UJUMBE WA LEO.
25/12/2014.
SABABU ZA YESU KRISTO KUZALIWA.
Ziko sababu nyingi sana za Yesu Kristo kuzaliwa ,lakini kuna
sababu moja kuu iliyopelekea kuzaliwa katika mwili.
A)Sababu kuu ya Yesu Kristo
kuzaliwa katika mwili na kuuacha
utukufu aliokuwa nao mwanzo ni ili aje awe sadaka ya ukombozi kwa kila atakaye mwamini.
(Hakuna sadaka nyingine yoyote ya ukombozi chini ya jua nje na Yesu Kristo).
Kuzaliwa kwa Yesu Kristo ndiko kunakoonyesha picha halisi ya
kuurithi ufalme wa Mungu katika haki na kweli.
Ninasherekea kwasababu ninakumbuka siku ambayo sadaka ya
ukombozi ambayo ni Yesu Kristo alipozaliwa.
Katika Luka Mtakatifu
1:30 ninaona thamani ya Neno la kinabii
(Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulitokana na Neno la Kinabii).
(Wakristo wengi wanapoteza Baraka zao (miujiza) na hii
inatokana na kutokuamini sauti ya Mungu kupitia Mtumishi wake).
(Kitendo cha mimi kupewa unabii maana yake nimepata Neema
machoni pa Mungu , na hili limethibitishwa wazi katika Luka 1:30).
Jambo hili ni la kuwa nalo makini sana inabidi nipambane
katika kuikuza imani yangu ,kwasababu
nikipewa Unabii na wakati huo huo imani yangu iko chini ninaweza
kujikuta nimepeperusha muujiza
wangu,kwahiyo ili Neno la Kinabii liyabadilishe maisha yangu inatakiwa nifanye mambo yafuatayo:-
A)Kufanya mwendelezo wa kuongezeka kiimani .
B)Kuulazimisha moyo wangu kukubali hali ya kufundishwa Neno
la Mungu
C)Mimi binafsi kuruhusu ndani mwangu hali ya kukua kiimani .
UFAFANUZI KUHUSU KIPENGELE ‘A’.
Maana ya neno
mwendelezo ni kutia bidii ya
kujikumbusha na kurudia mara kwa mara
kile kitu ambacho tayari nimesha fundishwa kuhusu Mungu ,kwa mfano katika hali
ya uhalisia ninapopanda mti nikauacha
bila kuuwekea mazingira ya kupata lishe Je! Utakuwa?
Mzaingira yatakayofanya
mti ukue uwe na afya njema ni haya:-
I)Mbolea
II)Maji
III)Kuzungushia majani makavu katika shina ili yatunze
unyevu wa umande.
(Jinsi ninavyomshukuru Mungu katika mwanga mdogo, mwanga
mkubwa utanizukia ).
Mkristo asiyetafuta mwendelezo wa kukua kiroho ni rahisi
akajikuta amemkufuru Roho Mtakatifu
(Mwendelezo katika maisha yangu ya kiroho ndio utakayo
yakomboa maisha yangu katika mitego ya
shetani)
Bila mimi binafsi kuruhusu hali ya mwendelezo wa kukua
kiimani ni vigumu kuushinda udhaifu nilionao.
1Timotheo 1:12…..inaonyesha
wazi madhaifu yaliyokuwa yakilitesa kanisa lakini kwa Neema ya Mungu likapata
ukombozi , na hii ni kwasababu likaruhusu hali ya mwendelezo wa kukua
kiimani katika maisha yao.
UFAFANUZI WA
KIPENGELE ‘B’
Lazima niruhusu moyo wangu kufundishwa Neno la Mungu , hii itanisaidia
masikio ya kiroho kusikiliza mwongozo wa
Mungu anaosema kuhsu mimi.
Ninapoenda kanisani lazima moyo wangu utamani kusikia kitu
kipya kitakachonipa hali ya mwendelezo wa kukua
kiimani ,hapo maisha yangu ya kiroho nitakuwa nimeyakomboa.
Kuruhusu moyo wanhgu kulisikiliza Neno la Mungu ni jambo la
thamanin sana kuliko fedha na dhahabu.
Moyo wangu ukipata ufahamu vizuri wa Neno la Mungu nitapata faida zifuatazo:-
I)Faida ya kwanza kuwa karibu na uwepo wa Mungu , hii itanisaidia kumiliki Baraka za
rohoni na za mwilini.
(Moyo wa mkristo
ukipevuka vizuri kuhusu Mungu maisha yake yataitwa haki)
II)Faida ya pili kina cha maarifa ya rohoni kitaongezeka ,
na hapo ndipo mwanzo wa kupata uwezo wa
kupambanua katika Roho ,na ndilo jambo la msingi ambalo waamini tunaliksda
kutoka kwa Mungu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni