Jumapili, 30 Novemba 2014

LAZIMA NITAMANI MABADILIKO YA KIIMANI SEHEMU YA TATU

UJUMBE WA LEO
30/11/2014
LAZIMA NITAMANI MABADILIKO YA KIIMANI
SEHEMU YA TATU
Hali ya kutamani mabadiliko  ndani mwangu ndiyo itakayonipa  ujasiri wa kulazimisha mabadiliko kutokea .

(Nikijiona  ninamkosea Mungu hiyo ni picha wazi bado nina udhaifu katika imani )

Roho ya uaminifu inajiumba katika maisha ya mtu pale ambapo ataruhusu roho yake kuendelezwa na Neno la Mungu.


Mwamini akiwa bado hajaruhusu  hali ya mabadiliko  ndani mwake ni vigumu kuambatana na Baraka za Mungu hata angekesha  na kuomba
                                                       Amosi 3:3.

(Suala la ufahamu katika kumtafuta Mungu ni jambo la muhimu sana).

Mtu wako wa nje ambaye ni wewe mwenyewe ukiishi sambamba na mtu wako wa ndani  Baraka za Mungu zitakuwa  kama maafuriko  ya mto,kwasababu  siku zote mtu wa ndani  ni mkamilifu na mnyenyekevu.

Dhambi ndiyo inayoharibu uthamani  wa maisha ya mwamini.

(Kama ninahitaji Baraka za Yesu Kristo lazima nifanye mabadiliko katika maisha yangu ya kiroho).

Maisha ya kiroho yanahitaji mambo haya yafuatayo
i)Uaminifu
ii)Kuishi katika kweli.
iii)Kujinyima .

Ni vigumu kuiokoa imani yangu bila kujinyima mambo mengine ambayo ni haki yangu
Mfano wa mambo ambayo ni haki yangu:-
i)Chakula
ii)Starehe za kimwili n.k.

Misingi ya uaminifu nitakayoamua kuijenga kuanzia sasa  ndiyo itakayo rejesha  heshima yangu kwenye uwepo wa Mungu, vilevile kunipatia kibali kwa upya kwenye uwepo wa Mungu.

(Chanzo cha magonjwa katika  maisha ya mwanadamu mwenye mwili ni dhambi, ndiyo maana Kumbukumbu la Torati 28:15-62 inathibitisha hili).

Ukamilifu wa maisha ya mwamini ni pale ambapo anaporuhusu kuishi maisha ya kweli yote ya Mungu.

Ninashindwa kuyatawala maisha yangu ya kimwili kwasababu sina ufahamu wa kutosha wa Neno la Mungu, mara nyingi hali ya mwamini kudhoofika kiimani inatokana na kukosa  ufahamu wa Neno la Mungu.

Namna ambavyo ninweza kuruhusu hali ya kupata ufahamu ni pale ambapo nitaruhusu roho yangu kuendelezwa katika misingi ya Biblia.

Ni vigumu kuishi maisha Matakatifu kama sijaamua kufuata nyayo za Yesu Kristo.

SWALI: Je! Yesu Kristo aliishi maisha yapi?
JIBU
a)Aliishi katika haki  1Yohana 2 :28-29
b)Aliishi katika Upendo
c)Aliishi katika  kusaidia (utoaji)
d)Aliishi katika  Uvumilivu.

UFAFANUZI KUHUSU KIPENGELE   ‘A‘ KINACHOZUNGUMZIA HAKI
Yesu Kristo aliishi katika maisha ya haki ndiyo maana kila jambo alilolikusudia  lilithibitika palepale.

Nikitaka Baraka ya Yesu Kristo niishi katika haki.

1Yohana  2:29 ni hali halisi katika maisha yangu kama mcha Mungu yaani Baraka za Ibrahimu ,Isaka na Yakobo, na ni uthibitisho uliopo wazi bila haki hakuna Baraka .

Asilimia sabini na tano za wakristo  hupata Baraka za umoja kutoka kwenye uso wa Mungu, Je! Zipi hizo? Zile alizozinena kwenye maandiko Matakatifu ya kwamba huwanyeshea mvua walio haki na wasio haki na ndizo Baraka ambazo waamini wengi wameridhika  nazo,ndiyo maana hawana mwamko wa kuruhusu mabadiliko katika masiha yao ili waweze kuendana na zile Baraka ambazo Mungu amewaahidia wenye haki yaani Baraka za Ibrahimu ,Isaka na Yakobo.

Nini maana ya Baraka za Ibrahimu, Isaka na Yakobo ?
Maana yake ni Baraka ya  kuurithi ufalme wa Mungu pamoja na haki yake.

*Pesa sio ishu ,ishu ni upako*

ANGALIZO 1:Safari ya kutafuta haki ya Mungu ni safari ndefu sana ambayo inahitaji uvumilivu wa                           hali  ya juu.

UFAFANUZI KUHUSU KIPANGELE ‘B’ KINACHOZUNGUMZIA UPENDO:
Siku zote mwanadamu ana upendo wa kibinafsi ,na upendo huu uliofungamana na maisha ya mwanadamu ndiyo umekuwa kipingamizi cha kwanza kinachozuia Baraka za Mungu kuyaneemesha maisha yake.

Ili upendo wa mwamini uwe katika kweli ya Mungu unatakiwa uwe katika mfumo wa mambo haya yafuatayo:-
i)Usomaji wa Biblia kwa kina
ii)Ufungaji (kuomba ) mara kwa mara
iii)Uaminifu.

Kama sijaruhusu maisha yangu kuwa chini ya mwongozo  wa Maandiko Matakatifu ile asili ya Mungu ambayo ni upendo haiwezi kujijenga , kwahiyo kama ninataka kuimarika katika upendo wa Mungu ni haki yake .

Lazima niandae mazingira ya kuheshimu mwongozo wa Roho Mtakatifu unapotoka kwa maelekezo fulani.

Mkristo akitaka wokovu wake uwe salama inatakiwa aruhusu upendo wa Mungu ujijenge ndani yake  hapo atakuwa ameiokoa imani
                                                               1Wakorintho 13:13.


Upendo ulio katika maisha ya mwamini ndiyo unaodhihirisha  kiwango cha imani aliyonayo katika maisha yake , nah ii ni kwasababu Biblia imethibitisha upendo ni roho ya Yesu Kristo. 

Hakuna maoni: