UJUMBE WA LEO
21/12/2014
IMANI NA SADAKA.
Imani na sadaka ni
vitu viwili vinavyoishi sambamba, kwa maana
zaidi ni vitu ambavyo haviachani ,hii yote inatokana na utoaji ni imani
Wakristo waamini walio wengi hawatambui maana ya sadaka ndani ya kanisa ,ukweli ni kwamba sadaka ni
moyo wa kanisa.
Utoaji wa sadaka unahitaji uwe katika msingi wa imani, ndipo
sadaka hiyo itapata kibali machoni pa Mungu
Luka 21:1-4.
Utoaji wa sadaka katika haki
uanao nafasi kubwa ya kutuongezea siku za kuishi, kwasababu sadaka ni
moyo wa kanisa.
Jinsi ninavyokuwa na bidii ya kutoa sadaka ndani ya kanisa ndivyo ninavyouimarisha ufalme wa Mungu.
(Mkristo ambaye amejiepusha na kweli ya Mungu na haki yake ,
kamwe hawezi kuwa na roho ya huruma
ndani yake).
Waamini wasiotoa sadaka kanisani bado hawajatambua nini maana ya kumwabudu Mungu, kwasababu
sadaka ni sehemu ya ibada.
Mkristo ambaye haoni uthamani wa kumtolea Mungu sadaka
inayoeleweka yuko mbali kabisa na uwepo
wa Mungu, hii hali inaweza kuathiri
maeneo mengi sana katika maisha ya
mwamini.
Nikitaka sadaka zangu Mungu azikubali inatakiwa nitoe katika
imani,kwasababu kutoa katika imani
kutanisukuma mimi kumtolea Mungu sadaka inayoeleweka sio
chenji zilizozidi kwenye nyanya sokoni.
(Sadaka ni kitu kinacho heshimika sana kwenye ufalme wa Mungu,kwasababu katika Matendo ya Mitume 10:1 ……..inaonyesha
picha ambayo Mungu alimtuma Petro Nabii kwa Kornelio,hii ilikuwa ina lengo la
kuonyesha dunia uthamani wa sadaka
tunazitoa kwenye uso,ndio maana Kornelio alipata kibali machoni pa Bwana).
Nikihitaji sadaka zangu ziwe na ukumbusho kwenye uso wa
Mungu inatakiwa nifanye mambo yafuatayo:-
I)Nitoe kwa imani
II)Nitoe kuujenga ufalme wa Mungu kwa mali zangu.
III)Nitoe kwa lengo la kusaidia masikini.
Nikiwa ninapenda kufanyiwa vitu vizuri au kupewa vitu vizuri,
lakini mimi mwenyewe sipendi kuwafanyia
watu vitu vizuri maisha yangu hayawezi kuinuka
yatabaki katika hali ya utumwa
siku zote.
(Siri ya kupata pesa ni kutoa).
Kuna maumivu mengi wakristo tunayoyapata yanatokana na
kujikwaa.
(Nisipofahamu cha Mungu ni kipi kwenye utajiri wangu maisha yangu ninakuwa
nimeyaweka rehani).
SADAKA YENYE
KIBALI:
Sadaka yenye kibali mbele za Mungu ni sadaka ile anayoitoa
mwamini akifahamu moyoni mwake kwamba sadaka hiyo aliyoitoa italitoa kanisa sehemu moja kwenda
sehemu nyingine
Luka 7:40-50.
(Mungu anamthamini sana mtu ambaye ni mtoaji bila kutazama
mazingira yake).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni