Jumapili, 16 Novemba 2014

UJUMBE WA LEO : LAZIMA NITAMANI MABADILIKO YA KIIMANI



16/11/2014
UJUMBE WA LEO
LAZIMA NITAMANI MABADILIKO YA KIIMANI
Mabadiliko katika maisha ya mwamini  yanatokana na mwamini anavyozidi kukua katika  ufahamu wa rohoni.
(Mwamini asiyekuwa na ufahamu wa Neno la Mungu ,hana mvuto wa kubarikiwa na Bwana)
Mkristo anavyozidi kutamani  mabadiliko ya kiimani ndivyo Mungu anavyomtengenezea wepesi wa kuzifikia Baraka zake ,vilevile Baraka za wakristo zimegawanyika katika makundi yafuatayo :-
a)Baraka za kiuchumi
b)Baraka za  kiafya
c)Baraka za kiroho
Mimi kama mkristo mwamini inatakiwa nifahamu maeneo ambayo natakiwa nifanye mabadiliko katika maisha yangu
Baraka za mkristo chanzo chake ni Neno la Mungu.
Kutokuitii sauti ya Mungu inayotoka madhabahuni inaonyesha wazi namna ambavyo mkristo hana ufahamu wowote na Neno la Mungu hata kama kila siku anaingia kanisani.
Lazima nifanye mabadiliko ya kiimani kwasababu maisha ya mkristo aliyeokoka yanahitaji msaada wa Roho Mtakatifu kwa asilimia mia moja, vilevile mwongozo wa Roho Mtakatifuutaimarika katika maisha ya mkristo ambaye amezama katika  kina cha Neno la Mungu.
Mabadiliko ya kiimani yatamsaidia mwamini kutembea katika misingi ya haki ambayo ndiyo Munguanaitaka aione kwa waamini.
(Nikiyaendesha maisha yangu katika misingi ya kiimani mabadiliko nitakayoyafanya yataniletea Baraka )
Kwanini Nuhu alipata kibali machoni pa Bwana ?Mwanzo 6:8,9.
Nuhu alipata kibali machoni pa Bwana kwasababu aliishi katika mazingira haya:-
a)Mazingira ya ukamilifu
b)Mazingira ya haki.
c)Mazingira ya utauwa
Kwanini wakristo wa leo hawapati kibali machoni pa Bwana?, ni kwasababu
a)Wanaishi katika mazingira ya visasi,na inafahamika wazi mtu mwenye kisasi ndani ya moyo hana uwezo  wa kusamehe, na hii imesababisha vifo kwa wakristo wengi
b)Wanaishi katika mazingira ya kutokuamini na hili jambo limepeperusha Baraka za wakristo wengi sana.
Wanaobarikiwa katika uwepo wa Mungu  ni wale wanaofuatilia kwa makini mwongozo wanaopewa na Roho Mtakatifu.
(Wakristo wengi wamepoteza miujiza yao kwa kutokutii maelekezo wanayokuwa wamepewa na Roho Mtakatifu).
Ukidharau maelekezo maana yake umeidharau nguvu ya uponyaji hakutakuwa na mabadilikom katika maisha yako, utakuwa ni mkristo aliyedumaa kiroho.
Mkristo ambaye ametamani mabadiliko ya kiimani maana yake ameamua kuishi maisha ya utauwa.
Maisha ya utauwa yatampa mkristo faida zifuatazo:-
a)Kibali machoni pa Mungu (Neema)
b)Maombi yake kupata mpenyo wa kuleta majibu Yohana 14:13.
c)Mamlaka itakayoweza kusababisha hali ya wepesi katika mzunguko wa maisha yake ya kila siku Luka 10:19-20.
Mkristo anayeishi maisha ya utauwa amepewa nafasi ya kujibiwa hoja yoyote kwenye uso wa Mungu,na hili limethibitishwa katika maandiko Yohana 14:13, vilevile ni hali halisi kwa mwamini anayeishi maisha ya utauwa.
Mkristo anayeishi maisha ya utauwa ameamua kujinyima kwa ajili ya Yesu Kristo.
Nikiwa ni mkristo ninayeishi katika misingi ya imani ya Yesu Kristo haitakiwi nihukumu juu ya jambo lolote hata kama linanipa maumivu, hiyo ndiyo njia ya kunionyesha  kwamba nimepata mabadiliko ya kiimani.
Ninapolipiza kisasi maana yake ninausaliti uso wa Mungu.
Luka 10:20 ni tahadhari nzito kwa wakristo wenye kiburi cha uzima.
Hali ya majivuno husababisha kiburi cha uzima ambalo ndiyo anguko la wakristo wengi waliokoka.

Hakuna maoni: