Jumapili, 4 Januari 2015

MAOMBI YANAYOLETA BARAKA

4/1/2015.
MAOMBI YANAYOLETA  BARAKA.
Maombi yanayoleta Baraka katika maisha  yangu, ni maombi ambayo inatakiwa niombe katika mazingira yafuatayo:-
a)Katika imani
b)Kwa kutumia misingi ya Neno la Mungu
c)Katika haki na kweli,haya mambo Kibiblia yameelezwa  Zaburi 51:6,10,17.

(Kweli ya Mungu nitakayoiruhusu kujijenga moyoni mwangu ndiyo itakayonisaidia kunifunulia hekima ya Kimungu katika misha yangu, vilevile ndiyo itaqkayoniingiza katika mkondo wa Baraka za Kimungu)

Maombi yatakayo lazimisha Baraka za Mungu kuja juu ya mtu lazima mwamini ahakikishe anaishi maisha ya haki na kweli.

(Ni vigumu kupata mpenyo wa Baraka kama sija ruhusu maisha yangu yaongozwe na Roho Mtakatifu).

Siri za Kimungu zinajifunua kwa mwamini anayeishi maisha ya kweli na haki.

Maombi ya wakristo wengi hayapati kibali machoni pa Mungu kwasababuwanaomba katika hila, na mtu yoyote anayeomba katika hila milango ya kiroho ,au kina cha maarifa ya rohoni hujifunga.

Kina cha maarifa ya rohoni kikijifunga nitakuwa mkristo nisiyekuwa na faida katika maeneo mawili:-
A)Katika uso wa dunia ,nikiwa na maana zaidi sitakuwa na msaada wowote kwa jamii iliyonizunguka bali nitakuwa mzigo kwa jamii iliyonizunguka,ndiyo maana wakristo wengi hunyooshewa vidole,hii ni kwasababuni mzigo kwa jamii
                                                                      Mwanzo 4:1-5.

Kilichomfanya Kaini apoteze kibali machoni pa Mungu heshima yake itoweke ni:-
i)Hila
ii)Wivu
iii)Majivuno
iv)Kiburi cha uzima ,haya mambo ndiyo yanayowagharimu waamini wa leo ndiyo maana huishia kwenye kutangatanga katika makanisa na kutaguta msaada.

Hii haitapingwa na chochote milele mbingu itafungua masikio kwa mwamini ambaye ameumimina moyo wake kwa Yesu Kristo peke yake.

(Maisha ninayoyaishi chini ya jua ninajiandalia maandalizi ya ufalme utakaonipokea baada ya kifo cha kimwili ,hapo inategemea maisha  ya dhambi baada ya kifo kuna ufalme utakao nipokea kwaajili ya kulipwa haki yangu sambamba na maisha ya kweli na haki baada ya kifo cha kimwili kuna ufalme utakaonipokea kwaajili ya kunilipa sambamba na maisha ya haki na kweli niliyoishi chini ya jua).

B)Sitakuwa na faida kwenye uso wa Mungu mwamini aiyekuwa na faida kwenye uso wa Mungu mara nyingi ni Yule mkristo anayepingana au asiyekubali kukaa chini ya mwongozo wa Biblia unavyosema .

Mara nyingi mwamini asiyekuwa na faida kwenye uso wa Mungu ni yule ambaye amepoteza kibali ,kwa hiyo mkristo anayepoteza kibali kwenye uso wa Mungu  huandamwa na mambo yafuatayo:-
i)Kukataliwa popote anapokanyaga.
ii)Kuandamwa na magonjwa yasiyoonyesha chanzo  katika vipimo vya madaktari
iii)Umasikini vilevile kupoteza ulichonacho.

Mkristo wa aina hii kwamwe haiwezi kuonekana hekima ya Mungu katika maisha yake kwasababu anakuwa ameshatoka nje na fomula ya Roho Mtakatifu.

B) ILI NIWE NA MUUNGANIKO WA BARAKA ZA MUNGU.
Ili niwe na muunganiko na Baraka za Kimungu inatakiwa nizame sana katika suala la maombi ndiyo yanayolazimisha njia ya mtu kumuona Mungu kufunguka ,vilevile maombi ndiyo yanayomsaidia mwamini kuzungumza na Mungu ,ndiyo maana inatakiwa niombe katika misingi ya Neno la Mungu (Biblia).

Maombi yatakayo sababisha muunganiko  wa mtu na Mungu ni maombi yanayoombwa sambamba na Maandiko Matakatifu (Biblia).

Kibali cha maombi yetu kujibiwa kwenye uso wa Mungu  kitatokana na misingi ya Neno la Mungu ambayo ni Biblia.

Mkristo anayeishi chini ya msingi wa Neno la Mungu maana yake anaishi katika kweli ya Neno la Mungu.

ANGALIZO 1:Jinsi ninavyopoteza muda wa kusoma Biblia katika mambo mengine yasiyokuwa
                        na maana Ndivyo ninavyojiongezea mashambulizi na hali ya kushambuliwa 
                        na shetani  katika roho.

Nguvu ya maombi huzalisha imani yenye uwezo wa kustahimili na uvumilivu ndani yake ,na imani hii mara nyingi ndiyo inayoweza kuzalisha Baraka hai kwa mwamini,vilevile ndiyo yenye uwezo wa kumshawishi Mungu kubariki,jambo hili  tunalisoma katika kitabu cha Danieli 3: yote.

Nikitaka kuitunza mamlaka ya Mungu katika maisha yangu haitakiwi niwe mwepesi  wa kunena mahali popote,kwasababu kinywa hunajisi nguvu ya Mungu  iliyoko ndani ya moyo wa mtu,ndiyo maana Meshaki, Shedraki na Abedinego hawakutaka kumjibu mfalme  neno lolote kama  ilivyoandikwa katika Danieli 3:16, waliepuka  kuiathiri imani waliyokuwa nayo kwa Mungu,ndiyo maana mwisho walipata ushindi.

(Hakuna mwamini aliyemtukuza Mungu katika ugumu alionao Mungu akaacha kumuinua ,Kwahiyo lazima nitambue siku zote imani niliyonayo ipo kwaajili ya kutengeneza njia mahali paliposhindikana  katika maisha yangu ).

Hekima ya Mungu ni namna ambavyo nitajiunganisha na mtiririko wa Neno la Mungu (Biblia).

C) NINI KIFANYIKE ILI NIWE SAMBAMBA NA BARAKA ZA MUNGU.
Ili niweze kuendana na Baraka za Mungu inatakiwa nifanye mwendelezo wa kuikuza imani yangu kupitia Neno la Mungu katika mazingira yafuatayo:-
a)Kukaa chini kufundushwa Neno la Mungu (Biblia),kwasababu kitendo cha mimi kufundishwa Neno la Mungu ndivyo milango ya ufahamu wa rohoni unavyofunguka  na kupata upeo wa  kuongezeka ziadi  katika ufahamu wa Kimungu.

Maelezo na ufafanuzi kuhusiana na ‘a’
Kitendo cha mimi  kukubali kukaa chini  kufundishwa Neno la Mungu  maana yake nimeamua kuyaruhusu maisha yangu  yaongozwe na Roho Mtakatifu,hapo kutazaliwa mambo yafuatayo :-
i)Kibali
ii)Mpenyo.
iii)Mafanikio.
iv)Ukaribu kati ya mimina Mungu .

Hali ya kufundishwa Neno la Mungu itanizamisha zaidi katika unyenyekevu wa kiroho kuhusiana na hapo nitapata faida zifuatazo:-
i)Macho ya kiroho kuwa wazi
ii)Masikio ya kiroho kusikia, hapo  ndiyo mwanzo wa kupata Neema ya kupambanua sauti ya Mungu pale anaposema na mimi.

ANGALIZO 2:Siku zote hakuna aliyefanya  kazi yoyote au biashara  kwa muongozo wa Roho
                       Mtakatifu akafeli, bali hufanikiwa zaidi maradufu .

Kufundishwa Neno la Mungu  humsaidia mkristo kutambua  haki zake kwenye uso wa Mungu ,mara nyingi hii humsaidia  mwamini kuimarika  zaidi katika misingi  ya kumjua Mungu, ndiyo maana hata Biblia  imeelezea kwa kina  1Timotheo 4:4-8.

Nikisimama vizuri  katika misingi ya Neno la Mungu nikafundishwa kweli kuhusu Mungu ukweli ni kwamba mila yangu haifai ‘‘Ee Yesu nisaidie akili yangu iyakubali haya niliyoyasikia leo’’.

b)Kusoma Biblia
Maelezo na ufafanuzi kuhusiana na ‘b’
Mimi kama mwamini lazima nifahamu kitendo  cha kusoma Biblia maana yake  ni moyo wangu unazungumza na Mungu waziwazi,kwasababu Mungu asili yake ni Neno  na maneno haya yamethibitishwa kupitia kitabu cha Yohana 1:1,2.

Yohana 1:1 ni udhihirisho tosha ya kwamba kitendo cha kusoma Biblia maana yake ni Mungu anazungumza na mimi waziwazi.

(Nikihitaji uponyaji inatakiwa nijifanyie maandalizi kwanza ya usomaji wa Biblia ili moyo wangu upate utayari wa kupokea  kutoka kwa Bwana pale nitakapotamkiwa).

Nikiongeza bidii katika kusoma Biblia  ndivyo ninavyozidi kuongezeka  katika nguvu za rohoni,kwahiyo ni rahisi sana  nikapata mpenyo utakaoweza kuendesha maisha yangu ya kiroho na kimwili.

Swali:Nini maana ya kuongezeka nguvu za rohoni?


Jibu:Maana ya kuongezeka nguvu za rohoni ni kile kitendo cha imani yangu kuliamini Neno la Mungu asilimia zote ndio maana hata Biblia imesema katika Waebrania 11:6.

Hakuna maoni: