Ijumaa, 27 Juni 2014

BIBLE STUDY: 26/6/2014.

                                                        BIBLE STUDY: 26/6/2014. 

                                                                  USIOGOPE

-Haitakiwi niogope hata kama ninakabiliana na mazingira magumu kiasi gani,bali inatakiwa nikikutana na ugumu katika maisha yangu ya wokovu imani yangu niielekeze katika maandiko Matakatifu.



-(Kitendo cha mimi kama mwamini kuruhusu uoga kuuvaa moyo wangu tayari ninakuwa nimeijeruhi imani ,huo ndio unakuwa mwanzo wa imani niliyonayo kupoteza mwelekeo).

-Nikiruhusu mpenyo wa moyo wangu kushambuliwa kina cha maarifa ya rohoni kinajifunga.Kwasababu ndani ya moyo wa mwamini kuna faragha ambayo Roho Mtakatifu huitumia kuzungumza na mkristo mwamini,ndio maana Biblia imetoa tahadhari.
                                                         Mithali 4:23.

-Mambo ambayo shetani huyatumia kuuchafua moyo wa mwamini upoteze utulivu :-
a). Hofu
b). Kutokusamehe.
c).Mawazo mabaya.

UFAFANUZI WA KIPENGELE ‘A’ KINACHO ZUNGUMZIA HOFU


-Hofu ni adui mkuu wa imani niliyonayo vilevile humpotezea mwamini hali ya ujasiri katika moyo wake.

-Hofu ina kawaida ya kubadilisha mwelekeo wa imani ya mkristo,ili ipoteze uwezo wa kupambanua katika roho.

-Hakuna jambo linalotutokea na kutusumbua katika maisha ya mwilini ,Mfano:Magonjwa, Umasikini,Mauti, ikiwa Mungu hajatupa taarifa katika roho,ila shida inatokana na kutokuwa na uwezo wa kupambanua kati ya sauti ya Mungu na roho chafu ,
                                                     Amosi 3:7.

-Hofu ya maovu ninayo yatenda ndiyo inayo ninyima ujasiri wa kusimama kwenye uso wa Mungu kudai haki zangu kama mwana wa Ufalme.

-Moyo wenye hofu, mashaka, uoga, manung’uniko hauwezi kupata ujasiri wa kuhojiana na Mungu katika roho vilevile katika mwili,kwa sababu Mungu ni Mtakatifu,ndio maana ninatakiwa nidumu katika misingi ya Neno la Mungu ili kuulinda moyo wangu usijeruhiwe ukapoteza hali ya ujasiri wa kujieleza kwenye uso wa Mungu.

-Amosi 3:7 ni Neno alilolisema Mungu katika misingi ya kiapo lengo kuu ni kumthibitishia mwamini anayedumu katika maisha ya ucha Mungu kwamba asiogope changamoto yeyote ile bali aamini tu.

UJUMBE HUU UTAENDELEA WIKI IJAYO………

Hakuna maoni: