UJUMBE WALEO
SABABU ZA WAKRISTO KUWA MASKINI
SEHEMU YA PILI
Watu wengi sanasana
jamii ya waaminio huwa wana utayari mdogo wa kutii ,vilevile kutendea kazi Neno
la Mungu pale wanapopewa mwongozo, ndivyo hata mafanikio yanavyyokuja kwa
kusuasua.
Mafanikio ya
kiuchumi katika maisha yangu yanakuja kwa njia moja ya utoaji ,kwasababu namna ninavyotoa
kusaidia wahitaji ndivyo ambavyo ninaongeza kiwango change cha kupokea kutoka
kwenye uso wa Mungu , juu ya hili utoaji ni thamani kubwa na inayoleta moyo wa
Mungukaribu na uchumi wa mtu.
Utoaji ni
sehemu kamili ya ibada kwenye uso wa Mungu.
Baraka za
Mungu zinajifunga kwenye maisha ya waamini sanasana jamii ya waaminio walio
wengi hawana hulka ya utoaji, ndio maana hata Mungu mwenyewe haoni sababu ya
kuwabariki na maneno haya
yanathibitishwa wazi katika Maandiko Matakatifu.
Ni vigumu
kupokea Baraka za Bwana ikiwa mimi
mwamini sijaandaa mazingira ya kubarikiwa .
(Hakuna
maombi yatakayo imarisha uchumi wangu nje na utoaji
Matendo ya Mitume 10:1-4)
Sababu za
sadaka ya mkristo kusikika kwenye uso wa Mungu na kuwa ukumbusho maana yake
mkristo huyo ametoa katika mazingira haya:-A)Ametoa kuwasaidia maskini Wagalatia2:10.
Tatizo la
watu wengi wanatoa nje na utaratibu wa Roho Mtakatifu, ndio maana utoaji wao
hauwazalii Baraka .
(Mimi kama
mwamini inatakiwa nitafute watu wa kuwasaidia ili nipate chanzo cha Baraka kuja
kwenye maisha yangu
2Mambo ya Nyakati 20:20.
Nikisahau
kuujenga mwili wa Kristo kwa kutoa basi nijue wazi shetani atajenga msingi wake
kwenye maisha yangu na msingi wa shetani
utakuwa umegawanyika katika makundi haya:-
Ukweli ni
kwamba kama familia yangu yenyewe siwalishi vizuri mimimwenyewe sijithamini
katika kuvaa vizuri,Je! Nitakuwa na uwezo gani wa kukumbuka yatima na wajane ‘’Eee
Yesu nisaidie’’.
Mimi kama
mkristo mwamini kuna vitu ambavyo inatakiwa nile navyo sahani moja ili niweze
kuuteka moyo wa Mungu
I)Mtumishi
wa Mungu :kuhusu Mtumishi wa Mungu ndipo jicho la Mungu lilipo kwasababu yeye
amebeba dhamana ya Mungu.
II) Yatima
na wajane.
(Hakuna
lingione lolote ninaloweza kulifanya likamgusa Mungu nje na utoaji , kwasababu
utoaji ndio umebeba dhamana ya utakatifu katika maisha ya mtu Malaki 3:10).
ANGALIZO 1:Kipengele cha utoaji shetani amewapiga
wakristo wengi upofu ili wasitambue uthamani wa utoaji kwenye maisha yao
,kwasababu yeye anafahamu fika Baraka itokanayo nautoaji Yeremia 23:23,24.
Mungu akiwa
ana faida na maisha yangu hawezi kuruhusu mimi niondoke mapema duniani ,kwahiyo
atanipa nafasi endelevu ili niweze kuyafurahia mema ya nchikama alivyosema
katika kitabu cha Isaya 1:19.
(Siku zote
maisha ya visasi hayaruhusu mafanikio katika maisha ya mtu, nikitaka kupona juu
ya hiliinatakiwa nijiunganishe na Neno la Mungu katika mazingira haya:-
i)Kusoma
Biblia
ii)
Kusikiliza Neno la Mungu katika mfumo wa Roho Mtakatifu
iii)
Kutafuta neno linalotoka katika kinywa cha Mungu kupitia Mtumishi wake
B)Ametoa
kuwasaidia yatima na wajane
1Yohana 3:17
Yakobo 1:26,27
(Baraka za
Mungu zinatoka kwa Mungu kuja kwenye maisha ya mkristo anayemwamini Yesu Kristo
huja kwa njia ya utoaji na hapohapo ndipo unapopimwa uthamani wa dini ya
mkristo).
(Nikitaka
kufurahia maisha ya wokovu inatakiwa nitembee katika kanuni za Roho Mtakatifu.’’Eee
Mungu nisaidie’’).
Mkristo
akianzisha njia za utoaji Mungu hufungua mlango ili asipungukiwe pale anapotoa
, kwasababu upendo huwa unadhihirisha picha wazi ya Mungu aliyeko ndani ya mtu.
Kama
ninahitaji mapenzi ya Mungu yathibitike kwenye maisha yangu inatakiwa niibebe nafsi
ya mwenzangu kama nafsi yangu , hata
hili neno Yesualiliagiza mwenyewe kupitia kinywa cha Paulo Mtume katika 1 Yohana 3:17.
(Hakuna
mabadiliko ysa kiuchumi yatakayotokea kwenye maisha ya mtu mpaka andiko litimizwe).
(Lazima
nyuma ya imani yangu kuwepo na tendo ndipo mambo mengine yaweze kuthibitika Yakobo
2:26.)
(Nikianza
kutenda kwa uaminifu kwenye uso wa Mungu maana yake nitafuta historia yote ya
mabaya yaliyokuwa yakinihukumu na kunishtaki kwenye uso wa Mungu Isaya
43:18)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni