Jumapili, 21 Septemba 2014

PALILIA IMANI SEHEMU YA TATU



21/09/2014
PALILIA IMANI      SEHEMU YA TATU
UFAFANUZI WA KIPENGELE (C )
NGUVU (POWER).
Wakristo  waamini  tunapata nguvu ya Mungu kupitia Neno ( Biblia).
Neno la Mungu ndilo linalompa mkristo mwamini nguvu( uwezo ) wa kukabiliana na ufalme wa giza
Jina la Yesu Kristo linakuwa na nguvu(uwezo) kwa mkristo mwamini anayeliamini Neno la Mungu.
( Mkristo atakaye mwuona  Mungu ni Yule atakayeweka mizizi katika Neno la Mungu).
Katika kufundishwa Neno la Mungu(Biblia ) ninapata faida ya upeo wa ufahamu wangu kuongezeka ,kwahiyo itanisaidia namna ya kuambatana na Baraka za Mungu.
Nguvu ya Mungu inajiumba kwa mkristo ambaye ameamua kuutia moyo wake ufahamu wa kufundishwa Neno la Mungu.
( Nikiwa kwenye uwepo wa Mungu nahitaji kuwa na uhalisia wa kile kinacho tamkwa ndipo nitafanikiwa).
Wakristo wengi wanaokuwa kwenye uwepo  wa Mungu wanapoteza uhalisia  wa kupokea Baraka zao kwasababu misingi ya imani yao imejijenga katika vinavyoonekana.
Biblia ni nguvu ya mkristo anayemwamini Yesu Kristo.
Mkristo anayesoma Neno la Mungu katika imani lile neno linakuwa hai kwake kwahiyo hata atakapo kutana na majaribu atapata wepesi wa kupenya kwasababu nyuma yake kuna nguvu ya Neno la Mungu.
Mkristo aliyelifanya Neno la Mungu kuwa sehemu ya maisha yake  akawa analisoma katika misingi ya kiimani akaliheshimu na kuliamini  hila  yoyote ya shetani haiwezi  kumsogelea kwasababu Neno la Mungu humfunua shetani na kumuacha uchi mbele ya  macho ya mkristo anayeliamini Neno la Mungu Waebrania 4:12.
Ninapolisoma Neno la Mungu moyoni mwangu ninajengeka katika  nguvu za kiroho,kwahiyo kila jambo nitakalolifanya  au nitakalolikusudia moyo wangu utanipa ishara kwamba ni sahihi au si sahihi.
Wakristo wengi wametumia nguvu  nyingi sana katika kujiharibu, tena sanasana jamii ya waaminio ,kuliko kutumia nguvu nyingi kujijenga katika imani.
Mkristo akifundishwa Neno akapata nguvu za rohoni shetani hawezi kupata nafasi ya kuingiza uvamizi.
Nguvu inakuja katika moyo wa mwamini kadri mwamini anavyoongeza juhudi ya kulisoma Neno la Mungu
Zaburi 119:11
Madhaifu yanaingia katika maisha ya wakristo ,kwasababu mioyo yao inakuwa tayari imepoteza nguvu ya Neno la Mungu.
Moyo wa mkristo ambao umepoteza nguvu ya neno  tabia za mwilini yaani za kimwili huanza kujidhihirisha.
Nikiona tabia Fulani ya kimwili inaambatana na mimi au inanisumbua sana inatakiwa niongeze juhudi katika kusoma  Biblia na kufundishwa Neno la Mungu hapo nitapata mpenyo wa ushindi.
Tabia yoyote iliyofungamana na maisha ya mtu isiyompendeza Mungu ili iweze kun’gooka  inatakiwa roho ya mtu huyo ielimishwe na Neno la Mungu  kwelikweli  kwasababu tabia haina tofauti na roho chafu, ndio maana Biblia Zaburi  119:9 imetoa siri ya ushindi.
Njia ya kuyafanya maisha yangu ya wokovu yawe safi ni namna nitakavyokuwa na juhudi katika kujifunza Neno la Mungu , hii husaidia zaidi kuyafanya maisha ya  mwamini kuwa karibu na uwepo wa Mungu.
FAIDA YA NGUVU YA NENO:
Moyo wa mwamini  ukiimarika katika Neno la Mungu ndani mwake  huzaliwa imani yenye uwezo wa kuumba ,jambo hili lilimkuta Petro na Yohana wakielekea hekaluni .
Matendo ya Mitume 3:1-.
Katika Matendo ya Mitume 3:4. Kuna kipengele ambacho Petro alisema “ tutazame sisi”  alikuwa akidhihirisha wazi nguvu ya Neno la Mungu iliyojawa ndani mwake.
( Kupokea kwa mkristo anayemwamini Yesu Kristo kunaanzia katika Roho).
Hata kitendo cha kutokuliamini Neno la Mungu ni uzinzi tayari.
Maisha ya wokovu nilionao yatakuwa salama  kama nikiweka jitihada za kutosha za kufundishwa Neno la Mungu ,faida nitakayoipata katika hilo maisha yangu yatakuwa chini ya uwepo halisi wa Kimungu  

Hakuna maoni: