Ijumaa, 22 Agosti 2014

BORESHA MAHUSIANO YAKO NA NENO



22/08/2014
BORESHA MAHUSIANO YAKO NA NENO
SEHEMU YA PILI.
SWALI:Kwanini inatakiwa niboreshe mahusiano yangu na Mungu?     
JIBU:Imani ya mkristo hulitegemea Neno la Mungu kukua.
MFANO:Mwili wa mwanadamu hutegemea chakula kukua,mfano wa chakula Ugali,Wali n.k.

Jinsi mwanadamu anavyoulisha mwili wake chakula kizuri ndivyo anavyozidi kustawi,yaani kupendeza zaidi.

Katika mambo ya rohoni imani hutegemea zaidi Neno la Mungu,kwasababu Neno la Mungu ndio chakula halisi cha roho zetu (imani zetu),Kwa hiyo jinsi ninaivyozidi kuzama katika kina cha Neno la Mungu ndivyo imani yangu inavyozidi kupata hali ya ufahamu wa kumjua Mungu zaidi.

(Roho yangu ikipevuka kuhusu Mungu lazima maisha yangu yatabadilika tu)

Nikijiona kuna mambo mengine kwenye maisha yangu ninashindwa kuyashinda nifahamu wazi roho yangu haijapevuka kuhusu Mungu ingawa ninaomba,kwahiyo juu ya hili ninahitaji ufahamu wa kina wa Neno la Mungu ili niweze kupata mpenyo.

Roho ya mkristo ikipevuka,Neno la Mungu hulisikiliza katika hali ya kiimani, na Neno hil;o huwa na uwezo mkubwa wa kufanya mabadiliko katika maisha ya mtu.

ANGALIZO 1:Nikisikiliza Neno la Mungu analolifundisha Mtumishi wa Mungu katika hali ya uziwi,hali ya upofu, kesho nitaposikia anasemwa vibaya hata mimi nitakuwa mmojawapo katika kuchangia hoja.

( Nikiwa msikiaji tu wa Neno la Mungu sio mtendea kazi Neno maisha yangu yatakuwa kikwazo kwa imani yangu,hapa au katika hili walokole huangukia katika mambo mawili
a)Kumlaumu Mungu kwamba hajibu maombi
b)Kuwanung’unikia watumishi wa Mungu kwamba hawana nguvu za kuwasababishia mabadiliko katika maisha yao,pia huishia kuwatukana na kuwasema vibaya,kumbe Mungu kila kitu amekiweka wazi sambamba na maandiko Matakatifu
Yakobo 1:21-25.

( ili niweze kuishi maisha ya haki inatakiwa nitafute kina cha ufahamu wa Neno la Mungu)

( Kama moyo wangu haumuelekei Bwana katika haki Mungu hawezi kusema chochote kwangu)

( Kutokana na Yakobo 1:21 mkristo anayeishi maisha ya dhambi kamwe hawezi kuendana na Baraka za Mungu,kwasababu Mungu ni haki na kweli).

( Nahitaji Neema ya kutawala, mafanikio yasije yakanitoa katika mapenzi ya Mungu)

Agizo la Mungu katika maandiko matakatifu kuhusu wakristo waamini ni kwamba Neno la Mungu tuliishi katika vitendo,na hii imethibitishwa kupitia Yakobo 1:22.

Nikiliweka Neno la Mungu katika vitendo nitaambatana na Baraka za Mungu waziwazi na hii ndiyo inayotushinda wakristo wengi na kuishia kwenye kuumana na kulana.

Biblia inazungumzia Baraka kwa mkristo ambaye ana mambo yafuatayo:-
i)Jambo la kwanza kuzingatia sheria ya Mungu.
Wakristo wengi wana bidii kuyazingatia mambo ya mwilini kuliko mambo ya rohoni. Je! Mambo ya mwilini ni yapi?
i)Tamaa ya mwili
ii)Tamaa ya macho
iii)Usingizi
iv) Chakula,katika mambo haya mkristo yupo radhi akosane na Mungu ili ayatimize,Tunahitaji Neema ya Mungu kanisa la leo.

( Mambo ya mwilini nikiyapa kipaumbele nitajikuta ninaishi maisha magumu yasiyokuwa na mpenyo,hii ndio picha wazi ya walokole wengi,ndio maana unawakuta wanatangatanga katika makanisa ovyo).

Maisha ya mkristo aliyeokoka ili apate mpenyo inatakiwa atambue kwanza udhaifu alio nao,aweke juhudi za kudhibiti udhaifu huo,hapo atakuwa ametengeneza mpenyo wa mafanikio ya Baraka za Mungu.

( Nikijifunza  kwa Yesu Kristo maisha yangu yatakuwa na usalama,Biblia imethibitisha hili Yohana 1:17).

Silaha ya mkristo aliyeokoka ni kusamehe.

Mkristo asiyekuwa na uwezo wa kusamehe huyo huitwa mtumwa wa dhambi.

Hakuna maoni: