AMINI KATIKA NENO LA MUNGU
SEHEMU YA PILI
Neno la Mungu inatakiwa lianze kujengewa mizizi ndani ya
familia yangu ikiwa bado ni changa , hiyo itasaidia katika kile kizazi
kinachotoka katika familia yangu kukua katika misingi ya kuamini zaidi katika
Neno la Mungu .
Familia yangu yaani watoto wangu nikiwajengea mizizi ya
kumcha Mungu katika roho na kweli siku za usoni .
Neno la Mungu inatakiwa lianze kufundishwa katika ngazi ya
kifamilia na hilo ni jukumu la baba na
mama , na hapo ndipo wanapojiandalia familia yenye hekima na busara au familia
ya wapumbavu, katika suala hili kunahitajika umakini wa hali ya juu sana
kwasababu wale watoto mnaoanza kuwajenga
kwenye mazingira ya kumcha Mungu na
ambayo ni hatua ya kwanza , hatua ya pili ni kwamba watoto inatakiwa wayashuhudie
matendo mema na maneno yenye hekima na busara katika vinywa vya wazazi wao.
Mzazi akiwa ana tabia ya kunena maneno yaliyoko kinyume na
mapenzi ya Mungu au kufanya matendo yasiyompendeza Mungu. Mfano wa matendo ;Baba kumpiga Mama watoto wakiwa wanaona au Baba
kumtukana Mama watoto wakiwa wanasikia , na wakati huohuo watoto wanaona
mnashiriki katika mafundisho ya Neno la Mungu kanisani na mnaleta Wachungaji nyumbani na
wazazi hamna mabadiliko yoyote , maana
yake mnaandaa kizazi cha nyoka kwenye familia yenu na ambacho kitakuwa
kimefunikwa na jina la Yesu Kristo juu lakini ndani ni mbwa mwitu.
Inatakiwa nichunge sana kufanya makosa kwa namna yoyote ile
mbele ya mtoto akiona , kwasababu mimi ndiye mwenye dhamana ya kuijenga familia
yenye ufahamu na familia isiyokuwa na ufahamu
1Yohana 1:1-6.
Ninaipenda sana injili ya Yesu Kristo , kwasababu Kristo
ndiye ambaye ameleta Neema na kweli , yaani ndiye ambaye ameleta wokovu
utakaouturithisha Ufalme wa Mungu ndio maana dunia haikuishia kipindi cha Musa,
lakini dunia itaishia katika kipindi cha
Yesu Kristo hakuna mwingine tena Yohana
1:16-18.
Nikiisoma Biblia au nikakaa chini nikasikiliza Neno la Mungu nikiwa bado
sijaokoka hiki kitabu kitakuwa kwangu ni historia yaani hakitakuwa na msaada na mimi , kwasababu jina
la Yesu Kristo linafanya muujiza wowote ule kwa mtu ambaye amejiunganisha na wokovu ni Yesu Kristo , ndiyo maana 1Wakorintho 6:17 imefunua jambo hili wazi.
Nikiwa ni mkristo ninayeenda kanisani kila siku lakini bado
sijamkiri na kumwamini Yesu Kristo maana yake sijaokoka kibiblia ninaitwa mtu
ambaye sio roho moja na Yesu Kristo, ndio maana watu wengi wanaishia kwenye
mataabiko ,Kivipi? Wanataka uponyaji
lakini hawataki kumwamini kwamba yeye ni mwokozi wa maisha yao.
Katika suala zima la kijiendeleza kiufahamu kunahitajika haekima ya Neno la Mungu katika
maisha ya mtu, kwasababu Neno la Mungu ndilo limepewa dhamana na Mungu katika
kuyajenga maisha ya mkristo na
kuyaimarisha kiroho.
Nikitaka makusudi ya Mungu yathibitike kwenye maisha
yangu mimi inatakiwa niambatane na Neno la Mungu yaani tuwe wamoja , na ili niweze kujitambua mimi binafsi kwamba
maisha yangu yameambatana na Neno la
Mungu kuna mambo haya yatajitokeza
kwangu:-
A)Sitapenda muda mwingi upite bila kushika Biblia kusoma.
B)Nitakuwa mtu ambaye wakati wangu wa kuomba ninasimamia
Maandiko yaliyoandikwa ndani ya Biblia.
C)Nitajitahidi kuwa mtu ambaye wa kuhudhuria mafundisho na
kutokukubali kupitwa na mwongozo wowote
ambao kiongozi wangu wa kiroho anautoa .
Nikisema ninamwamini Yesu Kristo na kumkiri na wakati
huohuo bado nina matendo ya giza kibiblia
ninaitwa mnafiki.
Inatakiwa nijitahidi kuliishi Neno la Mungu ili nipate
kibali ndani yake cha kuyaishi maisha Matakatifu, vilevile kushinda madhaifu
mabalimbali.
Jambo la kufahamu Neno la Mungu lina rekodi ya maisha ya kila mwenye mwili , ndio maana lina uwezo
wa kumponya mtu, lin uwezo wa kufufua , lina uwezo wa kubariki , vilevile lina
uwezo wa kumrithisha mtu ufalme wa Mungu hii yote inatokana na Neno ndiye Mungu mwenyewe Yohana 1:1-3.
Neno ana mamlaka ya kila kitu lakini anafanya kazi na mtu anayemwamini Yesu kristo , kwasababu
Yesu mwenyewe ni sehemu ya huyo Neno Yohana
1:14.
Katika nyakati zilizopita yaani za Agano la kale utukufu wa Neno ulionekana katika mazingira
ya kimwili , ndio maana hata wakina Petro, Yohana na Yakobo walitembea na
Yesu wakapanda mitumbwi wote pamoja
wakaenda Getsemane bustanini kuomba walikuwa
katika mazingira ya kimwili , baada ya hapo Yesu alivunja nguvu ya Agano
la kale na kuivalisha Agano jipya nguvu
, hata maandiko yanathibitisha katika Waebrania 7:21-22, Waebrania 8:6 na
Waebrania 12:23-25.
Nikifundishwa Neno la Mungu na mtu ambaye naye ameenda darasani kusoma neno hilo litakuwa na mapungufu makubwa sana Kivipi? Litakuwa halitoki katika
mtiririko wa Roho Mtakatifu, bali
litakuwa linatoka katika ufahamu wa kishule,na wote tunafahamu ufahamu wa
kishule ni kuiendeleza akili , bali
ufahamu wa Roho Mtakatifu ni kuiendeleza roho , kwahiyo ikiwa mimi ni mkristo
niliyeokoka kweli ninahitaji kusimama na
Mungu inatakiwa nikae chini ya Mtumishi
wa Mungu anayeongozwa na Roho Mtakatifu
katika kitabu cha Warumi kimeyafunua zaidi
Warumi 8:14.
Wakristo wengi wameshindwa kuimarika katika misingi ya
kiimani na roho zao zimebaki na hali ya upweke , kwasababu mafundisho
wanayojengwa nayo ni ya historia na siku
zote historia haina uhai ndani yake ya
kutengeneza wazo jipya, ndio maana
maisha ya walokole wengi yamedumaa, na hii inatokana na kufundishwa historia
tu.
Injili ya Yesu Kristo
inatupa mwanga na ufahamu wa
namna ambavyo tutaitimiza wokovu katika haki na kweli , ndio maana Biblia
ikasema katika Waebrania 12:24.
TAHADHARI
Inatakiwa niyachunge maisha yangu ya
wokovu nisije nikayachanganya na
watu ambao wanaopinga kazi za Roho
Mtakatifu lakini unaweza kukuta saa zingine
ni viongozi wa kiroho au ni watu
ambao waliokoka muda mrefu, kwanza
nifahamu kazi za Roho Mtakatifu:-
i)Uponyaji katikati ya kundi
ii)Ishara katikati ya kundi
iii)Miujiza katikati ya kundi
iv)Mafunuo ya Neno la
Mungu
v)Madhihirisho yote ya Roho Mtakatifu maana yako mengi sana
, kwahiyo nitakapokuta mahali popote hata iwe kwenye nyumba ya ibada kazi za
Roho Mtakatifu zinapingwa sehemu hiyo
inabidi niikimbie maana ina laana
Je laana inatokana na
nini?
Laana inatokana na kupinga maneno yaliyotoka katika kinywa
cha Yesu Kristo Yohana
14:12,Yohana21:25, Marko 16:17, kabla hujapinga kazi za Roho Mtakatifu hakikisha umesoma Biblia na
umeielewa.
Watu wengi tunashindwa kulitumia jina la Yesu Kristo kutuletea mabadiliko na kutubariki , kwasababu bado hatujawa na imani ya kuamini kwamba tunamwamini Yesu ingawa tunasema tunaamini , na chanzo cha matatizo hayo
yote ni kukaririshwa historia ya Biblia.
Watu wengi maisha yao yanalaanika , kwasababu wanatabia ya
kupenda kusikiliza sana maneno ya watu
ambao wanapinga kazi za Roho Mtakatifu, kwahiyo hujikuta na wao wameshaingia
katika ule mkumbo , ndio maana hata idadi ya vifo inaongezeka kila siku kabla ya wakati wa umri ulioandikwa kwenye Biblia .
Imani ni msingi wa maisha ya mkristo anayetumainia siku moja
kuurithi ufalme wa Mungu , kama mimi ni mmoja wapo kati ya wale wenye matumaini inatakiwa nifanye mambo yafuatayo:-
A)Niwe mtu mwenye kupenda
kusikiliza Neno la Mungu na
kuhudhuria vipindi vya kanisani .
B)Niwe mtu mwenye kupenda kujisomea Biblia na kupenda
kujisomea vitabu mbalimbali vya Watumishi wa Mungu waliotumika na Roho
Mtakatifu.
C)Niwe mtu mwenye mbinu mbalimbali za kujiongeza kiufahamu
kwasababu hali ya kujiongeza ndiko
kunakotokea tendo la ukuaji wa kiroho (kiimani)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni