Jumapili, 14 Desemba 2014

RUHUSU IMANI ITENDE KAZI: SEHEMU YA PILI:

UJUMBE WA LEO
14/12/2014
RUHUSU IMANI ITENDE KAZI:
SEHEMU YA PILI:
(A)IMANI INAVYOTENDA KAZI
Kila mwanadamu anayeishi katika mwili amepewa kiasi cha imani ,mwendelezo  wa imani hii aliyopewa  na Mungu utatokana na namna ambavyo ataruhusu moyo wake kumwamini  Yesu Kristo, vilevile na kinywa chake kumkiri Yesu Kristo,hapo ndiko kunakotokea chimbuko la wokovu
Warumi 10:9,10

Imani ya mwamini inapata nguvu ya kutenda kazi ikishakuwa na muunganiko wa ndani wa Neno la Mungu.
Ili imani niliyonayo iwe msaada na maisha yangu inatakiwa nisimame katika msingi wa mambo mawili:-
A)KWELI
B)HAKI.
(Maisha ya ukweli,maisha ya haki ni ufunguo wa Baraka zangu kwenye uwepo wa Mungu).
Maisha ya kweli katika jamii ya waaminio ndiyo yanayotakiwa, kwasababu jamii kubwa ya wasioamini inatakiwa washawishike kumjua Mungu kupitia maisha yetu sisi kama waamini.
(Mkristo yeyote anayemcha Mungu anastahili kuishi maisha ya kiimani ndiyo yanayozaa haki na kweli ndiyo maana hata Biblia imesema Zaburi 51:6).

Sababu ya imani ya mkristo kuwa na upofu inatokana na kutokuishi maisha ya kweli na haki ,vilevile ndicho kimekuwa chanzo cha Baraka za wakristo kujifunga yaani kutokupata mpenyo.

Jamii kubwa ya waaminio wanazikosa Baraka za Mungu kwasababu wanaishi kinyume  namapenzi ya Mungu.

Maisha ya kweli na haki huisaidia imani ya mkristo kudhihirisha mamlaka yake waziwazi na hapo ndipo unapotokea mwanzo wa mafanikio katika maisha ya mwamini.

Imani yenye uwezo wa kutenda kazi inayavaa maisha ya mtu pale ambapo mtu huyo ataamua kuruhusu Neno la Mungu kuiendeleza roho yake,Hili jambo lipo hata katika maandiko
Warumi 10:17.


(Nikihitaji kwenda sambamba na Baraka za Mungu lazima niruhusu hali ya ukuaji wa kiimani).

Hakuna maoni: