Jumapili, 23 Novemba 2014



UJUMBE WA LEO
23/11/2014
LAZIMA NITAMANI MABADILIKO YA KIIMANI
SEHEMU YA PILI
Mabadiliko ya kiimani yanaanza kuonekana kwa mkristo mwamini pale ambapo anaruhusu hali ya utii inayotoka chini ya mwongozo wa Neno la Mungu.
Mkristo mwamini anaporuhusu hali ya utii ndani ya moyo wake maana yake amefungua milango ya iamni yake kupevuka yaani kukua.

Utii alionao mkristo katika Neno la Mungu ndio unaotengeneza mazingira ya imani yake kukua siku hadi siku.
Utii ni hali ya kukubali  na kutendea kazi mwongozo unaopewa.
(Ni ngumu sana  kupata mpenyo kama niko kinyume na mwongozo).
Mungu amedhihirisha  wazi Baraka inayoambatana na mwamini mwenye utii katika moyo wake, vilevile amedhihirisha laana itakayompata mwamini asiyetii mwongozo wa Neno la Mungu
Isaya 1:19-20.
Baraka ya Mungu iko wazi katika maisha ya mkristo mwenye hali ya utii wa Neno la Mungu katika moyo wake.
Suala la utii lisiwe ni jambo la kuja na kutoweka bali inatakiwa liwe ndio mfumo mzima wa maisha yako ya ukristo.
(Utii alionao mkristo ndio unaomtengenezea kibali kwenye uwepo wa Mungu).
Ninapopewa taarifa nikaacha kuitendea kazi maana yake moyo wangu umemdhihaki Mungu waziwazi hii ni hatari sana , ndio maana watu wengi  chini ya jua wanakufa  kabla ya ule umri ambao Mungu aliunena kupitia kwenye kinywa chake.
Jinsi ninavyoruhusu hali ya utii katika moyo wangu ndivyo ninavyokaribia uwepo wa kubarikiwa.
(Utii ndio unaozaa hali ya unyenyekevu katika maisha ya mtu , vilevile ni hali inayorahisisha wepesi wa maisha ya kupata mpenyo).
Wakristo wengi wana hali ya kutokutii, nah ii ni kwasababu macho yao ya kiroho yamepofuka.
Hali ya utii kwenye moyo wa mtuitakua kulingana na mwaminianavyoongezeka katika ufahamu wa Neno la Mungu.
ANGALIZO :1.Nikienda kinyume na mwongozo wa Roho Mtakatifu maana yake ninajiharibia
                            mzunguko mzima wa Baraka zangu katika maisha yangu yote, vilevile kutatokea
                           hali ya kupoteza uhalisia wa ucha Mungu, kwahiyo ndio utakuwa mwanzo wa
                           mwamini kuyaishi maisha ya dhambi.
Nikitaka kushinda katika maisha ya kiroho niliheshimu Neno la Mungu, vilevile niishi chini ya sheria ya Mungu.
Namna ambavyo ninaonyesha  katika kile ambacho Mungu anasema na mimi ndivyo ninavyorahisisha hali ya ukuaji wa kiimani.
Bila kuruhusu hali ya utii kukua ndani ya moyoy wangu ni vigumu kupata utulivu wa kupambanua sauti ya Roho Mtakatifu pale anaposema na mimi, ndio maana waamini wengi humkemea Roho Mtakatifu pale anaposema nao  katika mioyo yao.
(Ufahamu ni ishu nyeti sana katika maisha yamwamini vilevile ni kitu ambacho kila mwamini anatamani kuukulia  ufahamu, maana bila ufahamu wa kiroho maisha yanakwama).
Nikiwa nina utii ninajiongezea asilimia za kukubalika kwenye uwepo wa Mungu.
Jinsi ninavyotii mwongozo wa Neno la Mungu ndivyo ninavyojiongezea hali ya kibali kwenye uso wa wanadamu.
2 Petro 1:1-11.
Mwamini anaporuhusu hali ya utii wa Neno la Mungu kuwa kama kiongozi katika maisha yake basi kuna misingi ya mambo kadha  itakayojijenga na kuambatana na imani yake  :-
a)Wema
b)Maarifa.
c)Kiasi.
d)Saburi.
e)Utauwa.
f)Upendo,kwahiyo mwamini mwenye misingi hii ataitwa haki kwenye uso wa Mungu.
NINI KIFANYIKE ILI HALI YA UTII IUMBIKE NDANI MWANGU:
Nikitaka hali ya utii ijiumbe ndani ya moyo wangu inatakiwa niruhusu roho yangu kuelimishwa na Neno la Mungu (Biblia).
Jinsi ambavyo ninatoa ushirikiano wa kujiendeleza kiroho kupitia Neno la Mungu ndivyo ambavyo Neema ya kukua  zaidi kiimani itakavyoimarika  ndani mwangu.
Bidii nitakayoionyesha  katika kujifunza Biblia ndani yake kutazaliwa Neema itakayo nirahisishia mpenyo wa mabadiliko ya kiroho.
Kumbukumbu la Torati 28:1.
Nini maana ya kusikilizasauti ya Mungukwa bidii? Maana yake ni kuliweka Neno la Mungu katika hali ya vitendo.
Bidii ya mwamini katika kumtafuta Mungu huonekana katika mazingira ya vitendo siku zote.
Bidii ya mwamini katika kumtafuta Mungu inaanzia pale ambapo mwamini anaamua kujinyima vitu ambavyo  ni haki yake kwa ajili ya Mungu
Mfano wa vitu ambavyo ni haki  yangu;-
I)Kula na kunywa ,itanilazimu nijinyime hivi kwaajili ya kumtafuta  Mungu yaani kufunga ,ndio maana hata Biblia  ikazungumzia kitu juu ya vyakula
Warumi 14:17-23.
ANGALIZO .2:Ninaposhindwa kutoa sadaka kanisani vilevile fungu la kumi kiuaminifu 
                        ninaonyesha
                       wazi utovu wa nidhamu kwenye uwepo wa Mungu, kwahiyo katika hali ya uhalisia
                      wa kimungu hakuna Baraka yoyote  inayoweza kuingia kwangu  zaidi ya laana ,
                       kwahiyo ili niweze kupona katika hili inabidi nionyeshe  hali ya utii kwenye Neno la
                         Mungu kama ilivyoandikwa  katika Malaki 3:8-10.
(Ufalme wa Mungu ni kufungua moyo wangu kwa utii wa mambo mema ).

Hakuna maoni: