Jumamosi, 21 Juni 2014

MAZIGIRA YA UOMBAJI



BIBLE  STUDY

MAZIGIRA YA UOMBAJI

Maombi ni mahojiano kati ya nafsi mbili,nafsi inayoishi mwilini  vile vie na nafsi inayoishi rohoni,yaani nafsi  ya Mugu na nafsi ya mwanadamu.

Nafsi hizi mbili huwa zinaungana kupitia imani iliyo simama katika misingi ya Neno la Mungu .

Nafsi ya mwanadamu ni vigumu kuishawishi nafsi ya Mungu kuleta mabadiliko ka mkristo  mwamini kama mkrosto huyo  hajaunganisha nafsi yake na Neno la Mungu kuwa kitu  kimoja.

Nafsi ya mwanadamu chimbuko lake ni Mungu, hili jambo alilithibitisha Yesu Kristo mwenyewe
Yohana 1:14.

Mimi nimeumbwa kwa Neno la Mungu, ndi maana intkiwa niishi maisha ambayo yanaendana na muongozo wa Neno la Mungu hii itanisaidia  hali ya utakatifu kuumbika ndani mwangu

Hali ya mwamini kukosa  mtiririko wa maombi inatokana na upungufu wa kina cha Neno  la Mungu ndani yake,hii husababisha madhara ya imani ya mkristo kuwa dhaifu.

Imani ya mkristo ikiishakuwa dhaifu ianakuwa haina uwezo tena wa kuhojiana na nafsi ya Mungu katika roho  au wakati wa kuomba, jambo  ambalo litamkuta mkristo ni kuomba sambamba na mapenzi  yake, wala si mapenzi ya Mungu “Haya maombi hufanywa na  asilimia  75 za walokole,kuomba sambamba na mapenzi yao binafsi, ndio maana maombi yao hayana matunda”
Mathayo7:7-11

Maneno yaliyoandikwa katika Mathayo 7:7 yatakuwa hai vilevile yataleta mafnikio kwa mkristo ambaye ataamua kuinyenyekeza nafsi yake kudumu katika mapenzi ya Mungu,juu ya hili hakuna anguko

Nikiishi katika mapenzi ya Mungu, ninalo likusudia kwa Mungu litatimia hata kama litachelewa.

Mkristo akitaka kufanikiwa katika maombi anayoomba kila siku kwenye uso wa Mungu,anatakiwa  afanye yafuatayo:-
      A)Maombi yake ayaweke katika vitendo

     Mfano wa kuweka  maombi katika vitendo
        i.            Ninaomba kupata kazi lazima nichukue hatua za kufuatilia kazi kwenye  makampuni, sio kuomba kupata kazi ,  nikalala nyumbani eti zita nifuata ,huo ni uksefu wa ufahamu

      ii.            Ninaomba nishinde dhambi,  lazima nichukue hatua   za juzuia mazigira yanayo nisababishia dhambi
(Nikiigeuza hoja yangu ninayoomba kwenye uso wa Mungu katika vitendo itazaa matunda )

(Imani yangu itakuwa hai zaidi nitakapo ijengea mazingira ya kusikiliza Neno la Mungu mara kwa mara yaani kulifanya Neno kuwa sehemu ya maisha yangu ya kila siku, kama nimnavyo kula chakula cha mwili kila siku(ugali na maharage)
Amen







Hakuna maoni: