MKAKATI WA KUJIENDELEZA KIIMANI
- Inatakiwa nijiendeleze kiimani kwasababu Imani za wakristo wengi zime poa kwasababu ya kujeruhiwa na mambo ya mwilini.
- (Imani yangu ikiisha jeruhika inapoteza mawasiliano na Mungu katika
roho kwasababu Imani ni daraja la kumuunganisha mwamini na Mungu)
- (Mkakati wa kujiendeleza kiroho utaisaidia roho yangu kupata uwezo
wa kupambanua kati ya sauti ya Mungu na roho zidanganyazo)
-Nina shindwa kutumia mamlaka niliyo nayo kwasababu ninawaza vibaya ,kwa hiyo nikiwaza vibaya nitaamini tofauti.
- Nina shauriwa kusoma Neno la Mugu ili ufahamu wangu uwaze sambamba
na Neno la Mungu linavyo waza hapo imani niliyo nayo nitakuwa
nimeiponya.
- Imani yangu imejeruhiwa na mambo ya mwilini, ndio maana imepoteza uwezo wa kunitoa katika dhiki niliyo nayo.
Kuna mambo mawili makuu yanayo ijeruhi imani za wakristo waamini.
a) Tabia za kale (asili)
b) Mawazo mabaya
Hivi viwili vina athiri Imani za wakristo kwa Mungu
- Mimi ninaye mwamini Yesu kristo, mlinzi wa maisha yangu ya mwilini na rohoni ni Imani, hata Biblia imeyathihirisha hayo,
1Petro1:5
-Ninapo ijeruhi Imani yangu kwa kuto kutii na kwa kutokufuata
muongozo wa Roho mtakatifu ninafungua mpenyo wa Imani yangu
kushambuliwa.
- Mimi kama mkristo mwamini maisha yangu ya
rohoni na mwilini hulindwa kwa Imani, kwa hiyo kama nikiruhusu Imani
yangu iwe dhaifu hapo ndipo shetani atakapo pata mpenyo wa kunidhoofisha
katika maeneo yafuatayo:-
A) Kiuchumi. Katika suala la uchumi kutatokea mambo haya
i)Kuona uchungu wakati ninatoa fungu la kumi, yaani kuona ile pesa ni nyingi mno
ii)Kupoteza hamu ya kutoa sadaka kanisani, yaani ninaweza
kuja na sadaka vizuri lakini wakati wa kutoa nisinyanyuke.
-Kesi ya uchumi haihitaji kuombewa bali inatakiwa mimi kama mkristo
mwamini nitembee katika formula ya utoaji na jambo hili limethibitishwa
wazi katika Malaki 3:8-12
Angalizo no1
-Nikitoa zaka
au michango mbalimbali kwenye madhabahu yenye ugomvi na Mungu
itanigharimu sana uchumi wangu yaani hata kufilisika kabisa nikawa sina
kitu.
Nisipotoa fungu la kumi kiuaminifu ninaijeruhi Imani
yangu ipoteze muunganiko na baraka zangu na Mungu, ndio maana maisha
yangu hayaendi juu.
- ( Mimi ninaye chuma na Mungu maana yake ninategemea ufalame wa Mungu kunibariki)
'' (Yesu nisaidie pesa isinitoe kwenye uwepo wako kwasababu
ninajaribiwa kupitia kile ninacho kipenda,kama mapenzi yangu yako kwenye
pesa nifahamu ndiko anguko langu lilipo)''
-Mafanikio
niliyonayo leo hayajalishi niya aina gani, kuna chanzo , na chanzo cha
chaweza kuwa kimegawanyika katika sehemu nyingi
a)
Katika kudhoofika kiimani, hiyo huwa ni njia rahisi ya shetani kumwingia
mtu na kumletea maumivu.Pia maumivu yamegawanyika katika sehemu
zifuatazo
i) magonjwa yasiyo tibiwa kwa dawa za kawaida
ii) Madeni
iii) Kukosa kibali na mengineyo
Angalizo no2
Nirahisi
nikaruhusu tatizo kuingia, ila kunagharama ya kulitoa tatizo likiisha
komaa , kwahiyo hapa inatakiwa niwe makini sana katika maisha yangu ya
kiroho.
b) Kudhoofika Kiuchumi
Kudhoofika kiuchumi kutaniathiri seemu hizi katika maisha yangu
i) Ufahamu wangu kushindwa kuzalisha wazo jipya yaani nikabaki katika hali ya mnung'uniko na malalamiko.
ii) Kupoteza kabisa mzunguko wa pesa katika maeneo yote yanayo niingizia kipato
iii) Kila kitakachoingia kushindwa kuitosheleza familia na majukumu mengine kimaisha , hayo
ndio mapigo yanayo ambatana na mkristo naye ishi nje na formula ya maandiko matakatifu (Biblia)
NINI KIFANYIKE ILI IMANI ISIJERUHIKE
-Nikita Imani yangu isijeruhike inatakiwa nianze kudhibiti nafsi yangu.
-Mkisto mwamini anapojitahidi kuidhibiti nafsi yake, huwa
anaiandalia mazingira ya kukua kwa kasi sana Imani yake kwasababu mambo
yaliyo jaa ndani ya nafsi ndiyo yanayo athiri mfumo wa utendaji kazi wa
Imani ya mkristo anaye litegemea Nenola Mungu.
-Nikitaka kuidhibiti nafsi yangu inatakiwa nifahamu ndani ya nafsi yangu kumebeba nini?
Mambo ambayo nafsi yangu imebeba
a) Hisia, ninafahamu wazi hisia huja hisia huondoka
b) Akili
c) Utashi
-Akili na utashi huwa vinategemeana kwasababu vyote huwa katika mfumo wa kunasa na kuelewa.
-Nikisoma Biblia hisia itaondoka itasimama Imani, nikisikiliza Neno
la Mungu utashi wangu utanasa , akili yangu itaelewa,italiweka Neno la
Mungu katika mfumo wa kukua zaidi katika misingi ya kiimani.
Nikiisha idhibiti nafsi yangu matendo ya mwilini yatakosa mguvu
kwasababu Biblia imeielezea wazi matendo ya mwilini na ndiyo yanayo
mfanya mtu akose haki yake kwenye uso wa Mungu "Ee Yesu nisaidie mimi
mtumishi wako" Wagalatia 5: 19-21
-Matendo ya mwilini yaliyo
nenwa katika Wagalatia5:19-21 kwa 100% ndio yanayo ifanya Imani ya
mkristo ipoteze muungniko na Mingu, na hapo mkristo asipo jigundua
mapema maisha yake ya ucha Mungu yatakuwa yamejengeka katika hisia za
kibinadamu , vile vile utashi wake utakuwa unanasa zaidi mambo ya
mwilini yaani ya kidunia , hapo ndipo mkristo huzitegemea akili zake
mwenyewe katika maisha yake ya kiroho , wakati Bwana alikwisha kutoa
angalizo juu ya hilo katiaka mithali 3:5
Swali: Kwanini Bwana alisema tumtegemee kwa mioyo yetu, tusimtegemee kwa akili zetu?
Jibu
: Kwasababu mawazo ya mwanadamu siku zote vile vile na akili yake
huwaza ubatili, ndio maana Biblia inazidi kuyafua zaidi katika Zaburi
19:14.
Utakatifu wa mkristo aliye okoka huja baada ya mkristo huyo kuwaza kama Neno la Mungu linavyo waza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni