AMINI KATIKA NENO LA MUNGU
Inatakiwa niamini katika Neno la Mungu, kwasababu Neno la
Mungu ndilo chimbuko halisi la Yesu
Kristo, hii ina maana zaidi Yesu Kristo ametokana na Neno la Mungu tunalolisoma
kila siku,hata Maandiko yanathibitisha
maneno haya Yohana 1:14
Kwanini ninasisitizwa niamini katika Neno la Mungu ni
kwasababu chimbuko la vitu vyote yaani duniani, chini ya nchi, mbinguni vimetokana na
na Neno la Mungu , kwahiyo nikiiendeleza roho yangu katika Neno la Mungu
nitapata faida nyingi sana na moja ya faida hizo kuurithi ufalme wa Mungu.
Mfano katika hali ya kibinadamu:Mtoto anapopelekwa Shule
lengo kuu la mzazi ni kumuendeleza mtoto wake kiakili apate elimu itakayo mheshimisha katikati ya
jamii na kuitwa mheshimiwa fulani , vilevile na kupata maisha ya duniani yaliyo
bora
SWALI: Je! kujiendeleza
zaidi kiroho hauoni utapata faida iliyo bora zaidi ?.
Maana kuu ya Yesu kuzaliwa katika mwili ni kurejesha kile
kizazi ambacho kilishamuasi Mungu ili kiishi katika haki na kweli.
Huu ni ukweli usiobadilika na haupingiki kamwe yaani kila
mwanadamu mwenye mwili atahukumiwa na
Neno la Mungu (Biblia).
Nisipo yaamini manen o ya Mungu kamwe siwezi nikaikwepa
hukumu ya milele ,kwasababu Neno la Mungu
ninalolisoma kila siku na
kulisikiliza ndani yake kuna pumzi hai, ndiyo maana lina uwezo wa kuponya
,kuokoa na kumrithisha mwamini uzima wa milele , hata Biblia inayathibitisha
wazi maneno haya Waebrania 4:12.
Hii ni picha wazi kwamba Neno la Mungu linanijua vizuri
sana hata kama mimi ninalisoma.
Neno la Mungu ndilo limeleta muunganiko kati ya mwanadamu mwamini na Yesu Kristo , hii ina maana kwamba hauwezi
kusema unamwamini Yesu Kristo kama kwanza hauliamini Neno la Mungu, vilevile
hauwezi kusema kwamba unaliamini Neno la Mungu
alafu haumwamini Yesu Kristo.
(Ni vigumu kusema ninayaamini Maandiko Matakatifu (Biblia)na
wakati huohuo sijamkiri Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu, hiyo
imani haitoki kwa Mungu aliyeiumba mbingu na nchi, kwasababu Yesu Kristo
ametokana na Neno , vilevile wokovu wa kuurithi Ufalme wa Mungu unatokana na
Yesu Kristo, Je! Hapo kama mkristo unatafakari nini?).
Mkristo kama hajaokoka yaani hajamkiri Yesu Kristo kuwa
Bwana na mwokozi wa maisha yake hawezi kusema anamjua Mungu wala ni sehemu ya Ufalme wa Mungu, kwasababu
Maandiko yanathibitisha neno hili katika kitabu cha Warumi10:9, vilevile kitabu cha Wafilipi 2:8-11.
Inatakiwa niende kanisani kwa kutamani kubadilika katika
tabia niliyonayo , kwasababu Neno la Mungu ndilo lenye nguvu ya kung’oa asili
yaani tabia aliyonayo mtu.
Neno la Mungu likiielimisha roho ya mwamini ufahamu wa
mwamini huyo ukakua , hapo ndio utakuwa mwanzo wa huyo mwamini kuishi katika
haki.
Inatakiwa nibadilishe mfumo wa maisha yangu nguvu
nyingi nguvu nyingi ninayoitumia katika
kutafuta pesa inatakiwa niitumie katika kumtafuta Mungu,kwasababu pesa sio
upako, ila upako ndio unaov uta pesa ,hata Maandiko yamethibitisha maneno haya Isaya 60;11,16.
Nisipoliamini Neno la Mungu maana yake nimefarakana na Baraka
za Mungu waziwazi.
Jambo la kujua kama mkristo ninayemwamini Yesu Kristo,lolote lililompata Yesu Kristo mimi
kama mwamini sitaliepuka ila tunitahitaji Neema
ya Mungu isababishe wepesi wa kuvuka .
Katika safari ya kumcha Mungu katika kweli na haki yaani
kwenye misingi ya wokovu inatakiwa nikubali kupata hasara ya kila kitu ndipo safari
yangu itafika salama.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni