Jumapili, 28 Desemba 2014

IMANI NA SADAKA SEHEMU YA PILI

UJUMBE WA LEO
28/12/2014
IMANI NA SADAKA
SEHEMU YA PILI
Sadaka sio agizo la mwanadamu  yeyote  bali ni agizo la Mungu mwenyewe ,kwahiyo sadaka ni kitu kinachotolewa  katika mazingira ya imani .

(Mungu ana wivu sana katika eneo la utoaji ,kwasababu kile kinachotolewa kinakuwa  na lengo kuu  la kuimarisha ufalme wake).


(Mkristo anayepinga katika eneo la utoaji wa sadaka huyo ameshavamiwa  na roho ya uasi ,kwasababu hakuna baraka yoyote ya kifedha inayoweza kumjilia mtu kabla yeye mwenyewe hajaandaa mazingira ya kumtolea Mungu kwanza).

Nikifanya vya Mungu kwanza kabla ya vyangu Mungu ataniona ni mwenye imani kwenye uso wake,kwahiyo lazima atanilinda na kila pigo au uvamizi uliokusudiwa dhidi yangu.

Mkristo asiyetambua uthamani wa sadaka katika nyumba ya Mungu lazima ataandamwa na mambo haya ili mradi tu kila alicho nacho kiteketee:-
A)Magonjwa –Inafahamika wazi magonjwa ni kitu kinachogharimu maisha yetu sana kwa pesa nyingi.

(Utoaji ni mfereji wa Baraka ya Mungu kuja kwenye maisha ya mtu).

Hii ni hatari sana kama mimi sio mtoaji wa sadaka nitavichuma sawa ila sitavila ,hii ilimtokea dhahiri Anania na Safira katika kitabu cha  Matendo ya Mitume 5:1-6,vilevileilmtokea Kaini mwana wa Adamu katika Mwanzo 4.

(Sadaka ina nguvu ya utajiri ndani yake vilevile sadaka ina nguvu ya laana ndani yake ambayo ninaiona laana hii ikimtafuna Anania na Safira  na Kaini na wengine wengi).

Kama sitambui uthamani wa sadaka kwenye nyumba  ya Mungu na Mungu  hatatambua uthamani  kwenye maisha yangu .

(Mafanikio ya wakristo wengi yanajifunga kwasababu  si watoaji).

ANGALIZO 1:Nkifahamu chanzo cha Baraka yangu  ni nani basi itakuwa  rahisi kufahamu 
                         wa  kumtolea.

Kama sisimami kikamilifu kutoa sadaka kwenye nyumba ya Munguukweli ni kwamba ulinzi wa Mungu hautakuwepo kwenye maisha yangu  hata Maandiko yamethibitisha  hili katika Kitabu  cha Hagai 1:1-15.

Baraka iliyo halali na yenye uwezo  wa kuyabadilisha  ni ile inayotoka kwenye mwongozo wa Roho Mtakatifu. 

JE!SADAKA NI NINI
Sadaka ni mbegu ninayoipanda kwenye uso wa Mungu  katika mazingira ya utoaji , ndio maana inatakiwa liwe ni jambo linalotoka katika imani .

SWALI- Je!nitajuaje udongo una rutuba ya kunizalishia Baraka?.
JIBU-Ni 2 Wakorintho 3:17.

(Jina la Yesu Kristo  linatenda kazi  pale nitakapo tamka  kwa imani).

Inatakiwa nitoe sadaka yangu kwenye nyumba  ya Mungu kwanza  katika  mazingira ya imani ,vilevile nikiwa na matarajio ya kupata Baraka kutokana na sadaka hiyo.

Wakristo wengi sadaka wanazozitoa   huzitoa katika hali ya kawaida ,ndio maana hazizai Baraka ,hii inatokana na wao kutokutambua uthamani wa sadaka wanazzozitoa kwenye nyumba ya Mungu.

Nikitambua sadaka ninayoitoa ninapanda mbegu kwenye uso wa Mungu itatakiwa niongeze kiwango cha kutoa .

(Nikitoa kama desturi siwezi kuona umuhimu wa kumtolea Mungu chenye maana).

Nikihitaji mpenyo katika suala  la uchumi lazima nibadilishe  mazingira yangu  katika utoaji wa sadaka.

Jinsi ninavyotoa kuwajali wenye shida ndivyo  Mungu anavyoniongezea Baraka tele  nisipungukiwe
                                              Wagalatia 2:10.

(Maisha ya mtu mchoyo mbinafsi hayana kibali machoni pa Mungu).

Katika suala la kumtolea Mungu wakristo wengi wanakuwa wanakaidi kwasababu wanatoa  nje na mapenzi ya Mungu.

Inatakiwa nimheshimu Mungu kuliko pesa nilizonazo  nitaongezewa siku za kuishi.

Ni vigumu kuimiliki Baraka ikatulia katika mkono wangu kama sijapewa ufahamu wenye uwezo  wa kunipa nguvu ya kuzitawala Baraka ,hili jambo ni nyeti sana.

ANGALIZO 2:Nikibarikiwa wakati huohuo  nikawa bado sijaimarika  kiimani nina hatari kubwa sana inayoweza kunifanya nimuasi Mungu,kwasababu imani  ya Yesu Kristo ni vigumu kuitawala pesa.

Ili niweze kuyatawala mafanikio inatakiwa niwe  katika misingi ya kweli na haki.

Pesa ina kawaida ya kumfanya mtu kuridhika , na huko kuridhika ndiko kunakompelekea mwamini kujisahau.

Baraka itakayoniingiza kwenye mafanikio ya kweli na haki mpaka nikainuliwa na jamii ikanishangaa ipo katika mazingira matatu:-
A)Kutoa shukrani katika kila kitu ambacho Mungu ananisaidia .


Sadaka ina nguvu ya kurejesha heshima ya mtu kwenye uso wa Mungu.

Hakuna maoni: