2/11/2014
VITA VYA KIIMANI: SEHEMU YA PILI.
Vita vya kiimani
vinapiganwa katika mazingira ya
rohoni, ndio maana vinaihusisha imani kwa asilimia mia moja , na hii yote
inatokana na imani ,kwamba ni kitu cha rohoni na siku zote kitu ambacho kipo
rohoni hakina umbo maalumu.
Imani haishikiki kwa
mkono wala haina umbo maalumu vilevile ni kitu kilichokamilika, ndio maana sisi
tunaomwamini Yesu Kristo tunasisitizwa sana kudumu katika misingi ya imani , na hapo ndipo unapotokea mpenyo wa
maisha ya mtu kueleweka vilevile
kufanikiwa.
Wakristo wengi
wamejichanganya vita vya kiimani wamevigeuza ni vya kimwili ndio maana
maisha yao yameishia kubeba hila na kujeruhika.
Vita vya kiimani
vinapiganwa kiroho na sio kimwili.
Nikivigeuza vita vya kiimani
(kiroho) katika hali ya kimwili lazima nitashindwa kwasababu
anayeni[pigania anaishi katika Roho.
Vita vya kiimani havipiganwi kati ya mtu na mtu bali
vinapiganwa kati ya mtu na madhaifu yaliyoko kwake.
MFANO: Mimi nina tabia
ya uongo tayari ile tabia ndio shetani
katika maisha yangu, vilevile kipingamizi kitakachomzuia Mungu asiseme
na mimi.
Vita vya kiimani ni kati yangu na dhambi inayokula
maisha yangu.
(Hii ni hatari sana wakristo wengi wataikosa mbingu
kwasababu ya kukubali kuaminishwa kinyume na Maandiko Mtakatifu).
Ni vigumu kuingia kwenye uwanja wa mapambano ukiwa hauna uzoefu wa kutosha wa kutumia silaha adui
atakumaliza, hii ni sawa na mkristo anayeingia katika vita vya kiimani yaani katika uwanja wa mapambano akiwa bado hajatubu dhambi.
Vita vya kiimani vinamhitaji mkristo mwenye upeo wa
ufahamu wa Rohoni wa kutosha.
Mahusiano na Neno la Mungu (Biblia) na mkristo ndiyo
yatakayomsaidia kupenya kwenye ulimwengu wa roho,kwasababu vita vya kuyaharibu
maisha ya mkristo havianzii katika mwili vinaanzia katika Roho.
Mwenye uwezo wa kuvishinda vita vya kiimani ni mkristo aliyeimarika katika Neno la Mungu.
Silaha itakayomsaidia mkristo kushinda vita vya kiimani ni Neno la Mungu (Biblia) na jambo hili
limethibitishwa wazi katika Waefeso 6:10-23.
Ili mkristo aweze kuvishinda vita vya kiimani inatakiwa
aungane na Neno la Mungu kwa maana zaidi yeye na Neno ni wamoja,huyo anaweza
kuitwa mkristo aliyekamilika kiroho.
Jinsi ninavyopoteza uwezo wa kusoma Biblia ndivyo ninavyomwongezea
shetani nguvu na uwezo wa kuyavamia
maisha yangu.
Nikiona nguvu ya kusoma Biblia kwangu imeondoka nijue kabisa
ipo nguvu ya kipepo imenivamia na
nisipokuwa makini itanidhalilisha.
Wakuu wa ulimwengu huu wa giza ambao ndio napambana nao
katika vita vya kiimani hawaji kwangu
katika umbo la kibinadamu bali wanakuja kwangu katika umbo la madhaifu
mbalimbali,kwahiyo nisipokuwa na upeo wa
kutambua nitajikuta tayari nimeshakuwa
mtu wa kudhalilika .
Na mazingira wanayoyatumia wakuu wa giza kuharibu maisha ya
wakristo ni kama haya:-
i)Kuujaza moyo wangu hasira muda wote,hii yote ni ili nisiwe
mtu wa kusamehe.
ii)Kunijaza hila kwenye moyo
iii)Kunivalisha tamaa ya mwili na mali.
iv) Kunisukuma zaidi
katika hali ya kusema zaidi uongo,haya pamoja na mengine mengi ndiyo
yanayotumiwa sanasana na akuu wa giza wa ulimwengu huu lengo ni kuharibu
mfumo wa mtu anayemcha Mungu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni