Jumapili, 9 Novemba 2014

NAMNA AMBAVYO IMANI INAATHIRIWA:



UJUMBE WA LEO
9/11/2014
NAMNA AMBAVYO IMANI INAATHIRIWA:
Inafahamika wazi imani ni kuwa na hakika na mambo yanayotarajiwa ,vilevile ni bayana ya  mambo yasiyoonekana ,kwa maana zaidi imani ni kitu cha Rohoni.

Ninaposema nina imani maana yake  ninatamka kitu chenye umbo la kiroho ,na ukweli ni kwamba umbo la kiroho halishikiki kwenye mikono ya damu na nyama, ndiyo maana tuna heri sisi tunayemuona Yesu Kristo  katika misingi ya kiimani  kuliko wale waliomuona  katika misingi ya kimwili ,kwahiyo haitakiwi nijidharau.
Yohana 20:27-29.
Mkristo anayepiga magoti na kumuomba Mungu katika imani ya Yesu Kristo huyo ni mkristo mwenye kibali kwenye uwepo wa Mungu, kwa hiyo katika jamii iliyomzunguka atakuwa ni mtu wa tofauti, kivipi yaani atakuwa ni mtu anayeyaendesha maisha yake na maisha ya watu wengine kwakutumia mamlaka ya Roho Mtakatifu.
Katika suala la kuamini  inatakiwa niutii utu wangu wa ndani ndiyo unaonipa uthibitisho,kwasababu Roho Mtakatifu anaishi ndani ya utu wa ndani wa mkristo mwamini.
Katika suala la kuamini inatakiwa niwe  mimi mwenyewe na utu wangu wa ndani hapo kutatoka imani hai.
(Utu wangu wa ndani ukikosa msaada wangu mimi siwezi kupata mabadiliko)
Kwa asilimia  sabini na tano imani za wakristo zinaathiriwa na mawazo mabaya.
(Mawazo mabaya yakishauvaa  moyo wa mkristo mwamini hata kile anachokifahamu kizuri kuhusu Mungu atakikataa)
Jambo hili ni la kuchunga sana na kuwa makini nalo jinsi ninavyoruhusu hali ya kuwaza vibaya moyoni mwangu  ndivyo ninavyo tengeneza taswira ya kuamini kinyume na Mungu.
Namna ambavyo ninaruhusu mawazo mabaya kuuvamia moyo wangu ndivyo ninavyotengeneza sumu ya kuathiri imani yangu kuhusu Mungu.
Mfanikio ya kiroho katika maisha yangu yatakuja kadri ambavyo ninakaribisha mawazo ya Mungu ambayo ni Neno lake katika maisha yangu.
Mwanzo wa maisha ya wakristo kuharibika  ni kuruhusu mawazo mabaya kujijenga katika mioyo yao,ninaporuhusu mawazo mabaya kujijenga kwenye moyo maana yake ninaruhusu utawala kamili wa shetani kuyaharibu maisha yangu ya kiroho.
Dhambi yoyote anayoifanya mwanadamu anakuwa na akili zake timamu ,ndiyo maana dhambi ni ugonjwa wa ufahamu.
Nikiamua kufunga milango ya vitu visivyokuwa na utukufu kwa Mungu maana yake ninailinda imani.
Ili niweze kujijenga kiimani haitakiwi moyo wangu niuweke wazi kwa mambo yasiyokuwa na utukufu kwa Mungu.
(Ninapomjali mtoto mdogo maana yake ninamjali Mungu,kwahiyo inatakiwa nimjali mtoto katika maeneo haya yafuatayo:-  i)Mavazi
                                               ii)Chakula kizuri
                                              iii)Shule nzuri.
                                              iv)Kumuonyesha upendo vilevile kumuonya katika mazingira ya upendo.
Ili kuzishiriki Baraka za Mungu inatakiwa niwe mbunifu sana.
Haitakiwi nikumbuke  ninacho samehe kwa mtu,ndiyo silaha ya kuilinda imani.
Imani ya mwamini itapona kama mwamini huyo ataruhusu Neno la Mungu kuingiza wazo jipya ndani ya moyo wake.
Inatakiwa niruhusu imani ya Yesu Kristo kusimama moyoni mwangu, kwasababu ndiyo inayonisaidia kukabiliana na mazingira yoyote yale.
Mimi nikiruhusu Neno la Mungu kuingiza wazo jipya kwenye moyo wangu, maana yake ninajikabidhi kwenye milki ya Mungu kuyaongoza maisha yangu.
Mkristo anavyoongeza bidii ya kujifunza Neno la Mungu ndivyo maisha yake ya kiroho na kimwili yanavyo badilika
1Timotheo 4:16.
Usalama wa maisha ya mkristo upo katika mafunuo ya Roho Mtakatifu.
Kanisa lisipoimarishwa kwenye misingi ya mafunuo (Neno la Mungu)lazima lipoteze mwelekeo,kwahiyo kanisa litakuwa hai kama lina misingi ya mafunuo ya Roho Mtakatifu.
MBINU ZA KUILINDA IMANI ISIPOTEZE MWELEKEO
(Inatakiwa nifanye kitu ili kumgusa Mungu,ili niwe mwanzo wa Baraka zangu kwenye uwepo wa Mungu).

Hakuna maoni: