MSAMAHA
Msamaha ni neno dogo sana lakini lina maana kubwa na nzito sanasana kwa jamii inayomcha Mungu.
Maisha ya mkristo aliyeokoka akiwa anajifunza kwa Yesu
Kristo, kusamehe kutakuwa ni jambo la kawaida katika maisha yake ,kwahiyo mtu
kama huyu kila Baraka inayotoka kwa Mungu itayavaa maisha yake
.
Nikiamua maisha yangu yawe chini ya mwongozo wa Neno la Mungu
kusamehe ni lazima bila kutazama mazingira ya kutendwa ,au mazingira ya maumivu
ninayoyapata.
( Kushindwa kusamehe kunazuia mpenyo wa Baraka za Mungu
katika maisha ya mkristo)
( Mkristo anayeshindwa kusamehe ndani mwake kumejengeka asili ya kulipiza kisasi).
Ninaposhindwa kusamehe maana yake ninamzuia Mungu asiingize
utetezi katika maisha yangu.
Kusamehe kunamsaidia mkristo kumwondolea hali ya
maumivu katika moyo wake ,ambayo
yangeweza kumsababishia mabo yafuatayo:-
i)Kuzuia mpenyo wa Baraka za Mungu.
ii)Kusababisha moyo wa mkristo kushindwa kupokea taarifa za
Mungu anaposema naye.
iii)Kumsababishia magonjwa, hii ni mbaya zaidi kwasababu
moyo ukizungukwa na mambo mengi na yanayosababisha maumivu ndani yake ina
athiri mfumo mzima wa mambo haya ;
a)Ufahamu
b)Mawazo
c)Fikra, hivi vitu vitatu vikiathirika katika moyo wa
mwamini ndipo matatizo yanapoanzia ya kuharibika kila kitu katika maisha yake.
Moyo wangu nisipouondolea maumivu ya kujeruhiwa nikasamehe
kila kitu ninachokifanya hakitafanikiwa
Luka 22:1-71
( Mkristo hata kama ameokoka akiwa hajafanyiwa ukombozi (Deliverance) hana uwezo wa
kusamehe).
Sina budi kusamehe hata kama jambo hilo limenijeruhi kiasi
gani inatakiwa nisamehe ili maandiko yatimie
Mithali 25:21
Kumtendea adui yangu mema ninaonyesha uhai nilio nao katika
ucha Mungu wangu,hapo ninadhihirisha zaidi kwenye uso wa Mungu kwamba nimejitoa
muhanga kwaajili ya Yesu Kristo.
Kutoa msamaha ni jambo linalohitaji Neema ya Mungu
kuingilia kati
.
Kabla ya mimi kutangaza msamaha kwa aliyenikosea inatakiwa
kwanza nijisamehe mimi mwenyewe ndipo msamaha nitakaoutoa utakuwa katika Roho
,kwasababu niliowakosea na kuwajeruhi ni wengi kuliko wanaonijeruhi mimi.
Nikifahamu kuna ambao mimi niliwakosea sina budi ya kusamehe
kila anayejikwaa kwangu,hapo nitarahisisha maandiko kutimizwa katika maisha
yangu,ndio maana Biblia ikasema wazi
Mithali
24:17.
Mtu ambaye ni kikwazo kwangu inatakiwa niingie kwenye maombi
mpaka niing’oe roho iliyomvamia hapo nitakuwa ninaitenda sawasawa sheria ya
Mungu.
Ninaposamehe ndio mwanzo wa kuruhusu hekima ya Mungu
kuniongoza.
( Ni aibu sana mkristo aliyeokoka kulipiza ubaya kwa ubaya).
Kushindwa kusamehe kumewafanya wakristo wengi kufarakana na
baraka za Mungu.
Kila mtu atakaye jikwaa kwangu kwa namna yoyote ile nifahamu
tu ameteleza ni ubinadamu ndipo nitapata wepesi wa kuachilia msamaha kwa
haraka,vilevile haijalishi amejikwaa mara ngapi kwangu au amenijeruhi mara
ngapi ninachotakiwa mimi kama mkristo aanayemcha Mungu aliye hai niyatende
maandiko,Hata Biblia imekonyeza juu ya hili
Luka 17:3-4
( Inatakiwa nilazimishe kusamehe ili ijengeke Roho ya Mungu
katika maisha yangu,na Roho ya Mungu ni Upendo).
Mimi ambaye nimeamua kutoa msamaha inatakiwa niwe na
tahadhari kuu nisije nikajikuta
ninajaribiwa kupitia hilo.
NINI KIFANYIKE ILI
NIWEZE KUSAHAU NILICHO KISAMEHE:
(Msamaha hauendi kwa mtu ambaye hajakiri na kutubu kosa).
Ili niweze kusahau nilicho samehe inatakiwa kwanza mimi
nitambue uthamani wa msamaha alioutoa Yesu Kristo katika maisha yangu,hapo
ndipo mwanzo wa asili ya kusamehe itakapojengeka katika imani yangu.
Mwanzilishi wa msamaha ni Mungu mwenyewe,aliusamehe
ulimwengu kupitia damu ya Yesu Kristo,kwahiyo kama mimi ni mcha Mungu sina budi
kuyaishi maisha ya Biblia ili neno msamaha liwe hai katika maisha yangu.
MSEMO:- “Nikiyatukana ninayoyashuhudia na
kuyasifu mbele za watu kwamba Mungu anaweza basi hata mimi ninaonekana ni
mkosaji vilevile ni mnafiki kwenye uso wa Mungu’’
SOMO HILI
LITAENDELEA WIKI IJAYO…………….
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni