Jumapili, 15 Februari 2015

TUNZA MAMLAKA ULIYOPEWA

UJUMBE WA LEO
15/2/2015
TUNZA MAMLAKA ULIYOPEWA
Ili niweze kutunzaq mamlaka  niliyokabidhiwa na Yesu Kristo inatakiwa nifanye mambo yafuatayo:-
A)Nijifunze Neno la Mungu (Biblia)
Kuhusu kujifunza Neno la Mungu inatakiwa liwe ni jambo lenye mwendelezo , kwasababu jinsi ninavyozidi  kujifunza ndivyo  ninavyopata kina  cha kumjua Mungu.


(Mamlaka aliyonayo mtu inahitaji nguvu ya Neno la Mungu ili iweze kuwajibika )

(Nikimjua Mungu mamlaka niliyopewa nitakuwa   na uwezo wa kuitunza)

Watu wengi sanasana jamii ya waaaminio wanashindwa kutunza mamlaka , kwasababu hawana muda wa kutosha  wa kujifunza Neno la Mungu.

B)Nijitahidi  kujisomea Neno la Mungu mara kwa mara
Nikijisomea Biblia kutanisaidia kuniwekea ulinzi vilevile kutanisaidia mbinu za kudhibiti aina mbalimbali za majaribu, kwasababu ndani ya kujisomea Biblia ninapata ufahamu wa kujua shetani pamoja na mbinu zake anazotumia kuathiri maisha ya waamini (Wakristo).

(Kama sina muda wa kusikiliza Neno la Mungu , vilevile muda wa kujisomea  Biblia nijiandae kuwa jalala la matatizo, kwasababu  ndani mwangu sitakuwa na mbinu yoyote ya kumkabili shetani , kwa hiyo ni rahisi yeye kupenya na kuleta kila aina ya madhara , Sababu sina kinga yoyote).

(Kuna matatizo mengine yanayotukumba kwasababu sisi wenyewe tunajitenga mbali na uso wa Mungu).

Neno la Mungu ni kiunganishi kinacho zaa imani ambayo inamfanya Mungu kujua uzito wa tatizo la mwamini .

Wakristo wengi wana shida hii,wakati wa tatizo linaanza hawaoni umuhimu wa kumtafuta Mungu, lakini wakati wa tatizo limeshakuwa kubwa yaani haliwezekani  tena ndiyo wanamtafuta Mungu , Je!kuna kuponywa hapo?

Mungu anahitaji mwamini ambaye amefanya  maandalizi ya imani yake kabla ya kuingia kwenye uso wake kuomba .
Yakobo 5:17-18

Kuiandaa imani yangu kabla ya kuingia kwenye maombi kutanisaidia kunipa utulivu  ndani ya moyo , vilevile kutanirahisishia  hali ya wepesi  wa mtiririko  wa Roho Mtakatifu katika hoja ninazopeleka  kwenye uso wa Mungu.

Kushinwa kwangu kunatokana na hali ya kutokuiandalia mazingira imani yangu ya kupokea kitu kutoka kwenye uso wa Mungu .

Sauti ya Mungu tunaisikia kupitia kwenye mlango wa ufahamu wa moyo wa mtu , ndio maana tunahitaji utulivu wakati wa kuomba
Mathayo 6:7.

(Kama sina utulivu kwenye moyo haitakiwi niombe , kwasababu nitakuwa najitaabisha bure).

Ninasisitizwa kusoma Biblia ili ufahamu wangu ujengwe katika hekima ya Kimungu.

Mwamini ambaye ni msomaji wa Biblia kinywa chake kinayo mamlaka ambayo ina uwezo  wa kusababisha  chochote kutokea muda wowote, ndio maana  tunahitaji kutamkiwa neno na kinywa chenye mamlaka.

Nikiamini neno ninalotamkiwa kutoka kwenye kinywa chenye mamlaka  linakuwa lina asilimia zote kudhibitika , kwasababu katika  mamlaka kuna  nguvu ya neno  nyuma yake inayolazimisha  jambo kuumbika.

Maisha ya wakristo yamekuwa magumu, kwasababu  wanashindwa kuitumia mamlaka waliyonayo, nah ii mara nyingi hutokana na vifungo vya dhambi wanazojikwaa kila iitwapo leo.

Nguvu ya dhambi mara nyingi huunyima moyo wa mwamini uhuru wa kuamini kile anachoomba kwenye uso wa Mungu kwamba kitajibiwa.

Mamlaka iliyo ndani ya mtu huathiriwa na mtu anavyozidi kujikwaa katika dhambi .

KAZI YA MAMLAKA
Mamlaka inayo kazi kubwa sana ndani ya mtu,kwasababu  ndio inayolazimisha mambo mengine magumu kudhibitika hata kama sio wakati wake.

(Uovu wangu ndio unaoninyima ujasiri wa kuitumia mamlaka niliyonyo kutnda kazi).

(Nikishakuwa na uwezo wa kusimama mbele ya adui  yangu bila hofu maana yake nimeshinda).

Tuepuke kukiri udhaifu , kwasababu jinsi ninavyokirik udhaifu ndivyo ninavyofungua malango wa kuathiriwa  jumla.

Ninavyokiri kushindwa ndivyo ninavyoathiri mfumo mzima wa Baraka za Mungu katika maisha yangu, vilevile mamlaka yangu ninaipotezea uwezo wa kuniumbia mambo mengine  kudhibitika , lazima nikubali kubadilisha ukiri wangu.

(Kama ninavyoweza kusikia nikaamini, ndivyo ninavyoweza kunena ikawa).

Mamlaka humvusha mwamini katika mazingira magumu sana , hata kama mazingira hayo hayamsapoti
Luka 10:19.

Mamlaka ina kazi ya kumtiisha  shetani juu ya kitu chochote na akatii.


Kushindwa kwangu ni matokeo mabaya ya mahusiano kati ya mimi na Mungu, ndio maana shetani hupata mpenyo wa kuniathiri.

Hakuna maoni: