12-10-2014
UJUMBE WA LEO: NAMNA YA KUKABILIANA NA ROHO ZA UDHOOFISHAJI
Roho ya udhoofishaji inamvaa
mkristo ambaye hajaimarika kiimani nahii
imekuwa ni ugonjwa kwa asilimia kubwa
katika wakristo wa leo, kwa maana
zaidi nguvu wanayo anzanayo katika kumtafuta Mungu sio wanayo maliza nayo ,
ndio maana Mgalatia akauliza swali
Wagalatia 3 yote
ANGALIZO 1:
Ni hatari sana kwa maisha ya kesho kukiwepo jambo nyuma yangu ili nimtafute Mungu.
Nivigumu kutambua nina roho ya udhoofishaji nikiwa nimefunga
milango ya Neno la Mungu moyoni mwangu.
Mkristo ambaye amefunga milango ya Neno la Mungu ndani ya
moyo wake anatabia zifuatazo
A)
Kutokuona umuhimu wa kumuabudu Mungu katika
vipindi vya kanisani yaani utoro
B)
Kujali majukumu yake ya kibinadamu kulikokukaa
chini kusikiliza Neno la Mungu
C)
Kuheshimu mwongozo wa mwanadamu mwenzake kuliko
kuheshimu mwongozo wa Mungu kupitia Roho
Mtakatifu.Mtu wa aina hii hawezi kukwamka katika hali ya kudhoofika ,mpaka pale
atakapo funguliwa (Delivarance).
Katika suala la kudhoofika kiimani
linatokana na wakristo wenyewe kutokufungua milango ya mioyo yao kulisikiliza
Neno la Mungu ndipo inapoanzia na mambo mengine kuharibika .
Ukidhoofika kimwili na mambo haya yatadhoofika kwasababu imani ndio msingi:-
i)
Utadhoofika kiuchumi
ii)
Utadhoofika Kiafya
iii)
Utadhoofika Kiufahamu
iv)
Utadhoofika Kifamilia n.k.
Mimi kama mkristo mwamini katika
maisha yangu ya kiimani lazima
nijichunge sana na jamii ninayokutana nayo
katika maisha yangu ya kila siku,kwasababu nisipokuwa makini athari za
kuathirika kiroho ni kubwa mno, vilevile
inabidi nitambue jamii ninayokutana
nayo kuna jamii ya waaminio na jamii ya
wasioamini.
Amosi
3:3
ANGALIZO 2:Nikiona
ninamwabudu Mungu alafu hapohapo nia ya
moyo wangu inaenda kinyume na kazi za Roho Mtakatifu maana yake ninalipinga
Neno la Mungu waziwazi ,mtu kama huyo hawezi kuambatana na Baraka za Mungu
kamwe.
Mkristo akiruhusu nia ya moyo wake kuambatana na Neno la Mungu
ameyaponya maisha yake ya kiroho kwasababu Neno la Mungu
litamuongoza kuyatenda mapenzi ya Mungu
tu.
Kumwabudu Mungu ni kufungua milango ya moyo kulisikilza Neno la Mungu
hapo ndio mwanzo wa hekima ya Mungu
kujiumba katika maisha Ya mtu.
Nia ya moyo wa mkristo mwamini ikienda kinyume tu na mwongozo wa Neno la
Mungu ndio mwanzo wa imani aliyonayo kudhoofika.
JE? NINAEPUKAJE HALI YA
KUDHOOFIKA KIIMANI
Ili niweze kuepuka hali ya
kudhoofika kiimani inatakiwa nifungue milango ya moyo wangu kusikiliza Neno la
Mungu peke yake yaani nisiruhusu yasiyofaa yapingananyo na Neno La Mungu
kuingioa kwenye moyo wangu
Warumi
10:17
Wakristo wengi wamedhoofika kiimani kwasababu haqwataki kuambiwa ukweli
na hiyo ndio silaha ambayo shetani
anaitumia kubomoa imani za watu wengi.
Hali ya kukubali kuambiwa ukweli inamsaidia sana mwamini kumuimarisha
katika misingi zaidi ya kumjua Mungu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni