24-08-2014
ANGUKO LA WAKRISTO SEHEMU YA PILI
UTII
Maisha ya
wakristo waamini yameathirika kiuchumi, kifamilia, kielimu,kiafya, hii
inatokana na kuto kutii muongozo wanaopewa na watumishi wa Mungu katika
kukabiliana na matatizo yao.
Inafahamika
wazi utii una asili ya unyenyekevu ,kwahiyo mkristo akiwa ni mtii katika
miongozo anayopewa na kiongozi wake wa kiroho, changamoto yoyote itakayo
jitokeza katika maisha yake ya ucha Mungu, atakuwa na nafasi kubwa ya kushinda.
Ushindi wa
maisha ya mkristo umejificha ndani ya utii, hili jambo waamini wengi
hawajaligundua kwamba Baraka zao zimejificha wapi.
Mfano katika
hali ya kibinadamu: Mwanadamu anapo umwa (kuugua) hawezi kufika hospitali
daktari akampa dawa tu! Lazima atamuingiza kwanza kwenye vipimo , ili
atafute kufahamu ni ugonjwa gani unamsumbua ili aweze kupewa dawa sambamba na
ugonjwa alio nao; sasa basi katka hali ya kiroho mkristo anapokwenda kwenye uso
wa mtumishi wa Mungu akihitaji msaada wa kuponywa shida aliyonayo,inatakiwa
muongozo atakaopewa na Mtumishi wa Mungu kulingana na shida aliyonayo kwa hapo
haijalishi ni mwongozo wa aina gani,labda anaweza kuambiwa hudhuria kanisani
utafunguliwa,au chukua maji unywe yaliyoombewa,au soma Biblia kifungu Fulani,huu
mwongozo kitendo cha mwamini kuutii lazima afunguliwe,lakini asipoutii mwongozo
huo atazidi kuathirika mara dufu,kwasababu Mtumishi wa Mungu mwongozo anaoutoa
unatoka kwa njia ya Roho Mtakatifu,kwa
maana zaidi anakuwa amekaidi waziwazi sauti ya Mungu mwenyewe kupitia Mtumishi
wake,Biblia imefunua wazi juu ya utii,vilevile imeainisha Baraka zitakazo ambatana
na mwamini anayeiheshimu sauti ya Mungu Kumbukumbu la Torati 28:1.
( Utii
humsogeza mwamini karibu sana na Baraka za
Mungu).
Mkristo anapokuwa
mtii katika agizo analolitoa Mungu kupitia Mtumishi wake katika roho,mkristo
huyo hupata kibali ambacho ndicho husaidia mwamini katika hali ya kimwili kutokupungukiwa
kamwe na Baraka za Mungu.
Utii
hufungua milango ya ufahamu wa rohoni katika maisha ya mwamini,ndio maana Mungu
kaweka wazi kupitia Kumbukumbu la Torati 28:2 baraka atakazo ambatana nazo
mwamini akiwa na asili ya utii; jambo hili lahitaji ufahamu zaidi kwasababu
kila kitu kimefunuliwa wazi kuanzia mstari wa pili na kuendelea.
Chanzo cha
mkristo mwamini kupiga hatua katika maisha yake ya wokovu ni pale atakaporuhusu
hali ya utii wa maagizo anayoyatoa Mungu kupitia watumishi wake.
Anguko
linalowakumba wakristo na kusababisha maumuvu yasiyoponyeka ni pale ambapo
wakristo hao kukaidi sauti ya Roho Mtakatifu.
ANGALIZO 1:Ninapoikaidi
sauti ya Roho Mtakatifu maana yake ninamkufuru Roho Mtakatifu nikiwa nina akili
zangu timamu,ndiyo maana unaweza ukamkuta mtu yuko juu sana kimaisha, ghafla
akapukutika akawa hana kitu ni kwasababu ya kukaidi agizo moja tu ambalo Mungu
analitoa kupitia watumishi wake,watu wa aina hii Mungu amefunua wazi mapigo
watakayoambatana nayo katika maisha yao inaonesha kuanzia Kumbukumbu la Torati
28:15….
Maisha ya
wakristo waamini yameathiriwa na laana ambazo hutokana na kukaidi agizo la Roho
Mtakatifu.
ANGALIZO
2:Siku zote hakuna madhabahu inayomtangaza Yesu Kristo wa Nazareti na
udhihirisho wa Roho Mtakatifu ukaonekana mahali pale watu wakiponywa,
wakifunguliwa, wakirejeshewa afya njema halafu madhabahu hiyo ikasababisha
umasikini kwa watu au matatizo kamwe haipo wala haitatokea milele, bali
wakristo wengi ni wavivu kutendea kazi miongozo wanaypopewa na watumishi wa
Mungu,kwasababu huathiriwa na hali ya kulizoelea kanisa.
( Nikiruhusu
haki ya Mungu kuniongoza (mapenzi ya Mungu) mimi nitakuwa ni mtu wa tofauti katika
jamii).
Hakuna
dhambi mbaya kama ya kukaidi agizo la Roho Mtakatifu analolitoa kwangu na wakati
huohuo liko ndani ya uwezo wangu kulitendea kazi kama nikiamua.
Maisha ya
walokole yamekosa mipenyo ya Baraka za Mungu, kwamaaana zaidi yamefarakana na Baraka
za Mungu kwasababu ya majivuno ya mambo yafuatayo:-
a. Hata mimi ninajua kuomba
b. Hata mimi ninaweza kufunga nikamlilia
Mungu akanisikia, kwani! Siunajua Mungu hujifunua kwa yoyote hana upendeleo.
c. Hata mimi ninaweza kunena kwa lugha ,
haya ndiyo mambo yanayo wadidimiza walokole wa leo wadidimie kimaisha, vilevile
na umaskini usiondoke katika nyumba zao, walokole hujisahau na kitu hiki
hawakitambui, mpakwa mafuta yaani mtumishi aliyeitwa kwa jina la Bwana ambaye
elimu hiyo anayo ihubiri hakuipata kwa mtu yeyote wala mahali popote isipokuwa kutoka kwa Mungu kwa uwezo wa Roho
mtakatifu, huyo mtumishi ni jicho la Mungu, utakapo tii agizo atakalo kupa
maisha yatabadilika jumla wala hautaishi maisha ya kushindwa kwasababu agizo la
Mungu huja kwa njia ya Roho mtakatifu kumfahamisha mtumishi wake, na mtumishi
wake kutoa muongozo kwa kanisa , ndio maana Biblia inamheshimu sana mwamini
aliye chini ya muongozo wa Roho mtakatifu.
Warumi 8:12-16
ANGALIZO 3: Nikitaka kufanikiwa katika maisha ya
wokovu niache tabia ya kulizoelea kanisa , kwasababu kulizoelea kanisa husababisha madhara kwa watu wengi wa Mungu,
na madhara hayo hutokana na kupuuzia agizo linalotoka kwa mtumishi wa Mungu,
hichi kitu ndicho kinacho didimiza kanisa mazoea.
( Atakaye
chota Baraka za Mungu ni yule anayeendana sambamba na maagizo ya Mungu).
Kinacho wafanya
wakristo washindwe kuinuka kimaisha ni hali ya mazoea wanayoiruhusu katika
maisha yao na inafahamika wazi tabia ya mtu ni jumla ya mazoea yake.
( Kama
ninahitaji mabadiliko katika maisha yangu ya wokovu ninatakiwa nipingane na
hali ya mazoea, bali niruhusu utii wa kila agizo nitakalo lisikia mtumishi wa
Mungu akiliagiza, hapo nitafanana na Baraka za Mungu).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni