SOMO LA
JUMAPILI: 7/9/2014
Somo la
Leo: PALILIA IMANI
• Inatakiwa
niipalilie imani yangu kwa sababu imani yangu ndio msaada wa maisha yangu,
vilevile Imani niliyo nayo nikiipalilia vizuri ndio itakayo nisaidia kupata
utawala wa rohoni, na ndicho kinachotakiwa kwa mkristo anayemwamini Yesu
Kristo.
ANGALIZO NO.
1 :
• Majaribu yaliyonizunguka yataondoka
kwangu kadri Imani yangu inavyokua .
• Namna ambavyo naweza kuipalilia Imani
yangu ikawa na mizizi ambayo itanisaidia kukabiliana na changamoto yoyote ile
ni kuruhusu moyo wangu uelimishwe na Neno la Mungu ( Biblia ).
•Hii inasikitisha wakristo wengi
hupuuzia kujifunza Neno la Mungu ( kusoma Biblia ) ndio maana shetani amepata
uwezo wa kuwaweka waamini chini ya mgandamizo
• Mgandamizo hauwezi kuruhusu imani ya
mkristo kupokea Baraka zake kutoka kwenye uso wa Mungu, kwa sababu mgandamizo
huyapofusha macho ya imani ya mkristo ,kwa hiyo ni vigumu mkristo kutambua
kusudi la Mungu katika maisha yake.
•( Macho ya imani yakipofuka mkristo
ataishi chini ya utumwa wa dhambi )
•Mkristo aliyepofuka macho ya kiroho
hawezi kuwa na ufahamu wa kutambua Baraka za Mungu zinakuja kwake kwa njia
gani.
-Jambo la kufahamu katika maisha
yangu kama mwamini wakristo tuliookoka lazima tuwe makini sana tunaishi katika
maisha yenye changamoto na vipingamizi vingi sana, ndio maana inatakiwa
kuziendeleza roho zetu katika kumfahamu Mungu zaidi ili tupate wepesi wa
kuyafikia maono yetu
• Nisipo ruhusu roho yangu kuendelezwa
na Neno la Mungu Imani yangu itapoteza ujasiri wa kukabiliana na utawala wa
giza.
- Mfano mzuri katika Biblia wa
mkristo aliyepoteza utawala katika roho ( ujasiri ) ni wana wa Skewa. Matendo ya Mitume; 19:13-16
•Mkristo anayeishi chini ya mgandamizo
ndani yake hana mamlaka yoyote ya kukabiliana na ufalme wa giza.
•Mkristo anayeishi maisha ya dhambi
maisha yake hukosa mpenyo, vilevile mwanga wa ki-Mungu Mstari wa 16,
•Imani ya mkristo ikikosa ujasiri ni
vigumu kuruhusu mpenyo wa Baraka
•Mkristo ambaye haishi maisha ya ukweli
kila jambo mbele yake litampa utata.
•Mwamini akiamua kuipalilia imani yake
kupitia Neno la Mungu changamoto zitakazo jitokeza mbele yake hazitakuwa na
nguvu.
•Ili niweze kuvuka kila changamoto
inayojitokeza mbele yangu inatakiwa niruhusu Neno la Mungu kuyaongoza maisha
yangu. Yohana 5:5-9
•Mgandamizo ukiyakalia maisha ya
mwamini, imani aliyonayo hupoteza mwelekeo yaani hata kile anachokijua anakisahau
*(Mkristo anayeishi katika maisha ya
mgandamizo kamwe hawezi kuishi maisha ya ukweli mpaka afunguliwe, na
inafahamika wazi maisha ya ukweli ndio yanayo ruhusu Baraka za Mungu kuambatana
na mtu. )*
•Sauti ya Mungu ni Neno lake kwa
maana zaidi ninaposoma Biblia najibishana na Yesu Kristo uso kwa uso.
•Wakristo wa leo hawaamini kwamba
Biblia ni hai katika maisha yao ndio maana kanisa la leo halisisitizwi kabisa katika kusoma Biblia,
ndio maana wakristo walio wengi wameweka tegemezi zaidi katika kuombewa kuliko
kukaa chini na kujifunza neno la Mungu likampa maarifa ya kumtoa katika
matatizo aliyonayo.
NIKIIPALILIA
IMANI YANGU ITANIPA FAIDA ZIFUATAZO :
A. Kutembea
na Roho Mtakatifu
B. Kupata
mamlaka ya Neno ( Uumbaji )
C. Nguvu (
Power )
UFAFANUZI WA
VIPENGELE HAPO JUU:
A. Kutembea
na Roho Mtakatifu.
o Mkristo anayeishi maisha ya Imani ndiye
mwenye uwezo wa kutembea na Roho Mtakatifu kwa sababu mwamini wa aina hiyo
anakuwa anaishi sambamba na mapenzi ya Mungu.
o Roho Mtakatifu anajifunua kwa mkristo
mwenye kina cha Neno la Mungu.
o Nikiwa Mkristo nisiyekuwa na kina cha
Neno ninakuwa ni Mkristo kimwili lakini kiroho sio Mkristo.
o Mwamini anayetambulikana kwamba ni
Mkristo katika roho ni Yule ambaye maisha yake anayaendesha kama Neno la Mungu
linavyosema hata kitabu cha Warumi kimesisitiza . WARUMI 8: 13- 16,
ANGALIZO NO.
2
o Mkristo mwamini akiishi kwa kufuata
maumbile ya kibinadamu yaani mapenzi ya mwili hawezi kuungana na Baraka za
Mungu, kwa sababu Mungu kuna kitu amesema katika kitabu cha Wakorinto.
o 1 wakorinto 6 : 17 -( Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho
moja naye ).
Nini maana
ya kuungwa na Bwana kama inavyosema 1kor
6:17 ?
• Maana ya kuungwa na Bwana ni kuyafanya
maisha yangu yakae chini ya muongozo wa neno la Mungu maana yake Biblia.
Wiki Ijayo
message hii itaendelea
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni