Jumapili, 9 Agosti 2015

SAFISHA MOYO ILI BARAKA ZA MUNGU ZIPATE MPENYO



SOMO LA LEO
9/8/2015
SAFISHA MOYO ILI BARAKA ZA MUNGU ZIPATE MPENYO
Moyo ndio njia kuu ambayo Mungu anaitumia kuzungumza na mtu,ndio maana Maandiko Matakatifu yanatusisitiza sisi ambao ni waamini kuilinda mioyo yetu ,hii ni kwasababu moyo wa mwamini ukijeruhika  moja kwa moja hupoteza mawasiliano na Mungu.

(Hekima na busara zinatokana na moyo wa mwamini kuwa safi na wazi machoni pa Mungu.)
Moyo wa mwamini ukiwa ukiwa safi hupata  Neema machoni pa Mungu yaani kuisikia sauti yake waziwazi ndio maana Biblia ikasema katika kitabu cha Mithali 4:23.

Moyo wa mtu anayemwamini Mungu unaweza ukwalindwa kwa njia zifuatazo:-
I) Kuusikilizisha moyo wake Neno la Mungu , na hili jambo linatakiwa liwe ni tendo endelevu.
II )Kuhakikisha unasikiliza mafundisho yenye mafunuo ya Roho Mtakatifu, mafundisho haya huwa hayapingani na Biblia  yaani kilichoandikwa ndani ya Biblia.

ANGALIZO 1:Kama sisomi Biblia maisha yangu yanakuwa hatiani muda wowote, kwasababu sitakuwa na ufahamu wa kupambanua hata kama ninadanganywa mimki nitakubali tu na ndipo kifo  cha watu wengi kinapo anzia.

(Moyo wangu usipo safishwa kwa Neno la Mungu ni vigumu kukubaliana na kile ambacho Mungu anasema kwa maana Zaidi ,kwa sehemu utakubaliana na sehemu utakuwa na mashaka  na Biblia imesema wazi juu ya hili Warumi 14:23.)

(Moyo ukikosa utulivu tayari ni ugonjwa ‘Eee Yesu niepushe na hili janga)’.

ANGALIZO 2:Ninapo ingiza shaka katika Neno la Kinabii ninalotamkiwa na Mtumishi wa Mungu maana yake ninaharibu mfumo mzima wa Baraka zangu kwenye uwepo wa Mungu.

NINI KIFANYIKE NIWEZE KUUTUNZA MOYO WANGU?
Kwanza kabisa kabla ya kupata mbinu ya kutunza moyo wangu inatakiwa nifahamu tabia za moyo wangu kupitia Biblia.

Tabia za moyo wa mtu zinaelezwa kama ifuatavyo katika kitabu cha Yeremia 17:9.

Udanganyifu ulioko ndani ya moyo wangu ni vigumu kudhibiti ikiwa sina kina cha maarifa ya Neno la Mungu.

(Nikilipokea Neno la Mungu katika hali ya Roho Mtakatifu hisia haitakuwa na uwezo wa kuathiri moyo wangu, ndio maana ninahitajika kulisikiliza Neno la Mungu kupoitia masikio ya kiroho, masikio ya kiroho humsaidia mwamini kupoata mabadiliko  kupitia kile anachokisikiliza 9Neno la Mungu).

Moyo uluiofunguliwa na ambao unahitajika awe nao mwamini anayemwamini Yesu Kristo ni kama ifuatavyo kupitia Maandiko Matakatifu Wagalatia 5:22-26.

Moyo uliofunguliwa ndani yake kuna kitu kinachoitwa Roho ya Munguna hiyo ndio inayohitajika kwa kila mtu amwaminie Mungu.

Moyo uliofunguliwa kwa Neno la Mungu ndani yake kuna mambo yafuatayo:-
i)Roho ya Upendo
ii)Roho ya Furahas
iii)Roho ya Amani
iv)Roho ya Uvumilivu.
v)Roho ya Utu wema
vi)Roho ya Fadhili
vii)Roho ya uaminifu
viii)Roho ya Upole kiasi

Roho iliyofunguliwa ina uwezo wa kubeba madhaifu ya kila  namna, nah ii ndio ilikuwa tabia ya YESU KRISTO

Ikiwa mimi ni mwamini na hapohapo bado roho yangu haijafunguliwa ni vigumu kuyatimiza mapenzi ya Mungu , na hili ni jambo limeaathiri kanisa la leo.

WAKRISTO WA LEO WAMEATHIRIKA ZAIDI KIIMANI NDIO MAANA WANASHINDWA  KUZITAMBUA SIRI ZA MUNGU
Kuna siri  ambayo kanisa la leo halijagundua  ndio maana jamiikubwa ya wakristo hawana mpenyo katika maisha yao ingawa wanaomba na kuombewa.

Mambo yote ninayoyahitaji ya kimwili yawe ya ziada lakini roho yangu inatakiwa iwe safimuda wote machoni pa Mungu, kwasababu muujiza wa kwanza katika maisha ya mtu ni kuwa na uhakika kwamba jina lakelipo katika kumbukumbuya vitabu vya uzima wa milele.

Tunaporudi katika suala la Baraka hapo inategemea kiwango cha akaunti yangu jinsi inavyosoma kulingana na jinsi ninavyowekeza kwenye uwepo wa Mungu.

(Kama uchumi wangu hakuna mkono wa Mungu ndani ya hayo ni mafanikio ya muda mfupi muda wowote yanaweza kufilisika ).

(Tabia haiponyeki  ukiwqa nje na uwepo  wa Mungu bali tabia inaponyeka  ukiwa mbali na uwepo wa Mungu ).

Katika suala hili nahitaji umakini  hapas nitaepuka mambo yaliyo mengi.

Ninapoingia kwenye uso wa Mungu kuomba labda jambo Fulani inatakiwa nihakikishe , kwasababu majibu ya mtuyanakuja.

MAELEZO KWA UFUPI  KUHUSU SUALA LA UCHUMI
Ukweli ni kwamba sualka la uchumi ni jambo ambalo  halihitaji maombezi kwa kuombea bali ni jambo linalohitaji  kudumu katika kanuni ya utoaji kama Maandiko yanavyosema Malaki 3:8-10, Luka12:34. Luka 16:10 Matendo ya Mitume10:1-5 ,Matendo ya Mitume10:9:36-40 NA 2Wakorintho 9:6-8

Utoaji wangu inatakiwa autambue Mungu asiutambue mwanadamu ndipo utakuwa na Baraka.

Utoaji nisehemu inayoufanya moyo wa Mungu kuwa na furaha na mtu.

Utoaji una nguvu ya kutiisha mauti.

Ninaposimama kwenye uso wa Mungu  kuomba kuhusiana na suala la uchumi Mungu anatazama  kiwango ninachokihitaji kwenye uso wake  Je! Kinaendana na utoaji wangu?

Ninaposimama  kusapoti kazi ya Mungu maana yake ninaweka muunganiko na Mungu katika roho yaani  kibiblia  ninaitwa mtu ambaye  ninamkopesha Mungu  na jambo hili hata Biblia imesema  katika Miithali 19:17.

Ninapotoa pesa yangu kusapoti jambo lolote ndani ya kanisa  linalohusiana na faida za Mungu ,Kibiblia ninaitwa mtu ambaye ninamkopesha Mungu sehemu ya mali yangu na inafahamika wazi vyote  nilivyo navyo  na vinavyofanya watu waniheshimu na kuniogopa  vinatokana na Mungu Je! Nikitoa sehemu yangu kumpa Bwana ni faida gani nitakayoipata? Katika hili inatakiwa nilijibu swali hili mwenyewe.





Hakuna maoni: