Jumapili, 25 Januari 2015

JIMIMINE KWENYE NENO : SEHEMU YA TATU

UJUMBE WA LEO
25/1/2015
JIMIMINE KWENYE NENO
SEHEMU YA TATU
II)UJASIRI
Ujasiri ndani mwangu utakuwepo pale ambapo moyo wangu utaamini katika kile ninacho jiamini nacho.

Siku zote ujasiri unapotea juu ya kitu  ambacho sina uhakika nacho.


(Shetani anatumia udhaifu  wetu wa hofu  kuyaathiri maisha yetu ,juu ya jambo hili lazima niwe makini)

(Mimi  ninayelitumia jina la Yesu Kristo sipaswi kuwa muoga kwenye uwanja wa mapambano ,kwasababu kwenye uwanja wa mapambano kuna mambo makuu mawili
a)Kushinda
b)Kushindwa,kwahiyo hali yoyote nitakayoionyesha  ninapokuwa kwenye uwanja wa mapambano ndio matokeo nitakayoyapata)

Siku zote kinachotesa maisha ya waamini Mungu sawa lakini hawana ujasiri wa kukabiliana  na changamoto katika uwanja wa mapambano ,ndio maana hupata matokeo kimyume na vile wanavyoamini ,hata Biblia imeyathibitisha  1Yohana 4:18.

(Hofu ikitanda kwenye moyo wangu hata kile ninachokiamini kitayeyuka).

Kuna silaha moja kuu na hii ndio itakayoweza kutupa ushindi kwenye uwanja wa mapambano  na silaha hiyo ni upendo , kwasababu ndani ya upendo tunapata  mambo kadha wa kadha :-
i)Tunapata msamaha Warumi 12:19-21
ii)Tunapata Imani Waebrania 11:1,6,8,11 na 17
iii)Tunapata uvumilivu  Mathayo 10:22
iv)Ujasiri 1Yohana 4:17.

Silaha ya kushinda vita vya kiroho ni upendo,cha ajabu neno upendo huwa hawaoni ni kitu cha maana kwenye maisha yao.

Mwamini ambaye hasamehi huyo haishi na Mungu.

Maisha ya visasi ndiyo yanayowafanya wakristo waamini kushindwa kwenye uwanja wa mapambano, kwasababu katika visasi hamna  upendo vilevile hamna imani.

ANGALIZO:Lazima nitambue maisha ya visasi , kutokusamehe,hofu,woga,wasiwasi,mashaka                                  hayana Baraka kwa Bwana ,kwahiyo nahitaji mabadiliko haraka sana.

Kama sina uvumilivu katika imani yangu siku zote nitakuwa mtu wa kushindwa.

Uvumilivu ndio unaoimarisha misuli ya ujasiri kwenye imani ya mwamini  kwahiyo ili niwe mtu wa kushinda popote pale ninapokutana na changamoto  inatakiwa niboreshe  zaidi mambo yafuatayo  katika maisha yangu :-
a)Mahusiano na Neno la Mungu (Biblia)hapa ndipo chimbuko la utawala katika roho linapoanzia.

Inatakiwa niyaishi maneno ya Mungu yaani niyatendee kazi maandiko ninayoyasikiliza kila siku kanisani , ndipo neno la Kinabii  ninalotabiriwa na Mtumishi wa Mungulitatimia juu yangu.

(Wokovu ndiyo mpango wa Mungu  kwa wanadamu wote wenye mwili).

1Yohana 4:17 ni picha wazi ya kwamba Yesu Kristo aliyaishi maisha ya utakatifu humuhumu  ulimwenguni,kwahiyo nikitaka niyaishi maisha aliyoyaishi Yesu Kristo  inatakiwa niboreshe mahusiano yangu na Neno la Mungu  ndipo nitakapoweza kuyatimiza yaliyoandikwa humo.

Mahusiano yangu na Neno la Mungu yataniponya sehemu zifuatazo:-
1)Nitaponywa Ufahamu
2)Nitaponywa Akili
3)Nitaponywa Moyo , na hiki ndio kiungo kikuu  sana kinacholeta madhara hata Biblia imeyathibitisha haya Yeremia 17:9.

Mwenye uwezo wa kuutawala moyo wake ni Yule  anayesoma Biblia kupita kiasi.

Ili utumishi wangu usilaumiwe inatakiwa nitie juhudi nyingi  katika usomaji wa Biblia ,kwasababu usomaji wa Biblia utanisaidia kina cha maarifa ya rohoni kufunguka , kwahiyo hapa ndipo nitakapopata  ufahamu wa kupambanua  ndani mwangu neno lolote  ninalolisikia ndani mwangu  kabla ya kulitamka.

Kila neno ninaliolitoa katika kinywa changu inatakiwa lihakikishwe na Neno la Mungu ambalo tayari nimeshaliamini  moyoni mwangu ili nisiwe kikwazo kwa wanaolisikia  bali liwe msaada, kwahiyo kinywa changu kitaitwa kinywa chenye hekima  sambamba na Maandiko Mtakatifu  katika kitabu cha  Malaki 2:7.


Kile ninachokitoa kwenye kinywa changu ndicho kipimo cha imani  niliyonayo ,kwahiyo nikilitambua hilo inatakiwa niwe na bidii sana kwenye kusoma Biblia ili kuongeza maarifa zaidi. 

Hakuna maoni: