Ijumaa, 10 Aprili 2015

NAMNA YA KUISHI KATIKA HAKI

UJUMBE WA LEO
10/4/2015
                                    NAMNA YA KUISHI KATIKA HAKI
Ili niweze kuishi katika haki ya Mungu ambayo ndiyo Mungu  anahitaji kuiona katika maisha ya wanaomwamini Yesu Kristo,inatakiwa nikubali mimi mwenyewe kupata hasara ya mambo ya kimwili kwaajili ya Mungu.


Nisipo kubali kupata hasara kwa mambo ninayoyapenda ambayo yapo kinyume na kweli ya Mungu ni vigumu Baraka za Mungu kuambatana na mimi.

(Ukweli ni kwamba  nisipokubali kupata hasara katika mambo ninayoyapenda ni vigumu kupata mpenyo wa mafanikio).

                                                                  Warumi 14:15-19
Paulo Mtume alipoingia katika kanisa la Warumi alikuta jamii ya waaminio wakihukumiana kwaajili ya vyakula kama ilivyoandikwa Warumi 14:17,Lengo kuu alilokuwa nalo Mtumishi  wa Mungu ni kuifanya jamii ya waaminio kuwa na msingi katika Neno na si kuhukumiana katika vitu vinavyoonekana.

(Siku zote vitu vya mwilini havina utukufu kwa Mungu).

(Nikiwa nina imani na maneno ya Mungu ,Mungu ataongea na mimi waziwazi).

Inatakiwa niitumie Biblia kutatua  matatizo yaliyonizunguka, kwasababu Biblia ni sauti ya Mungu mwenyewe Yohana 1:1-3.

Nikitaka kuishi maisha ya hakilazima niliatamie Neno la Mungu,kwasababu nguvu ya kushinda kila aina ya udhaifu ipo ndani ya Neno la Mungu.

Neno la Mungu linafanya kazi ndani ya mtu kutokana na imani aliyonayo katika Neno hili.

Ukiona umeombewa ukawa bado hujapokea uponyaji ni picha wazi kwamba bado kiwango cha imani yako  kina udhaifu,kwahiyo hakina uwezo wa kukabiliana na jambo hilo,hapo inatakiwa niongeze bidii katika kujiongeza kiufahamu wa Kibiblia.

Ili mabadiliko yaweze kutokea kwenye maisha ya mtu lazima moyo wa mtu huyo ukubali mafundisho ya Neno la Mungu.

Moyo wangu ukikubali mafundisho ya Neno la Mungu ndipo hatua za mabadiliko zinakoanzia,Hata kitabu cha Mithali kimesema wazi Mithali 1:8-9.

Watu wengi hatujibiwi maombi yetu ingawa tunasikiliza na kuyasoma,sababu hii inatokana na jamii kubwa ya waaminio hawana tabia ya kutendea kazi Maandiko Matakatifu.

(Kuishi maisha Matakatifu kuna raha yake,
MFANO-Kutambulika kwenye uso wa Mungu kwamba hata mimi ni sehemu ya Ufalme wa  Mungu Yohana 1:12).

(Maisha ya dhambi ndiyo yanayotunyima kibali cha upendeleo kwenye uso wa Mungu). 

(Haki ndiyo inayoleta kibali kwenye maisha ya mcha Mungu).


Nikiwa kama mwamini inatakiwa muda wangu mwingi niutumie katika kubuni mbinu mbalimbali za kumpendeza  Mungu,hii itanisaidia kunisogeza karibu na uwepo wake.

Hakuna maoni: