Jumamosi, 12 Julai 2014

VITA VYA KIROHO.



11/7/2014.
UJUMBE: VITA VYA KIROHO.

  • Vita vya  kiroho maana yake ni vita vya kiimani katika ulimwengu wa roho.



  • Ni vigumu kushinda vita vya kiroho nikiwa sina mahusiano mazuri na Neno la Mungu, kwa sababu Neno la Mungu ndilo linalosaidia imani ya mkristo kutawala katika roho.



  • Ninaweza kushinda vita vya kiroho (vita vya kiimani) kama nia ya moyo wangu imeamua kuambatana na Neno la Mungu

.

  • ( Vita vya kiroho vinahitaji ukomavu wa kiimani).



  • Mimi kama mkristo mwamini ninatakiwa niishi  maisha ya utawala katika roho, ndio maana Biblia imesisitiza jambo hili

Wagalatia 5:25.


  • Biblia inasema “Tukiishi kwa roho na tuenende kwa roho” maana yake zaidi tukiishi kwa imani na tuenende kwa imani,  huu ndio unaotakiwa  uwe msingi wa mkristo aliye okoka.



  • Nikiamua kuishi maisha ya imani yaani maisha ya wokovu,inatakiwa niwe tayari kujinyima baadhi ya vitu fulani ,ili kuilinda imani yangu inayomkiri Yesu Kristo isijeruhike.



  • ( Mkristo aliyesimama katika misingi ya kiimani ndiye mwenye uwezo  mkubwa wa kushinda vita vya kiroho).



  • ( Imani  ikidhoofika ndani mwamini ndipo mpenyo wa dhambi hutokea).



  • “Mkristo asiyekuwa na tabia ya kusamehe ana ugonjwa wa roho’’, mtu wa aina hii hata uso wake unaonyesha wazi kabisa, yaani hupoteza asili yake ya kawaida , bali huvaa kwenye uso wake asili ya hasira.



  • Siwezi kupenya katika vita vya kiroho kama sijaruhusu nia ya moyo wangu kupata mabadiliko kupitia Neno la Mungu

Warumi 12:1-3.


  • ( Chimbuko la dhambi ni mawazo mabaya, yaani nia mbaya ndani ya moyo).



  • “ Shetani huja kumjaribu mwamini katika umbo la kiroho,kama ufahamu wangu ni mdogo katika Neno la Mungu, nitamgundua akiwa tayari amekwisha kuniangusha katika dhambi”



  • Mkristo anayeishi maisha ya imani yaani maisha ya kumwamini Yesu Kristo hupata faida zifuatazo ;-

      a)Utawala wa rohoni.
      b)Kibali machoni pa Mungu.
      c)Baraka za Mungu kwa jinsi zake.


  • Nikidhibiti tabia zinazo nitoa kwenye uwepo wa Mungu hapo nitapata mpenyo wa kutawala katika roho , vilevile Mungu aweza kujifunua kwangu.



  • ( Nia ya moyo wangu ikiwaza sambamba na Neno la Mungu , ni rahisi mimi kama mwamini kudumu katika mapenzi ya Mungu ).



  • ( Vita vya kiroho nitavishinda iwapo utu wangu wa ndani utaamua kuishi sambamba na mapenzi ya Mungu ).



  • Mkristo aliye mwamini Yesu Kristo sio wito wake kuishi maisha ya dhambi, huwa wanalazimisha tu, ndio maana huangukia katika hali ya kujihukumu na kukosa amani mioyoni mwao

Mithali 1:23-31.


  • Lazima niweke mikakati ya mabadiliko katika njia zangu ili ziendane sambamba na Baraka za Mungu, ili wakati wa kujaribiwa Mungu aingilie kati.

.

Hakuna maoni: