UJUMBE WA LEO
18/1/2015
JIMIMINE KWENYE NENO SEHEMU YA PILI
HASARA ZA
KUTOKUJIMIMINA KWENYE NENO LA MUNGU
Kutokujimimina kwenye Neno la Mungu maana yake ni kutokuupa moyo wangu uhuru wa kuambatana na
Neno la Mungu .
Mkristo mwamini jinsi anavyounyima moyo uhuru wa kufundishwa
Neno la Mungu ndivyo anavyozidi kujiathiri katika maeneo muhimu yafuatayo katika maisha yake :-
i)Afya njema
ii)Uchumi
iii)Mahusiano na Jamii
iv)Ndoa. ,haya ndiyo maeneo muhimu sana katika maisha ya
mwanadamu yatakasyoathirika pale ambapo
mwanadamu huyu atakataa kuongozwa na
ufahamu wa Neno la Mungu.
Mkristo mwamini akiruhusu maisha yake yaongozwe na ufahamu
wa Neno la Mungu
(Biblia)mawazo yake yataendana
sambamba na mawazo ya Mungu,kwahiyo mkristo huyu ndani mwake kutatoka
mambo yafuatayo:-
i)Hekima
ii)Busara
iii)Nidhamu
iv)Utii,kwahiyo mtu wa aina hii anaitwa mkristo
aliyeyalingana mapenzi ya Mungu.
Siku zote aliyeyalingana mapenzi ya Mungu kitokacho ndani
mwake ni msaada kwa jamii inayosikia
,ndiyo maana Biblia inatusisitiza sana kuimarika katika imani na pia imenena kitu kwa mtu anayeishi katika
misingi ya kiimani,mbona hata Biblia imeyafunua haya katika kitabu cha Warumi 1:17.
(Imani ndiyo inayonitengenezea mazingira ya mimi mwamini
kupata kibali kwenye uwepo wa Mungu)
Ili roho ya Bwana isigeuke idumu na mimi siku zote inatakiwa
nijijunganishe na Neno la Mungu (Biblia).
Hasara nyingine inayoweza kutokana na kutokujimimina kwenye Neno
ni hali ya kuvamiwa katika roho ,hali hii ya kuvamiwa katika mazingira
ya ndoto, vilevile magonjwa mengi yanayowatesa jamii ya waaminio huanzia katika
ndoto.
MFANO:Ninaota
nakula nyama mbichi ,nisipofunguliwa
mapema kutatokea vidonda vya tumbo ,uvimbe tumboni.
Ili niweze kushinda mfumo wa ndoto za kishetani katika roho inatakiwa nifanye
mambo yafuatayo:-
i)Kabla ya kulala inatakiwa noisome kwanza Biblia
MAELEZO KUHUSIANA NA SENTENSI HAPO JUU
Nikisoma Biblia kabla ya kulala ninakuwa nimejiunganisha
moja kwa moja na sauti ya Roho Mtakatifu,kwahiyo taarifa zote nitakazozipata au kwa lugha ya kawaida ndoto
itakuwa inahusiana namambo haya kwenye maisha yangu:-
i)Itanipa mwongozo wa maisha ya leo baada ya kuamka
usingizini
MFANO: 1
Nimepanga kwenda kazini asubuhi lakini usiku nimeota
nimegombana na mfanyakazi mwenzangu ,maana
yake haitakiwi niende kazini siku hiyo,kwasababu nitakapoenda kazinikuna hatari
ya ugomvi kutokea na kazi ikawa ndio mwisho siku hiyo.
MFANO :2
Nimeota ndoto jirani yangu amepata ajali lakini mimi
ninampango wa kusafiri,maana yake ndoto hii ni tata,lazima niende kwa
muonajianipe mwongozo juu ya hili.
NAMNA YA KUEPUKA HASARA ZA KIROHO ZINAZOWEZA
KUNIATHIRI
Ili niweze kuepuka hasara
za kiroho zinazoweza kuniathiri inatakiwa niruhusu moyo wangu ,vilevile
niulazimishe kufundishwa Biblia,kwasababu hasara za kiroho anazoweza kuzipata
mtu mara nyingi zinasababishwa na upofu wa kiroho.
(Kufanikiwa kwangu
kunatokana na jinsi ninavyoongezeka
kiufahamu)
Yeremia 23:23,24
Mungu yupo katika mfumo wa namna mimi ninavyoamini,kwahiyo
nikiongezeka katika kuamini ndivyo Mungu anavyoongeza Baraka zaidi,katika
sentensi hii ni kuiruhusu akili ikubali.
Yeremia 23:23
inadhihirisha wazi uhalisia wa umbo la Mungu kwamba ni Roho.
Yohana 4:24
Neno ni Mungu anazungumza waziwazi na kanisa, ndio maana tunashauriwa kusoma Biblia sana.
Ili niweze kupata ufahamu wa kutosha kwamba Neno ni Mungu
anazungumza waziwazi ni pale ambapo moyo
wangu unakuwa umeghafirika, ninaposhika Bibliakusoma amani inarejea kwenye moyo
,kwanini kwasababu akili inakubali urejesho wangu uko ndani ya Neno la Mungu.
Mkristo aliyejiunganisha na uwepo wa Neno la Mungu ndani
yake kuna mambo haya ni :-
I)
Mamlaka, mamlaka hii ndiyo humtengenezea mwamini mfumo
wa kijiamini sambamba na Neno la Mungu linavyosema katika Luka
10:19.
Mamlaka inazaaje mfumo wa kujiamini ndani ya mtu?
JIBU:Ni kwasababu akili ya mtuinatambua nafasi aliyonayo
mtu, ndiyo maana moyo wake unaamini
nafasi hiyo hakuna mtu anayeweza akaipindua .
Kwanini mioyo ya wakristo inapoteza nguvu ya kuamini , ni
kwasababu akili zao zinawashuhudia
matendo yao kwamba yako kinyume na kile wanachokiamini
3Yohana 1:1-4
Maisha ya wakristo yanakatishwa yaani wanakufa kabla ya
wakati wa Bwana ,kwasababu wanajikwaa kwenye Neno la Mungu.
Kutokutambua Mungu yu karibu na mimi kunaathiri sana imani
ya mtu kwenye eneo la kupokea Baraka kutoka kwa Mungu, nini kifanyike ?
inatakiwa nikisimamie kile ambacho
nimekiamini na kukiri kwenye kinywa change mpaka kitoe matokeo,hapo nitaitwa
mkristo aliyeokoka ,vilevile mkristo mwenye mamlaka .
Ili niweze kushinda vita vya kiroho inatakiwa moyo wangu
ujengwe katika misingi ya kiimani si katika misingi ya kihisia ,kwasababu hisia
ina tabia moja huja na kutoweka.
II)
Ujasiri
Maelezo na ufafanuzi kuhusiana na Ujasiri.
Somo hili bado litaendelea wiki
ijayo………………
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni