mungu (Mafundisho)
iii)                 Kujifinza hali ya kujisomea Biblia mara kwa mara usiku na mchana kamaneno aliloagizwa aliloagizwa Yoshua
                                                              Yoshua 1:8
Jambo hili ni la kuelewa  sana mkristo anayemwamini Yesu Kristo mwongozo wake ni Biblia.
ANGALIZO :1.Ushauri wa kweli na haki uko ndani ya Biblia,ukiteleza hapo mzunguko wote wa maisha
                          Wote unaharibika.
( Nikizitaka Baraka za Mungu lazima nilipe gharama )
Hakuna Baraka ya Mungu inayoweza kuyavaa maisha ya mtu mwenye asili tatu ndani mwake ambazo ni:- 
      i) Hila
      ii) Wivu
     iii)Tamaa

( Inatakiwa nimshukuru Mungu kupitia Baraka ya jirani yangu ambayoMungu amemsaidia huo ndio upendo).

KIFO CHA WAAMINI.
Kifo cha waamini asilimia tisini na tano duniani  kinatokana na kumwibia Mungu sehemu ya kumi yaani fungu la kumi.

( Mungu ana wivu na sehemu ya kumi kuliko kitu chochote,ndio maana akasisitiza kwa maandishi  kwenye Maandiko Matakatifu)
Malaki 3:8-12
Sehemu ya kumi ya Mungu mwamini anapoitoa kiuaminifu humlinda katika mazingira haya:-
a)      Hulinda kazi yake au biashara na mzunguko mzima wa kipato chake.
b)       Humlinda afya yake  na mzunguko mzima wa familia yake.
c)       Humuongezea wingi wa siku na maisha marefu.
Kama mimi ni mtoaji wa fungu la kumi kwa uaminifu maana yake ninairahisisha kazi ya Mungu isone mbele,lakini kama mimi ni mwizi wa fungu la kumi maana yake ninaididimiza kazi ya Mungu ikwame.
Baraka ya Mungu huja kwa mtu kulingana na mtu anavyokuwa na bidii ya kutoa.
Maisha ya wakristo walio wengi yanaathirika kwasababu wanayakataa maarifa ya Mungu na Mungu naye anawakataa wakati wa msiba wao,na hili jambo kalinena katika maandiko
Mithali 1:24-29.
Ninapomnyima masikini  haja ya moyo wake vilevile nikamnyima Mungu sehemu yake nisitoe kwa uaminifu,nitakuwa nimetangaza ugomvi na uwepo wa Mungu,kwa hiyo kitakachofuata katika maisha yake ni majanga tu.
( Mwamini anavyotoa ndivyo anavyojisogeza karibu na uwepo wa Baraka ya Mungu).
Mkristo anapomuibia Mungu sehemu yake yaani fungu la kumi huaribu Baraka yake na baraka ya familia kwa ujumla.
NINI INATAKIWA NIFANYE ILI NIWE MWAMINIFU KWENYE FUNGU LA KUMI
Inatakiwa nitambue kwanza Baraka  ninayoipata inatokana na nani, hapo utakuwa mwanzo wa kuona uzito wa utoaji kiukamilifu kwenye uso wa Mungu.
Jinsi ninavyokuwa mtoaji zaidi katika kuuimarisha ufalme wa Mungu ndivyo Mungu anavyoniongezea mambo yafuatayo katika maisha yangu:-
i)Wingi wa siku na maisha marefu.
Shauku ya Mungu ni kutuona wakristo waamini  tukiuimarisha na kuujenga ufalme wake kupitia mali zetu, ndio maana katika kipindi cha Mitume mali za wale wakristo waamini wa kipindi kile  zilikuwa ni ushirika mmoja.
Kama unahitaji Baraka za Mungu kwelilkweli nijifunze kuuwezesha ufalme wa Mungu.
Kinachowafanya wakristo wasitimize wajibu wao ndani ya kanisa ni hali ya mazoea na ndiyo inayowaletea laana.

Hakuna maoni: