Jumapili, 11 Januari 2015

JIMIMINE KWENYE NENO.

                                                                                     UJUMBE WA LEO
                                                                                                 11/1/2015
JIMIMINE KWENYE NENO.
Kujimimina kwenye Neno la Mungu kutanisaidia kunipa ufahamu wa rohoni ambao ndio utakaonisaidia kuniunganisha na uwepo wa Mungu (Yesu Kristo).

Kuna hatari inayomkumba mtu sanasana jamii ya waaminio kupotoshwa nah ii mara nyingi inawakumba wakristo wavivu katika  maeneo makuu mawili
i)Usomaji wa Biblia
ii)Ufundishwaji Biblia (Neno la Mungu).
Watu wengi wamepotoshwa na hii inatokana na fahamu zao zao za kiroho kujifunga ,sentensi hii inanitahadharisha mimi kama mwamini yakwamba kila  linaloingia masikioni mwangu lazima nilipime katika Neno.
Maisha ya wakristo sansan jamii ya waaminio Baraka zao zimejifunga ,kwasababu wameruhusu mioyo yao kubebeshwa laana ambazo hazikuwa nazo,Hii imetokana na wakristo  wengi kukosa upeo wa ufahamu wa kupambanua ,ndio maana inatakiwa nisome sana Biblia ili niwe na asili moja na Mungu.
2Timotheo 4:1-8.
Mwamini akilisikiliza Neno la Mungu na wakati huohuo ana upofu wa kiroho maisha yake yana hatari kubwa ya kukosa mpenyo kwasababu moyo wake  utapingana na kile ambacho masikio yake yamesikia .
Nikiruhusu moyo wangu kujimimina kwenye Neno la Mungu, nah ii ndio itakayo nitengenezea  mtiririko wa Baraka za Mungukatika maisha yangu ,ndio maana katika kitabu cha Wakorintho kimesema wazi
1Wakorintho 6:17.
Ninaporuhusu moyo wangu kukaa chini kulisikiliza Neno la Mungumaana yake ninatengeneza muunganiko wa siri na Mungu ambao ndio utakaoleta hali ya urejesho  wa kiimani.
(Magonjwa yanayowakumba wakristo yaanza kwenye ndoto,ndio maana tunashauriwa kutia bidii katika usomaji wa Biblia ,vilevile kuhudhuria kanisani).
Kujimimina kwenye Neno la Mungu kutanisaidia kunizamisha kwenye maisha ya kweli ambayo ndio Mungu anahitaji kila mwenye imani aishi.
Maisha ya kweli ndio yanayompelekea mwamini kujibiwa maombi wakati wote anapohitaji kwenye uso wa Mungu
2 Yohana 1: yote na  3Yohana 1:yote.
Mwamini anayetembea klatika kweli ya Mungu maisha yake hayana ubaguzi kwa maana zaidi atawabeba watu wote kama ndugu zake waliotoka katika tumbo moja.
Baraka za watu zimejifunga kwasababu wanaishi maisha ya visasi na hila ndio maana wamekosa mipenyo katika maisha.
Ili niwe sambamba na Baraka za Mungu (Yesu Kristo) lazima niyalazimishe maisha yangu yaendane na kweli ndipo karama za Kimungu zitajifunua kwngu dhahiri.
Suala la kutembea katika kweli ni la mkristo aliyeamua kuikana nafsi yake kwaajili ya Mungu.
Sisi ambao ni jamii ya waaminio tunahitaji hekima sana ya kuishi na jamii ya wasioamini,kwasababu jamii ya wasioamini wako makini sana kuchunguza mienendo yetu ili watuhukumu nayo.
Ili niweze kuwa na nguvu ya ushawishi katika jamii ya wasioamini inatakiwa mimi kamamkristo nizame katika mambo makuu yafuatayo:-
i)Nisome Biblia ,katika usomaji wa Biblianitapata kufahamu kwa undani maisha aliyoishi Yesu Kristo na mienendo yake ,hapo itakuwa rahisi  kwangu mimi kuanza kupambanua ni namna gani ninatakiwa niishi kama mkristo niliyejaa imani.
Maeneo haya yanathibitishwa na kitabu cha Yohana 14:1-30.
Katika kitabu hiki cha Yohana 14Yesu alizungumza na wanafunzi wake (kanisa) kabla ya kuuvua mwili wa damu na nyama.
Yohana 14:19 kwenye kipengele  ambacho Yesu anasema ninyi  mtakuwa hai  kama mimi nilivyo hai anadhihirisha  wazi kwa ulimwengu katika ile jamii iliyoandaliwa kuurithi ufalme wa Munguyakwamba maisha ya Yesu Kristo wakati ameuvaa mwili aliishi katika haki na kweli,kwahiyo mimi ili niwe sambamba na andiko hili inatakiwa  niyazamishe maisha yangu katika kweli ndipo Baraka za Mungu vilevile kuurithi  ufalme wa Mungu utakavyokuwa sehemu yangu.
B. FAIDA ZA KUJIMIMINA KWENYE NENO LA MUNGU
Zipo faida nyingi ninazoweza kupata zitokanazo na kujimimina kwenye Neno la Mungu:-
a)Faida ya kwanza nitakayoipata katika kujimimina kwenye Neno la Mungu nitapata imani yenye uwezo wa kukabilianan na kila aina yoyote ya jaribu linaloweza kujitokeza katika mzunguko wa maisha yangu ya kila siku, katika jambo hili la kiimani ni la msingi sana lakini jamii nyingi ya waamini hupuuzia, ndio maana maisha yao hukosa mwanga wa mafanikio ingawa wanamuomba Mungu,hata Biblia imethibitisha     Waebrania 11:6.
Ninashauriwa kuishi katika misingi ya imani kwasababu imani ni kiunganishi kati ya mtu na Mungu,vilevile imani inarahisisha mwamini kupokea Baraka zake pale tu anapoomba kwenye uso wa Mungu.
b)Faida ya pili itokanayo na kujimimina kwenye uwepo wa Mungu ni kibali,Kibali ni jambo la msingi sana kwa kila mwanadamu mwenye mwili,kwasababu kibali kinampa mwamini fursa ya kukubalika mahali popote anapoingia,vilevile kibali huweka wepesi wa mkukubalika mbele ya jamii iliyomzunguka.
ANGALIZO 1:Nikipoteza kibali maana yake nimepoteza mwelekeo wa maisha inatakiwa nirudi
                    magotini, na jambo hili wakristo wengi wamejikwaa kwa kuwalaumu Watumishi wa Mungu.
Hali ya kufundishwa Neno la Mungu ndio inayonisaidia mimi kama mwamini kunipa ufahamu wa kutambua,Je! Nina kibali kwa Bwana cha kupokea Baraka zangu? Ndio maana hata Zaburi 199:130 inaweka wazi kila kitu.
Kufundishwa Neno la Mungu kunaleta hali ya mwanga katika maisha ya mwamini itakayomsaidia kumpa uwezo wa kupambanua vilevile kujisimamia katika imani.
(Hali ya wakristo kushindwa kujisimamia inatokana na udhaifu wa imani waliyonayo).
Nikidhoofika kiimani nitakuwa jalala la matatizo na magonjwa ,kwahiyo ili niweze  kuliepuka hili inatakiwa niruhusu maisha yangu yaongozwe na Neno la Mungu.
c)Faida ya tatu itokanayo na kujimimina kwenye Neno la Mungu nii kupata mtiririko  wa maombi na watu wengi jambo hili hawajui kama ni la maana sana.
Mtiririko wa maombi unakuwepo ndani ya mwamini mwenye kina cha ndani cha Neno la Mungu, na maombi yanayojibiwa kwenye uso wa Mungu ni yale yanayoombwa sambamba na Neno la Mungu.
Kuna mahusiano kati ya neno  YESU KRISTO na MUNGU, ndio maana Yesu Kristo akasema mtu akiomba sambamba na  jina langu hilo atalifanya ili baba atukuzwe ndani ya mwana,ila hapa kuna siri nzito.
Yohana 1:1-2 ,14
Wafilip 2:8-11.
Imani ndio inayo niimarisha kwenye misingi ya wokovu,Wokovu ndio unaonirithisha uzima wa milele.
(Nikitaka kushinda vita vya kiroho ishu ni Neno).
(Nikmitaka kubadilika kitabia na asili zote ziniache inatakiwa nikubali kufundishwa Biblia).
ANGALIZO 2: Nikitambua uthamani  wa kumheshimu Mungu sitaruhusu maisha yangu yadhalilishwe
                         na kitu ambacho nina uwezo wa kukiepuka.
Maisha ya Neno la Mungu ndani ya mtu ili yaweze kumletea mabadiliko  inategemea mahusianao ya mtu aliyonayo na imani ya  Yesu Kristo.
MFANO:
Nahitaji kubarikiwa kwenye uchumi wangu lakini Mungu anatazama mahusiano yangu mimi na utoaji ndipo ufungulie Baraka.
Nikitaka maisha yangu yapate mabadiliko lazima niruhusu moyo wangu uelimishwe na Neno la Mungu (Biblia).
Kitendo cha Neno la Mungu kuelimisha moyo wangu maana yaek ni Yesu Kristo mwenyewe anaelimisha moyo wangu, kwasababu Biblia imethibitisha Ufunuo 19:13.
(Kitendo cha kusoma Biblia maana yake moyo wangu  unazungumza na Mungu moja kwa moja,kwahiyo nahitaji suala la nidhamu wakati wa kusoma Biblia).
Je! Inatakiwa nidhamu hii iwe katika mazingira gani?
i)Wakati wa kusoma Biblia inatakiwa nijifungie mahali ambako hakuna kelele hii itanisaidia moyo wangu kupata utulivu wa kupokea.
MFANO WA MAHALI AMBAKO HAKUNA KELELE
Chumbani.
ii)Wakati wa kusoma Biblia inatakiwa nizime simu na vifaa vinavyoweza kuashiria kelele,
MFANO WA VIFAA VINAVYOASHIRIA KELELE:-Televisheni,Redio ,Feni ,Simu n.k.
Kelele za vifaa hivi vilivyotajwa hapo juu huaribu mfumo wa ufahamu wa mtu katika kupokea sauti ya Mungu kupitia Neno.
d)Faida nyingine nitakayoipata kutokana na kujimimina kwenye Neno la Mungu ni mamlaka, na jambo hili  ni nyeti sana kwasababu mamlaka ndiuo inayomsaidia mkristo anayeliamini Neno la Mungu kushinda katika roho.
Mamlaka iliyoko ndani mwangu nikizidi kuipalilia  katika Neno la Mungu ndivyo nitakavyozidi kunizalishia faida na siku zote mamlaka hiushi katika kinywa cha mwamini ,ndio maana Mithali 18:20,21. Imethibitisha wazi maneno haya.
Ulimi una nguvu hai ya kuumba vilevile kuua, kwahiyo inatakiwa niwe mkristo mwenye nidhamu sana kwenye moyo wangu ili maisha yangu yapate mpenyo.
ANGALIZO 3:Nikimuona mtu yupo kwenye uwepo wa Mungu yaani kanisani alafu
                         anachukia  kufundishwa maana yake hakuja kanisani kwa nia njema,kwahiyo mtu wa
                       aina hii atapata madhara yafuatayo:-
i)Laana
ii)Magonjwa yote na matatizo wanayofunguliwa watu wengine huambatana nay eye, vilevile mtu wa aina hii  huwa ana roho ya udhoofishaji ndani yake.
Rafiki asiyetaka kwenda kusali kanisani ni kuwa naye makini,kwasababu roho anayokuwa ameibeba ni ya udhoofishaji, kwahiyo nisipokuwa naye makini  anaweza kuniua kiroho.
Somo litaendelea wiki ijayo…………………………..



Hakuna maoni: