Jumapili, 21 Februari 2016

MADHARA YATOKANANYO NA KINYWA KWA WAAMINI WANAO MCHA MUNGU

MADHARA YATOKANANYO NA KINYWA KWA WAAMINI WANAO MCHA MUNGU

 Mamlaka ambayo Mungu amenipa inatakiwa niitumie katika kubariki sio kulaani watu wengine.


Mkristo ambaye anamcha Mungu inatakiwa awe na tahadhari  sana katika maneno ya kinywa chake, kwasababu katika maneno hayo ndipo anapopatia wepesi wa kubarikiwa au ugumu wa kuharibu maisha yake.

Jinsi ninavyoamini moyoni mwangu , ndivyo inavyotakiwa katika kinywa changu ninene, hapo kuna Baraka Warumi 10:10.

Kama moyo wangu unaamini katika mapenzi ya Mungu vivyo hivyo hata kinywa changu kinatakiwa kikiri mapenzi ya Mungu.

Nikiwa mimi ni mkristo ninayemcha Mungu,ninayempenda Mungu inatakiwa niulinde  moyo wangu kupitia Neno la Mungu, kwasababu kitendo cha  moyo wangu kukosa utulivu kinywa change hakiwezi  kuwa sambam,ban a mapenzi ya Mungu, ndio maana unaweza  kukutana na mkristo aliyeokoka  lakini maneno ya kinywa  ni aibu hata  kuyasikiliza.

TAHADHARI
Jambo lolote nisilokuwa na uwezo nalo kulifanya haitakiwi nimahidi mtu  kwamba nitakufanyia ,kwasababu jambo hilo laweza kuwa mtego kwangu wa kufunga Baraka zangu siku zote,Hata Biblia imesema  katika Mhubiri 5:2.

Kitu cha kuchunga sana nikiwa kama mkristo shetani anajitahidi kuchunguza  maneno ya kinywa change ilia pate sababu ya kuharibu maisha yangu, ndio maana Biblia ikatoa tahadhari hii Mithali 6:2.

Juu ya jambo hili Yesu anisaidie , ninavyonena kinyume na kinywa changu ninaandaa mazingira ya mgandamizo ambao utayafanya  maisha yangu  yapoteze mwelekeo  wa Baraka za Mungu, kwahiyo  hata kama nimekutana na ugumu  kiasi gani katika maisha inatakiwa nikiri mapenzi ya Mungu peke yake, kwasababu hata kama  Mungu hajafanya haitabadilisha maisha yake.

Mabaya huja katika maisha ya mtu anayemwamini Mungu kumpima kiwango chake cha kumwamini  Mungu,kwahiyo wakristo walio wengi  hii siri hawaijui, ndio maana wengi huangukia  katika dhambi ya kumkufuru Mungu kwa bvinywa vyao.

Jambo la kujua
Kuna magumu mengine au mabaya mengine au majaribu huja katika maisha yetu kwa lengo zuri  la kukusogeza karibu na uwepo wa Mungu ,hata Biblia imetoa maelezo juu ya hili Yakobo 1:2-3.

(Haitakiwi nisubiri maumivu ndio nimtafute Mungu kuna gharama zake).

Kila jaribu linalopita katika maisha yangu ndani yake kuna Baraka za Mungu,ndio maana inatakiwa nisitetereke katika imani.

Kinywa  cha mkristo ambacho  hakineni kweli hakina muunganiko wowote nba Baraka za Kimungu,kwasababu Mungu ni kweli na wote wamwaminio inatakiwa  waishi katika kweli.

Anenaye kweli huupendeza moyo wa Mungu na nafsi ya Mungu huwa karibu na mtu anayenena kweli.



Hakuna maoni: