Jumapili, 19 Oktoba 2014

UJUMBE WA LEO:VITA VYA KIIMANI.



19/10/2014
                                           UJUMBE WA LEO:VITA VYA KIIMANI.
Vita vya kiimani vinapiganwa kwenye ulimwengu wa  roho kwasababu imani ni kitu cha Rohoni.

Vita vya kiimani havipiganwi katika ulimwengu wa damu na nyama kwasababu imani haishikiki kwa mkono.

Wakristo walio wengi wanashindwa kwasababu vita vya kiimani wanavigeuza kimwili,kamwe mtu wa aina hii hawezi kushinda
.
Vita vya kiimani anaweza kuvishinda mwamini mwenye mambo matatu;
a)Msimamo.
b)Ujasiri.
c)Uvumuliviu, mtu mwenye asili hizi tatu  ndani mwake ni mtu wa imani.
 Vita vya kiimani vinamtaka mwamini jasiri.
 Waamini walio wengi wanashindwa  kufikia maono yaokwasababu wanapoingia kwenye uwanja wa mapambano  wanakuwa hawajavaa silaha kamilifu,Je! Silaha kamilifu katika uwanja wa mapambano ni zipi?.
i)Neno (Biblia)
ii) Imani (Yesu  Kristo)
iii)Uvumilivu (Ushindi).,Hizi ndizo silaha muhimu anazotakiwa kuwa nazo mkristo mwamini atakapoingia kwenye uwanja wa mapambano yaani (majaribu).

Mimi ninayemtegemea  Yesu Kristo inatakiwa maisha yangu yawe haki ndipo  nitaendana  sambamba na baraka za Mungu vilevile katika uwanja wa mapambano nitapata mpenyo.
Kipindi cha kujaribiwa ndio nafasi sahihi ya mwamini kuinuliwa.

Mungu anafurahia sana tunapopita katika kipindi cha kujaribiwa tukiwa tunalitumainia  jina lake kwasababu hata maandiko yanasema wazi uweza wa Mungu hutimilika  katika udhaifu katika maisha ya mtu.
2 Wakorinto 12:1-10.
 Hii ni  hatari sana na ndio  inayosababisha  watu wengi kuishia njiani  yaani wasifikie  maono yao wanapokuwa  katika kipindi cha kujaribiwa hutoa  maneno mengi sana ,na maneno hayo huwa hayana Baraka katika maisha yao zaidi kuwaharibu  kabisa,na mojawapo ya maneno ni kama haya:-
i)Nimemkosea nini Mungu mbona mimi tu?
ii)Yesu amenisahau
iii)Mbona sijatenda dhambi?
iv)Mbona mimi sadaka natoa na michango mbalimbali n.k.;Maneno kama haya katikati ya uwanja wa mapambano ndio yatakayo kufanya  ushindwe.
HATARI NAMBA MBILI
Wakati wa kujaribiwa wakristo wengi  hutoa nadhiri nyingi sana ambazo baadae hushindwa kuzitimiza ndio maana watu  hufa  vifo vya ghafla na matatizo mengi huwashukia ,pia mojawapo ya nadhiri wanazozitoa  ni kama hizi :-
i)Yesu ukinipa mtoto nitatoa sadaka ya gari .
ii)Mungu ukinibariki sitakuibia fungu la kumi .
iii)Yesu ukiniponya ugonjwa wangu hili ndilo kanisa langu  nitakalosali siku zote.
iv)Mungu ukinifungulia milango nitamjali mtumishi wako,maneno kama haya yasipotimizwa kwa wakati wake huleta madhara sana katika maisha ya watu.
Vita vya kiimani atavishinda  mkristo mwenye ufahamu sawasawa na Neno la Mungu.
NINI KIFANYIKEKATIKA UWANJA WA MAPAMBANO
Kitu ambacho ninatakiwa kukifanya ninapokuwa  katika uwanja wa mapambano  ni kuhakikisha imani yangu  iko hai yaani niwe na imani yenye  tendo,hili jambo hata kitabu cha Yakobo  kimesema
Yakobo 2:14- 26
Imani ya mkristo inahesabiwa kuwa hai pale matendo yanapodhihirika.
Ujumbe utaendelea  wiki ijayo…………..

Hakuna maoni: