14/09/2014 JUMAPILI
UJUMBE WA LEO: PALILIA IMANI.
SEHEMU YA PILI.
KIPENGELE (B) KUPATA MAMLAKA YA NENO (UUMBAJI)
Ili niweze kutumia vizuri mamlaka
niliyopewa inatakiwa nifahamu kwanza chanzo cha mamlaka yangu ni wapi au ni
nini.
Chanzo cha mamlaka ya mkristo
anayemwamini Yesu Kristo ni Neno la
Mungu , na hii inategemea namna ambavyo mwamini ana kina katika kuliamini Neno
la Mungu.
( Kina cha imani ndicho kinazaa
mamlaka yenye nguvu ya kuumba jambo likatokea).
Waamini walio wengi hawalisomi
Neno la Mungu (kulisikiliza) katika misingi ya imani ndio maana mamlaka ndani
mwao hukosa nguvu ya kubomoa aina za vipingamizi wanavyokabiliana navyo katika
maisha yao ya ukristo.
( Kama mwamini haliamini Neno la
Mungu katika kina maana yake mamlaka alioyo nayo imekufa).
Mimi kama mkristo mwamini
inatakiwa nifahamu Neno la Mungu ninalolisoma ni hai,kwahiyo nikilisoma Neno
hilo lazima nilisome katika misingi ya kiimani,hata Biblia imeyathibitisha haya
katika Waebrania 4:12.
Mkristo anayeishi maisha ya ukweli
,yaani yaliyo sambamba na maandiko matakatifu yanavyosema huyo ndiye mkristo
mwenye mamlaka iliyo hai.
Maandiko matakatifu yanakuwa hai
kwa mkristo mwamini anayeishi maisha ya ukweli na huyo ndiye mkusudiwa katika
ufalme wa Mungu.
Ø
Mkristo asiye tii ndani ya kanisa anachoelekezwa
na Mtumishi wa Mungu maana yake huyo ni mtalii wa kiroho.
Ø
Mtalii wa kiroho huwa ana sifa hizi:-
i)Huwa ana imani ya tomaso.maana ya imani ya
tomaso huwa haamini anachoambiwa mpaka kitokee ndipo aamini
ii) Huwa hakubaliani na mwongozo anaopewa na
Mtumishi wa Mungu na kumfanya atoke katika shida aliyonayo,bali yeye hupenda
kuwekewa mikono , ndio maana utamkuta anatangatanga katika makanisa
tofautitofauti.
iii) Huwa ni mtu anayeihangaisha roho yake na kuinyima uhuru wa
kumtafuta Mungu,kwahiyo mtu wa aina hii amefarakana na Baraka za Mungu.
Biblia inathibitisha katika Waebrania 4:12 kwamba Neno
la Mungu li hai lakini litakuwa hai kwa mkristo mwenye imani ya Neno la
Mungu(Yesu Kristo).
Nguvu ya Neno la Mungu
ndio mamlaka yenye uwezo wa kuamuru chochote kikathibitika, kwahiyo
nikitaka hii mamlaka iumbike ndani mwangu inatakiwa nifanye mambo makuu mawili
yafuatayo:-
i)Kulisikiliza Neno la Mungu mara kwa mara hii ipo katika
misingi ya ufundishwaji.
ii) Kulisoma Neno la Mungu mara kwa mara, hii ipo katika
misingi ya kuielimisha roho yangu kuhusu Neno la Mungu katika kina zaidi.
Mahali ombapo moyo na roho hukutana ni kwenye faragha, na
katika faragha hiyo ndipo Mungu hupitishia taarifa zake.
Faragha ni sehemu ya utulivu na usikivu ndani ya moyo wa mkristo
anayemwamini Yesu Kristo.
Ili niweze kufahamu neno hili ninalolisoma li hai ndani
mwangu ni pale litakapoyagusa mapenzi
yangu.
( Siku zote mapenzi ya mwanadamu hayana utukufu kwa
Mungu,ndio maana mamlaka za wakristo zimekuwa butu).
MFANO;Panga lina sifa
ya kukata likiwa butu haliwezi kukata maana yake sifa ya panga imepotea;Ndivyo
ilivyo kwa mkristo mamlaka aliyonayo inanolewa kwa Neno la Mungu,asipo noa
mamlaka yake kupitia Neno la Mungu atakapokutana na majaribu hataweza kupenya.
ANGALIZO :Inatakiwa
nijihadhari sana vilevile niwe na bidii sana katika kuliamini Neno la Mungu,
kwasababu ninaweza kujikuta ninaitwa mkristo katika mwili lakini katika roho ni
mpinga kristo namba moja,hii inatokana na namna ambavyo ninakataa kuingiza
maarifa ya Mungu ndani mwangu yaniongoze.
KINACHO ATHIRI
MAMLAKA YA MTU.
Kila mkristo anayemwamini Yesu Kristo yaani aliyeokoka
tayari anayo mamlaka.
Yapo mambo mengi yanayoweza kuathiri mamlaka ya
mkristo,lakini kuna jambo moja kuu ambalo ndilo hupoteza kabisa uwezo wa
mamlaka ya mtu kufanya kazi
a)Maneno yasiyokuwa na maana.
Maneno yasiyokuwa na maana katika kinywa cha mkristo mwamini
ni sumu inayozima nguvu ya imani ipoteze uwezo wa mamlaka
Inatakiwa niwe makini katika kauli zangu,kwasababu kauli
zangu ndizo zinazothibitisha mahusiano yangu na Mungu kwa jamii inayonizunguka.
( Maneno yangu mimi ndio yanayofunua siri ya moyo wangu kwa
watu wengine)
Maneno ya kinywa changu ndio yanayothibitisha moyo wangu
umejawa na kitu gani.
Nikijifahamu mimi kwamba ninamkiri Yesu Kristo na kumwamini
yaani ninaishi katika maisha ya wokovu inatakiwa niwe na tahadhari katika
kunena kwangu,kwasababu Biblia imetahadharisha kitu yaani ukamilifu wa mkristo
unatokana na Yakobo 3:2b.
Ukamilifu wa mkristo anayemwamini Yesu Kristo upo katika
Neno.
Mkristo mwamini akilinda kinywa chake atakuwa ameiokoa
mamlaka aliyonayo hapo ndio utakuwa mwanzo wa mamlaka hiyo kumsababishia
Baraka.
Mkristo mwenye mamlaka kazi yake ni moja kuamuru vimrejee
alivyoibiwa na shetani.
Ili niweze kuipalilia mamlaka niliyo nayo inatakiwa
nilazimishe kinywa changu kunena kweli hata kama mazingira hayaruhusu kwa muda
huo , kusema ukweli,lakini nitakaponena kweli katika kinywa changu Roho
Mtakatifu ataingilia kati kuleta msaada kwangu.
Kuongezea maneno yasiyo ya kweli katika kauli zangu za kweli
kuna athiri mahusiano yangu na Roho Mtakatifu, huo ndio mwanzo wa Roho
Mtakatifu kumkimbia mtu, kwasababu Roho
Mtakatifu ni kweli ataishi kwa mtu anayeishi maisha ya ukweli.
Nikiishi sambamba na ndio yangu ni ndio na sio yangu ni sio
nitaambatana sambamba na Baraka za Mungu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni