KIMBILIO NI YESU
KRISTO PEKEE
Hakuna
kimbilio lingine pengine popote nje na
jina la Yesu Kristo.
Jamii kubwa
ya waamini wanaokata tama wengi wao bado hawajafahamu
ukweli kuhusu Maandiko Matakatifu.
Jina la Yesu
Kristo liko tayari kumbeba mtu au kuficha aibu ya mtu ambaye moyo wake ameufungua katika Neno la Mungu.
(Nikifundishwa
Neno la Mungu vizuri nikaimarika kiufahamu siwezi kuwa limbukeni wa nyakati
zozote ninazokutana nazo).
Kama
kimbilio ni Yesu Kristo pekee inatakiwa nijiongeze kiufahamu ili niweze
kuendana sambamba na Baraka zitokanazo na waliaminio jina hili, hapo nitakuwa
nimeyarahisishia maisha yangu hali ya
wepesi katika kila hatua ya jambo ninalolikusudia.
Wafilipi 2:1-10
Ili niweze
kulilingana jina la Yesu Kristo na kila niliitapo linipe faida inatakiwa
nifanye mambo yafuatayo kwenye maisha yangu:-
I)Upole wa
roho, na upole wa roho huzaa hali ya uvumilivu katika maisha ya mtu
II)
Haitakiwi majivuno katika maisha ya mcha Mungu
III) Hali ya
unyenyekevu
IV) Upendo
(Mtihani
wowote unaohusiana na mambo ya kiroho
nitaweza kuushinda kama nitakubali kukaaa chini ya mafunuo ya Roho Mtakatifu,
kwasababu Roho Mtakatifu yuko maalumu kufunua siri yoyote au kutupasha habari
katika yale tunayokusudiwa siku zijazo
haijalishi ni mazuri au mabaya , Biblia imethibitisha neno hili katika kitabu cha 1Wakoritho 2:10).
Kinachofanya
jina la Yesu Kristo lionekane linatenda mambo makubwa katika maisha ya mtu ni
ile hali aliyonayo mtu ya mahusiano mazuri na Roho Mtakatifu kupitia Neno la
Mungu .
Mahusianao
mazuri na Roho Mtakatifu ndiyo
yanayolifanya jina Yesu Kristo liwe hai
na kuthibitisha miujuza uponyaji na
mambo mengine mengi , ndiyo maana huyu anaweza akalitumia jina la Yesu Kristo
likaponya wagonjwa na watu wakafunguliwa , wakaponywa na mwingine anaweza akalitumia jina la Yesu Kristo lisitokee chochote. Je!hapo shida inakuwa ni
nini?,
Shida
inayosababisha mtu ashindwe kulitumia jina la Yesu Kristokufanya ishara mara
nyingi inatokana na ufahamu mdogo anaokuwa nao katika kulijua Neno la Mungu.
Neema ya
Mungu imetolewa bure kwa kila aaminiye , Hata neno hili Maandiko
Matakatifu yamelithibitisha katika
kitabu cha Marko 16:15-18.
ANGALIZO 1:Ninapoukimbia uso wa Mungu yaani
nikaacha kwenda kanisani kwa kuvunjika moyo
au kukata tama, shetani atayageuza maisha yangu jalala la matatizo
,ndiyo maana wakristo wengi leo hii wanahaha hawana pa kuelekea.
Kinachowafanya
wakristo (waamini) wakate tama ya kumtafuta Mungu zaidi ni mambo haya
yafuatayo:-
I)
Wengi
wao wamejeruhiwa na viongozi wao wa kiroho yaani wachungaji wao, Kivipi?
A)Kuzini nao
B)Kuwabebesha mimba
C)Kuvunja ndoa zao na maengine mengi
II) Wengine wametapeliwa na viongozi wa kiroho
na kufilisiwa mali zao , Kivipi?
A) Bwana anasema umtolee sadaka Fulani.
B) Nikopeshe kadhaa nitarejesha lakini
ndio kwaheri yaani hiyo hairudi tena ,
Mambo kama hayaau mkristo aliyekutana na mambo kama haya yakamkuta kwenye
maisha yake asipopata mshauri wa kiroho
mwenye ufahamu wa ndani wa Kimungu maisha yake hayawezi kurudi kawaida
bali ataishi katika mazingira haya:-
A) Kutokusamehe
B) Visasi
C) Chuki
D) Lawama
E) Manung’uniko
Je! Ikiwa ni
kiongozi wa kiroho umesababisha mambo
kama haya kwa mwamini wako ambaye
unamhudumia kiroho, Damu ya mtu huyo itadaiwa mikononi mwa nani?
Jibu
mwenyewe msomaji
(Nikiruhusu
kukaa chini ya mwongozo wa Roho Mtakatifuhakuna mahali popote nitakapo
tetereka,, nikitetereka Roho
atanirejesha kwa sauti ya upole na upendo).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni