Uumbaji wa
kila ninachokiona chini ya mbingu chanzo chake ni Neno la Mungu.
( Simuamini Mungu kwakuwa ninamuoa katika machoya damu
na nyama bali ninamuamini Mungu kwasababu maandiko Matakatifu yananithibitishia
kwamba Mungu ni Roho;na hii imeandikwa katika : Yohana 4:24)
Yohana 4:24
ni agizo kwa kila aaminiye kwamba katika ucha Mungu wake lazima uwe katika
misingi ya rohoni (imani).
(Neno la Mungu ndilo linalotoa mpenyo wa baraka za Mungu
katika maisha ya mkristo)
(Neno la
Mungu ndio chanzo cha kila kitu)
Yesu kristo
anaishi ndani ya mwamini anayeliamini Neno la Mungu peke yake,na huyo ndiye
mkusudiwa katika ahadi za Mungu.
Neno la
Mungu ndilo linalotoa au linaloruhusu mambo yafuatayo kuja kwa mwamini:-
a)Baraka
b) Uponyaji
c)Afya njema
d)Mafanikio
ya mwilini kwa jinsi zake
e)Uzima wa
milele , vilevile hata maandiko yamelithibitisha hili; Mithali 4:20-22
Ninapo yasoma
maandiko na kuyaamini kwenye ulimwengu wa roho huwa napata ulinzi dhidi ya
nguvu za giza katika maeneo yafuatayo:-
a)Kuhusu
afya yangu
b)Kuhusu familia
c)Kuhusu
kazi zangu(biashara)
d)Kuwa na
kibali machoni pa Mungu na machoni pa wanadamu.
FAIDA YA KULIISHI NENO:
1.Faida ya
kwanza nitakayoipata katika maisha ya kuliishi Neno nitapewa mamlaka.
Neno la Mungu
ndilo linalozaa mamlaka ya uumbaji ,na mamlaka hii hufanya kazi katika
mazingira gani
a)Kuamuru
b)Kutamka,Hii
ni picha wazi katika kitabu cha Mwanzo 1:1,2,3,6,9,14,20 na 24.
Mamlaka
ninayoipata katika Neno la Mungu nikiitumia vizuri nitakuwa mtu wa tofauti katika jamii inayonizunguka.
Wakristo
wengi wamepoteza mamlaka ila wokovu wanao,ndio maana wengi wamedumaa kiroho.
Kinacho
ruhusu mpenyo wa mkristo kuwepo ni mamlaka inayotoka katika Neno la Mungu.
Ili
maisha yangu yawe salama kiroho na kimwili
inatakiwa niikuze mamlaka ya Kimungu
ilioko ndani mwangu.
Kushindwa
kuitumia mamlaka iliyoko ndani mwangu
inatokana na mahusiano yangu na Neno la Mungu kuwa mabovu.
2. Faida
pili ya kuliishi Neno itanisaidia mimi kupata roho ya uumbaji.
3. Faida ya
tatu ya kuliishi Neno ni kupata ufahamu wa rohoni na hii ndiyo inayotakiwa kwa
mcha Mungu.
Hali ya
ufahamu ikiisha jiumba ndani ya muamini
hupata uwezo wa kupambanua, vilevie halihiyo ya ufahamu itamsaidia
muamini kudumu katika Roho.
Hali ya ufahamu
huwa inaathirika ndani ya mkristo akiruhusu tabia za asili kumuongoza.
Ili mkristo
apate ufahamu wa kuishi maisha Matakatifu inatakiwa yeye na Neno la Mungu kuwa
wamoja, vilevile hata Yesu Kristo kuna jambo alilolisisitiza kudhihirisha
upendo wa kweli alionao mtu kwa muumba wake
Yohana14:23,24.
Udhihirisho
wa upendo wangu kwa Mungu ni namna ambavyo ninavyo iamini Biblia na kusoma Neno
la Mungu lililondikwa ndani ya Biblia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni