Jumapili, 7 Desemba 2014

RUHUSU IMANI ITENDE KAZI

UJUMBE WA LEO
07/12/2014
RUHUSU IMANI ITENDE KAZI
Wengi tunafahamu nini maana ya imani , vilevile tumejifunza mengi kuhusu imani lakini kuna wengine wasio fahamu imani ni nini ingawa wanasema tunaamini.

Ili niweze kufahamu nini maana ya imani inatakiwa nifahamu kwanza imani inapatikanaje.
Imani kama imani chanzo chake ni  hutokana na kusikia ujumbe wa Neno la Mungu,hapo huwa ndio mwanzo wa mwamini kuwa na hofu na Mungu.
Warumi 10:17.
Imani ya mkristo inakua anavyozidi kujiwekea mazingira ya kusikiliza Neno la Mungu,mkristo akiongeza bidii ya kusoma Biblia,kusikiliza Neno la Munguyaani kufundishwa imani itakayojengeka ndani mwake itakuwa na uwezo mkubwa wa kusababisha kitu kutokea.
Mkristo asiyeruhusu imani yake kutenda kazi anakabiliwa na mambo yafuatayo:-
a)Ufahamu wa rohoni kujifunga
b)Kina cha maarifa ya rohoni kushindwa kupambanua
c)Kifo cha kiroho, mtu ambaye ameingia katika mazingira haya ya mambo tajwa hapo juu anakuwa hana tena muunganiko na Baraka za Mungu kwa maana zaidi akifanya biashara itakosa mpenyo,akiajiriwa atapoteza mpenyo kwa bosi wake kifuatacho ni kufukuzwa kazi na mengine mengi yanayofanana na haya.
Nikitaka kuijenga upya familia yangu katika misingi ya hofu ya Mungu inatakiwa nianze upya kuruhusu imani yangukutenda kazi kwa maana zaidi kuliruhusu Neno la Mungu kuielimisha roho yangu.
Huduma ya Yesu Kristo wakati akiwa katika mwili ilikuwa na nguvu kubwa sana na jamii nyingi ya waamini iliongezeka sana kwa wakati ule,vilevile miujiza na ishara  maajabu mengi sana yalithibitika , ni kwasababu aliliimarisha  kanisa katika misingi ya mafundisho na Biblia inayathibitisha haya:-
Mathayo 9:35,36
Mathayo 8:1,5
Mathayo 7:28 na Marko 2:1,2.
(Hakuna muujiza wowote unaoweza kuthibitika bila imani ya Neno la Mungu kuhusika).
Ili mkristo aweze kutoa hekima katika kinywa chake ,na hekima hiyo iwe msaada kwa watu wengine inatakiwa awe katika mfumo wa mambo haya:-
i)Awe ni msomaji wa Biblia sana,kwasababu hekima ya kweli na haki iko ndani ya Neno la Mungu.
ii)Awe muombaji hiyo itamsaidia muda wote kuwa na muunganiko na Roho Mtakatifu.
(Mkristo mwenye kina kirefu cha imani ana uwezo mkubwa wa kupambanua sauti ya Mungu anaposema)
Nikitaka kuisikia sauti ya Mungu inatakiwa nitafute kina cha imani.
Marko 2:1,2 ni picha wazi inayodhihirisha huduma ya Yesu Kristo kwamba ilikuwa chini ya msingi wa mafundisho , ndio maana kanisa liliimarika.
(Fahari ya kwanza inatakiwa iwe kwenye Maandiko Mtakatifu  yaani Biblia).

IMANI INAVYOTENDA KAZI
Siku zote imani inatenda kazi katika mazingira magumu yaani mazingira yaliyoshindikana , na hii inatokana na iamani ni kitu cha rohoni kwa maana zaidi ni kitu kisichokuwa na umbo maalumu.
Nikitaka mazingira yanisaidie kumwamini Mungu nitakuwa sina tofauti na mtu aliyekufa lakini anatembea ambaye Biblia ilimsema katika kitabu cha Ufunuo 3:1.
Ili mkristo awe hai kiroho inatakiwa imani aliyonayo airuhusu kutenda kazi, na imani ili iweze kazi inategemea ushirikiano wa mtu binafsi.
Mkristo anapomwamini Mungu tayari anakuwa na muunganiko katika roho na sio katika hali ya kimwili.
Mkristo asiporuhusu imani yake kutenda kazi maono yake hayawezi kutimia hata kama anaomba usiku na mchana .
Ili niweze kuifahamu  imani yangu imekuwa hai ni pale ambapo nitakapoanza kutendea kazi kila mwongozo nitakaopewa na Roho Mtakatifu kupitia mtumishi wake.
(Hichi kitu inabidi nikiache  kabisa nizaliwe upya .Je! kitu gani?)
Ushabiki wa kiroho ni mbaya sana unaharibu makanisa ‘Yesu nisaidie’)


Hakuna maoni: