Jumamosi, 21 Juni 2014

HAITAKIWI NIKATE TAMAA



MKESHA
HAITAKIWI NIKATE  TAMAA
Ø Kukata tamaa  huwa kuna onesha wazi hali ya kushindwa kwa mwamini na hii hali huwa inadhihirika kupitia maeneo yafuatayo:-

Ø Manung’uniko ndani ya kinywa cha mwamini,kupoteza kabisa hali ya kukiri ushindi  au inawezekana.


Ø Kupoteza hali ya kujihudhurisha kwenye  uso wa Mungu 

Ø Mfano:Siku za Juma pili vilevile  mkesha na vipindi vingine vinavyohusiana    na mafundisho ya Neno la Mungu

ANGALIZO:Mkristo ambaye amefarakana na kweli ya Mungu kamwe hawezi           kutoa neno la kunijenga,zaidi ya kuniingizia roho ya uasi

Ø Kukata tamaa ni hali ambayo humvaa mkristo katika mazingira yafuatayo:-
a)Pale ambapo  mkristo atatazama mazingira anayoyapitia au yaliyo mzunguka

Ø ( Ili wokovu nilio nao nikitaka ubaki salama haitakiwi nitazame mazingira ninayoyapitia hatakama yana ugumu kiasi gani).

Ø ( Mkristo anapokata tamaa huwa anaungana na ufalme wa giza kuukufuru ufalme wa Nuru “Yesu nisaidie nisiwe mmoja wapo”).
Yoshua 1:6-7.

Ø Neno la Mungu linavyosema “Uwe hodari na ushujaa”ni tahadhari mbele niendako hakuna urahisi bali ni kupambana, yaani ni kukabiliana na changamoto(majaribu) bila kukata tama.

Ø Nikitaka mwamini mwenzangu ashinde vita vya kiroho inatakiwa nimfariji kwa maneno ya imani.

Ø ( Ushindi wa mkristo ni namna anavyokiri)

Ø ( Mtu ambaye amekata tamaa maana yake, mbele anakokwenda haoni mpenyo)

Ø Mimi kama mkristo mwamini lazima nifahamu kwamba,kila jambo lina wakati wake chini ya jua,cha msingi nidumu katika mfumo wa kujihudhurisha  kwenye uso wa Mungu, ili wakati wa kubarikiwa ukifika unikute ndani ya uwepo wa Mungu.
Mhubiri 3:1-8

Ø Mapito ninaoyapitia leo sio mapito nitakayo yapitia tena kesho ,bali ya leo yatakuwa historia ya kesho ,kinacho takiwa ni kudumu katika  misingi ya ucha Mungu mpaka yatakapo timia.

Ø Mungu ni rafiki wa mwamini ambaye ana roho ya  uvumilivu, kwa sababu mtu mvumilivu hana historia ya kukata tamaa,bali hutazama mapenzi ya Mungu mpaka yatakapo timia.

Hakuna maoni: