SOMO LA LEO
2/8/2015
JIIMARISHE KATIKA
ROHO
Inatakiwa nijiimarishe katika roho kwasababu adui
ninayepambana naye yupo katika roho,ndio maana kushindwa kwa mkristo kunaanzia katika roho na ukiona hali hiyo imedhihirika kimwili jua wazi mtu
huyo kiroho amekufa kabisa (anakabiliwa
na kifo cha kiroho).
Katika maisha ya kiroho ufahamu ni suala la msingi sana.
Kujiimarisha kiroho kwa tafsiri nyingine ni kujiimarisha kiimani , na hii ni kwasababu
Imani ni kitu kamili cha rohoni.
Mfumo wa mawazo ukisha tetereka kwa mwamini mwelekeo wa Imani
unapotea, na hapo ndiyo unakuwa mwanzo
wa mwamini kuwaza vibaya , linda mfumo
wa mawazo yako utakuwa umeitunza Imani .
Nikiruhusu hali ya kuwaza vibaya nitakuwa nimeathiri mfumo
wa Imani ,kwahiyo nitaamini kinyume pia
ndiyo maana Biblia ikasema wazi katika Nuhumu 1:9.
Mawazo ni aina Fulani ya mipango inayotengenezwa ndani ya
moyo wa mtu, ndiyo maana kile ambacho mtu anakinena ndani ya kinywa chake amekidhamiria kabisa.
Ni vigummu kuyatambua mawazo ya mtu anayoniwazia akiwa hajafungua kinywa kunena au kuongea, ndivyo
ilivyo ni vigumu kuyatambua mawazo ya Mungu anayokuwazia ikiwa sio msomaji wa
Biblia wala msikilizaji wa Neno la Mungu.
Kushindwa kwangu kwingi kunatokana na kutokutambua mawazo ya
Mungu anayoniwazia , ndiyo maana naweza kujikuta nimejikwaa kwenye uwepo wake na kupoteza mtiririko wa Baraka
zangu.
Ninaharibikiwa
kwasababu bado sijatambua mapenzi ya Mungu ni yapi katika maisha yangu, ndiyo maana
nahitajika kujiimarisha kiufahamu.
(Ufahamu wangu ukikua kuhusu Mungu nimeyaponya maisha yangu ya
kiroho na hili jambo walikutana nalo
Meshaki , Shedraki na Abednego
Danieli 3:1-30
SWALI
Katika Danieli 3:15
ndani ya huo mstari kuna maneno gani
JIBU:
Kuna maneno ya kushawishi
Mwamini aliyefunikwa na uwepo wa Mungu mahali popote
anapokanyaga anakuwa tayari amepatawala katika roho , kwahiyo hali hii
humsaidia mwamini kugeuza mawazo ya adui
yake kwenda sambamba na jambo analolikusudia
yeye, nah ii lilithibitika dhahiri mwisho wa safari ya Meshaki Shedraki
na Abednego mawazo ya adui yao ambaye ni Mfalme Nebkadreza yalibadilishwa
yakaendana sambamba na mawazo ya Watumishi wa Mungu kama inavyosema katika
msatari wa 29-30.
(Sababu itakayomfanya adui
yangu kugeuza ufahamu wake na kukaa chini ya miguu yangu ni mimi kujiomheza kiufahamu Zaidi
wa Neno la Mungu).
Katika Danieli 3:16,
17 unadhihirisha wazi maneno ya kiufahamu , maneno ya kiimani , maneno ya
hekima maneno ya uaminifu kwa wanae mtumaiania , mtu wa aina hii hawezi
kushindwa na changamoto yoyote atakuwa mshindi tu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni