UJUMBE WA LEO
01/2/2015
NAMNA YA KUDHIBITI UDHAIFU NILIONAO
Kwanza kabisa kila mwanadamu mwenye mwili anao udhaifu ndani
mwake,lakini udhaifu huu huwa unatofautiana kila mmoja kwa jinsi yake .
Udhaifu ni hali fulani ndani ya mtu vilevile ni mapungufu anayokuwa nayo
mtu, wakati huohuo akiwa ana taarifa hiyo ndani mwake, kwa maana zaidi ni roho
anayopagawa nayo akiwa na akili timamu.
Udhaifu ni hali ambayo inaweza kuepukika iwapo mwamini
ameamua kufanya mabadiliko .
Udhaifu ni hali ambayo inaweza kuwa kipingamizi cha maombi
ya mwamini ,vilevile kizuizi cha kufanya majibu ya maombi ya mtu kuchelewa.
Bila kudhibiti udhaifu nilio nao ni vigumu kupata mpenyo,
kwasababu udhaifu huo unakuwa ni kibao kinachosimama mbele za Mungu na
kunishitaki .
Zaburi 51:3.
Waamini walio wengi wana bidii ya kumjua Mungu lakini hawana
bidii ya kupambana na madhaifu ambayo
ndio kikwazo kinachozuia wasimjue Mungu ingawa wanamtafuta usiku na mchana .
(Udhaifu ni kipingamizi kinachoyafanya maombi ya mtu
kutokujibiwa kwa wakati, kwasababu katika mahakama ya kiroho mwamini anapoanza
kuomba kitu kitu cha kwanza katika mahakama hiyo kinachotazamwa ni mwenendo
wake, kwahiyo mwenendo wako kwenye mahakama ya kiroho ndio ushahidi wa
wewe kujibiwa au maombi yako kuzuiliwa).
Mfano mzuri ni ni katika mahakama ya kidunia ;Hakimu hawezi kuhukumu kesi bila ushahidi
anaouthibitisha taarifa nzima ya mashatakiwa
Yakobo 2:23-26.
Mimi kama mwamini inatakiwa imani niliyonayo kwa Mungu
niiweke katika mazingira ya matendo ,kwasababu yale matendo ndio ushahidi wangu
mimi kwenye mahakama ya kiroho kwamba ninastahili kubarikiwa au sistahili kubarikiwa.
Kwenye mahakama ya kiroho ili nibarikiwe au nisibarikiwe ni
unatazamwa ule mwenendo wangu wa kila
siku,kwahiyo nikikutwa mwenendo wangu unaendana sambamba na imani yangu mbingu
inanibariki, ndio maana Biblia ikasema iamni pasipo matendo imekufa.
Udhaifu nilio nao lazima nijilazimishe mimi binafsi kupingana nao ndipo hali ya mabadiliko
itakapoanza kujitokeza.
Nikishapata ufahamu ya kwamba udhaifu nilio nao ni
kipingamizi cha maombi yangu yasijibiwe ndio mwanzo wa kuanza mikakati ya
kupindua utawala wa udhaifu huo ndani mwangu.
Kitendo cha mtu kutambua chanzo cha shida yake, hapo huwa
ndio mwanzo wa mtu kuingia katika hatua ya kushinda hali hiyo.
Kama udhaifu nilionao na hapohapo ninajitambua kwamba ninao, Basi hata
kuushinda inawezekana .
Wakristo wengi sanasana jamii ya waaminio wamepoteza Baraka zao
kwenye uwepo wa Mungu,kwasababu kuu mbili:-
A)Kukata tamaa ,
kukata tama inafunua wazi moyo wangu kwenye uso wa Mungu kwamba mimi ni mvivu
wa kusibiria , kwahiyo hata siku moja mtu wa hivyio maisha yake huwa hayana
mpenyo vilevile kibali mahali popote.
(Mtu mwenye hali ya kusuburia ndani mwake ana upendo ulio hai, kwa lugha
nyingine ana imani yenye matendo).
Kama ilivyo mwili pasipo roho umekufa basi, ndivyo ilivyo
imani bila uvumilivu haizai matunda
B)Kushindwa
kuamini kwamba alilolinena Mungu ni kweli
Jamii nyingi ya waaminio maisha yao yamekwama na sababu kuu
ya maisha yao kukwama wamekosa uvumilivu
wa kusubiri ahadi za Mungu.
Mfano Mungu akisema atanibariki badala ya mimi kuweka
maandalizi thabiti ya kumiliki Baraka zile ninaanza kunung’unika, kwahiyo ni
vigumu katika nafasi hiyo kubarikiwa.
HATUA YA KWANZA YA
KUDHIBITI UDHAIFU
Ili niweze kudhibiti udhaifu nilionao inatakiwa niuimarishe
ufahamu wangu katika Neno la Mungu.
Kwanini inatakiwa niimarishe ufahamu wangu ,ni kwasababu
ufahamu ndio unaopokea taarifa zote za moyo wangu
2Wakorintho 10 :3-5.
Bila mimi kuimarisha ufahamu wangu katika Neno la Mungu
itakuwa ngumu kumiliki Baraka za kiroho ambazo ndizo huyafanya maisha yangu ya kimwili
kuheshimika.
Mkristo mwamini
akiimarisha ufahamu wake katika Neno la Mungu huwa ana mambo
matatu:-
A)Mamlaka ya kuumba
B)Nguvu ya Rohoni
C)Upendo.
A)UFAFANUZI
KUHUSIANA NA MAMLAKA KWA UFUPI
Mamlaka ni hali Fulani ya nguvu ya Mungu inayoyavaa maisha
ya mtu aliyeimarisha ufahamu wake vizuri katika Neno la Mungu,vilevile ni uwezo
anaoupata mtu kutoka katika serikali ya mbinguni kupitia Maandiko Matakatifu
a,mbyo ndio katiba ya kiroho, lakini katiba hii hainaga mapinduzi.
(Katiba ya kiroho ni Neno la Mungu (Biblia).
Hiki kitu ni cha kuwa nacho makini sanan majivuno yanaathiri
mfumo wa ufahamu sana , kwahiyo ili niweze kuepuka hilo inatakiwa niwe mtu wa
kutaka kujua kitu kila siku kutoka kwenye Neno la Mungu, hapo nitakuwa
nimeuokoa ufahamu wangu, ndio maana katika kitabu cha Yakobo amesema neno hili
Yakobo 4:13-17.
Kukuza ufahamu wangu kwa kusoma Maandiko Matakatifu ni jambo
la muhimu sana , kwasababu hatua za kuyaishi maisha Matakatifu,Maisha ya Baraka,
Maisha yenye faida kwa Bwana, zinaanzia pale ambapo ufahamu wangu
umepevuka.,Jambo hili lilimkuta Mtumishi wa Mungu Danieli,
ufahamu wake
ulipevuka kwa kusoma vitabu ,akatambua nyakati amabzo Neno la Mungu lilinjia
Yeremia NabiiDanieli 9:1-3.
Ufahamu wangu utaongezeka kadri nitavyotia bidii ya kusoma
Maandiko Matakatifu.
Ili nikue kiufahamu na nizae matunda yaliyo bora inatakiwa
nijifunze kwa Yesu Kristo.
Nikiukuza ufahamu wangu kupitia Maandiko Matakatifu kumbukumbu yoyote
ya dhambi ambayo tayari nimekwisha itubu
kwenye uso wa Mungu itafutika na hapo kutazaliwa hatua zaidi za kuimarika kiroho.
Kumbukumbu ya mambo yaliyopita kwenye maisha ya mwamini mara
nyingi huwa inaathiri ukuaji wa ufahamu wa amkristo, kwasababu kitendo cha
kukumbuka jambo ambalo Mungu amekwisha
kunisamehe na nimekwisha kulitubia ninamfanya Mungu kuonekana muongo, ndio maana akatoa tahadhari kupitia kitabu cha Isaya 43:18.
(Nikiona nimeanza kuona aibu juu ya jambo lolote
ninalomkosea Mungu au dhambi
ninayoifanya kwa siri nijue wazi maisha yangu Mungu ameshaingilia kati ,
kwahiyo inatakiwa nitie bidii kuudhuria ibada na wakati huo huo nikitarajia
mabadiliko).
Nikiyang’ang’ania mambo yaliyopita na kuyarejesha
kwenye ufahamu wangu kuendelea kuyawazawaza ninaonyesha jinsi nilivyo
mchanga kiroho, kwahiyo ni vigumu sana mtu wa aina hiyo kuzishiriki Baraka za
Mungu.Udhaifu wowote ulioko juu ya maisha ya mtu ataushinda pale atakapo amua kusoma Maandiko
Matakatifu, vilevile na vitabu ,mbalimbali
vilivyoandikwa na Watumishi wa Mungu wenye nguvu, hata Danieli Biblia
alitambua nyakati za Neno la Bwana
lilivyomjia Nabii Yeremia kwa kusoma vitabu, hii inaonyesha ni Maandiko
Matakatifu vilevile ni vitabu vilivyoandikwa na manabii waliopita.
B)UFAFANUZI MDOGO
KUHUSIANA NA KIPENGELE ‘B’ NGUVU YA
ROHONI.
Nguvu ya rohoni inayavaa maisha ya mwamini pale ambapo
mwamini huyo ameamua kusoma Biblia, vilevile kusikiliza Neno la Mungu.
Nguvu ya rohoni ni jambo la muhimu sana sanasana katika
maisha ya jamii ya waaminio , kwasababu mapambano au vita vya waamini na
shetania hufanyika katika roho, kwahiyo kuvishinda vita hivyo inatakiwa niwe imara katika nguvu ya rohoni, ndio maana Biblia ikasema
katika kitabu cha Waefeso 6:10-15.
Nivigumu kuushinda ulioko juu yangu kama sina uwezo wa
kutawala katika roho,kwasababu nguvu ya udhaifu
inaanzia katika roho, ndio maana Kitabu cha Waefeso 6:12 kimesisitiza kwamba
vita vyetu ni vya kiroho.
Wakristo wengi wanashindwa na madhaifu yaliyowakalia
kwasababu ya upungufu wa kina cha Neno la Mungu ndani yao, na upungufu huo huwa
unaondoa kibali kwenye maisha ya mtu.
Kibali kikiondoka katika maisha ya mtu ataandamwa na mambo
yafuatayo:-
i)Magonjwa
ii)Kukataliwa
iii)Kufilisika kiroho na kimwili
iv)Kuandamwa kila
baya hata kama hakuusika atalazimishwa
kahusika.
Kibali ndiyo mafanikio.
Maoni 1 :
Maisha yangu Maajabu yanashangaza ushuhuda, Jinsi nimepata kisanduku chenye nguvu sana ambacho sasa ni pesa yangu mara mbili kutoka mia hadi elfu ya pesa ndani ya masaa 24, na pia jinsi nimerudisha mpenzi wangu wa zamani, sababu kuu niliwasiliana na Dk Lomi kwa msaada mimi kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, basi ananisaidia ni nguvu kubwa ya kumrudisha mpenzi wangu wa zamani, na ananipenda na ananithamini sasa, basi mimi na Dr Lomi tukawa marafiki, baada ya mazungumzo kadhaa namuuliza ikiwa kuna njia anaweza kuniganga ili nipate pesa, hapo ndipo aliponiambia juu ya sanduku hili la uchawi, akaniambia kuna aina na saizi tofauti ya sanduku, aliniambia aina zote za sanduku, ningeweza kumudu ndogo tu ya sanduku, baada ya maombi muhimu anayofanya kwenye sanduku, ananipeleka kupitia huduma ya kujifungua, aliniambia niweke pesa ndani, niliweka ndani ya sanduku 100 euro baada ya masaa 24 nikagundua ilikuwa elfu 10 euro ndani, na nimekuwa nikitumia sanduku kwa miezi 7 sasa, mimi na mchumba wangu tunaishi maisha bora, ikiwa unahitaji b ack mpenzi wako au pesa spell wasiliana na Dr Lomi kwa barua pepe: lomiultimatetemple@gmail.com au WhatsApp namba +2349034287285 unaweza pia kumwandikia kupitia Jina la Mtumiaji la Snapchat: drlomi20 atakusaidia nje, asante kwa kusoma,
Kwaheri Gerd Ulrich
Chapisha Maoni