USIOGOPE: SEHEMU YA
PILI
Mambo ambayo shetani huyatumia kuuchafua moyo wa mwamini upoteze uvumilivu.
b)
Kutokusamehe.
c) Mawazo
mabaya.
UFAFANUZI WA KIPENGELE ‘B’
KUTOKUSAMEHE.
Kutokusamehe
ni hali ambayo huunyima moyo wa mkristo ushindwe kutambua mapenzi ya Mungu ni
yapi katika maisha yake.
Mkristo
ambaye hana uwezo wa kusamehe huyo haishi na Mungu ndani mwake, hata kama
anashinda kanisani usiku na mchana.
Mtu mwenye
uwezo wa kusamehe ni yule ambaye moyo wake umeamua kuambatana na Neno la Mungu.
Kama moyo
wangu unaambatana na Neno la Mungu msamaha nitakao utoa ndani mwangu utakuwa
unatoka rohoni yaani kwenye nia ya ndani
ya moyo wangu.
( Haijalishi
nimetendewa nini cha kuumiza , bali inatakiwa niwe mtu wa kusamehe na kusahau
ndipo Baraka za Mungu zipate mpenyo wa
kuingia katika maisha yangu).
( Kuna mambo
mengi sana yanajifunga katika maisha ya waamini ingawa wanaomba usiku na mchana
hakuna mafanikio , hii hutokana na
kushindwa kusamehe na kusahau).
ANGALIZO 1: Maisha ya dhambi hapa chini ya jua husababisha wakristo kufa
mapema kabla ya wakati ambao Mungu amekusudia , ndio maana mkristo
anayeishi katika dhambi hana ufahamu
wowote
kuhusu mapenzi ya Mungu.
Nikiwa
mkristo ambaye ninatabia ya kusamehe na kusahau maana yake ninakuwa ninaishi
sambamba na mapenzi ya Mungu, jambo hili hata maandiko yamesisitiza zaidi ;
Marko 11:25,26.
Jinsi
ninavyo ruhusu moyo wangu kutangaza msamaha dhidi ya walionikosea au kinikwaza
vile vile kiniumiza , maana yake ninakuwa ninaruhusu mapenzi ya Mungu kuingilia
kati katika maisha yangu ya wokovu, vilevile Mungu ataniatamia.
Kutokusamehe
ni roho ambayo inatakiwa niikemee katika maisha yangu , kwasababu hali hii ya
kutokusamehe husababisha ufahamu wa
rohoni wa mkristo mwamini kujifunga.
Mimi kama
mkristo mwamini inatakiwa hali ya kusamehe iwe ni tendola kila siku katika
maisha yangu , hapa ninaweza kusema ninadumu katika mapenzi ya Mungu, kwasababu
mtu ambaye hasamehi amefarakana na imani ya Yesu Kristo.
Ninapotangaza
msamaha hatakama jambo hilo limenijeruhi kwa kiasi gani , ninakuwa ninamruhusu
Mungu mwenyewe kuingilia kati;
Warumi 12:14-21.
( Ninapo samehe ninaonyesha wazi asili ya
Mungu inayoishi ndani mwangu )
( Kusamehe
huwa hakutazami maumivu,bali hutazama mapenzi ya Mungu).
Kitendo cha
mimi kusamehe maana yake ninamkabidhi Mungu kutoa maamuzi ya haki.
(Siku zote
hukumu ya kweli na ya haki ni ya Mungu peke yake).
Suala la
kusamehe liwe ni tendo endelevu katika maisha yangu ya wokovu pasipo kukumbuka
maumivu ya jana, hapo nitakuwa mkristo anayeishi katika haki ya Mungu kweli
kweli.
( Kusamehe
ni upendo)
Siku zote
mtu anayekuchukia mtendee mema, mwisho wa siku roho yake itaona aibu.
“ Upendo ulioko ndani ya mkristo utaimarika zaidi
atakapo chukua hatua za kuutamka mara kwa mara”.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni