17-08-2014
ANGUKO LA WAKRISTO
Wakristo
wengi wameanguka katika anguko la kuto kumuheshimu MUNGU, vilevile anguko la
kuto kutii sauti ya MUNGU pale inaposema.
Swali: je
sauti ya Mungu au agizo la Mungu nitalisikiaje?
Kuna njia
kadha wa kadha za kuisikia sauti ya Mungu:-
a). sauti ya
Mungu nitaisikia kwa kusoma Biblia
b). sauti ya
Mungu nitaisikia kwa kutoa muda kulisikiliza Neno la Mungu
Lazima awepo
mwanadamu aliye uvaa mwili ambaye Mungu anamwamini kupitishia ujumbe wake.
Anguko langu
mimi linatokana na kudharau muongozo ninaopewa na mtumishi wa Mungu,ambaye ndiye
kiongozi wangu wa kiroho katika mambo kadha wa kadha.
Wakristo
wengi huwa wanasikiliza Neno la Mungu katika hali ya uziwi wa kiroho, ndio
maana huwa hawana utayari wa kutendea kazi muongozo wanao pewa na Roho
mataktifu katika maisha yao, hiyo ndiyo inayosababisha vile vile huathiri
maisha ya wakristo wadumae katika maeneo haya:-
i. Eneo la uchumi.
ii. Eneo la afya
iii. Eneo la familia kukosa msimamo
iv. Eneo la ndoa kukosa kibali
i. Eneo la uchumi.
ii. Eneo la afya
iii. Eneo la familia kukosa msimamo
iv. Eneo la ndoa kukosa kibali
( Kitendo
cha kukaidi muongozo anao toa Roho mtakatifu kupitia mtumishi wake ni laana
ambayo huathiri watu wengi sana ).
(Sio kusudi
la Mungu niwe na maisha magumu niliyo nayo, bali ni laana inayo tokana na mimi
mwenyewe kushindwa kuheshimu agizo la Mungu linalotoka katika uwepo wake).
Maisha ya
wakristo wengi yameathirika sana kwasababu ya kudharau sauti ya Roho mtakatifu,
jambo hili lilimkuta mfalme Sauli.
1Samweli 15
Mtumishi wa
Mungu anapotoa agizo nikalikaidi nisilitendee kazi,maana yake nimekaidi sauti
ya Roho mtakatifu,kwahiyo Mungu atatoa mkono wake wa ulinzi kwangu vilevile mkono wa Baraka.
Agizo la
Mungu linapo toka huwa lina makusudi mema kwa kusanyiko la watu wa Mungu.
( Bila
kuzilingana hukumu za Mungu hakuna mpenyo kabisa).
Hali ya
majuto na maumivu hutokea katika maisha ya wakristo pale wanapo ikana sauti ya
Mungu na kuto kuitendea kazi, kwamaana zaidi mwamini anapoikana sauti ya Mungu
inayo mpa mwongozo katika maisha yake maana yake anamkana Mungu wazi wazi , na
inafahamika wazi hata kimaandiko “ Mtu anapo mkosea mwenzake Mungu aweza
kumsamehe, lakini mtu anapomkosea Mungu ni nani awezae kumsamehe?”.
1Samweli
15:13 Imeonyesha picha dhahiri ambavyo Sauli alivyo idhihaki sauti ya Mungu
makusudi , kwasababu, hilo alilo jisifia sio agizo la Bwana alilolinena
Samweli, Sauli alitendee kazi; bali agizo la Bwana ambalo Samweli nabii
alimueleza Sauli linathibitishwa kwenye mstari wa tatu.
Makosa ya
Sauli ya kukaidi agizo la Mungu yanathibitishwa na mstari wa tisa, na hapo
ndipo mwanzo wa laana yake ilipo anzia,vilevile huwa ndio mwanzo wa laana kwa
wakristo waamini katika kanisa la leo maisha yao kuharibika.
Ninapo kataa
kutii agizo la Mungu ninajisababishia athari katika maeneo yafuatayo ndani ya
maisha yangu:-
A. Kuzuiliwa Baraka za Mungu: Mtu ambaye Baraka
za Mungu zimezuiliwa juu ya maisha yake huandamwa na mambo yafuatayo:-
i.
Magonjwa,
hii husababisha pia mlipuko mbalimbali
wa kuathiri afya.
ii.
Kuathirika
katika suala la uchumi, hii husababishia madeni, biashara kukosa
wateja,kufukuzwa fukuzwa kazi ovyo, vilevile
kukataliwa.
iii.
Familia
kuambukizana roho za kurithi,vilevile roho za udhoofishaji, ndio maana unakuta
familia ufukara unaanzia kwa baba, mjukuu mpaka kwa kitukuu.
NAMNA YA KUEPUKA
ANGUKO KATIKA MAISHA YANGU
Ninaweza kuepuka anguko nitakapo ruhusu nia ya moyo wangu
kuambatana na sauti ya Mungu inayonipa mwongozo.
Hali ya nidhamu na utii nikiviruhusu kuambatana na maisha
yangu ya wokovu hiyo ndiyo njia itakayo
nisaidia kuepuka anguko lililo kusudiwa .
Nikitaka kuepuka matatizo kwa jinsi zake katika dunia ya leo
ninayoishi inatakiwa nikubali kuongozwa na uwepo wa Mungu.
Hali ya nidhamu na utii ikinitawala , bahati mbaya kukatokea
matatizo katika maisha yangu(majaribu), nitakapo muita Mungu kuwa mtetezi ataitika,
ndio maana Mungu alisikia kilio cha nabii Esta kama ilivyo andikwa,
Esta 4:
Siku zote kiongozi wangu wa kiroho akiwa anaufahamu wa Neno
la Mungu kwa kina, anauwezo mkubwa wa
kunifikisha mwisho wa maono yangu niliyonayo.
Ili maisha yangu ya wokovu yaweze kustawi inatakiwa nitafute
ufahamu wa rohoni yaani ufahamu
unaotokana na Neno la Mungu,ndiyo itakuwa njia pekee ya kutoka niliko kusudiwa.
Nikitaka kupona katika anguko lililokusudiwa katika maisha
yangu, inatakiwa nizame zaidi katika Neno la Mungu , ili nipate kibali cha
kunivusha.
(kibali anakipata mtu anapopata ufahamu wa rohoni).
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni