Jumapili, 18 Mei 2014

SUNDAY SERVICE 18THmay2014 RIVER OF HEALING MINISTRY ARUSHA( KAPERNAUM CHURCH)


               


                                    ujumbe:  WOKOVU SEHEMU YA PILI
 
Ø  Wokovu  ni nini?
Ø  Wokovu ni Neema ya Mungu iliyoko juu ya mtu ambaye amemwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake, ndio maana Bibllia ikasema  Waefeso 2:8.

Ø  Wokovu ni Neema vilevile Neema ni upendeleo usio stahili juu ya mtu yaani ‘’hakustahili kuitwa mtumishi wa Mungu lakini kwasababu ya Neema ya Mungu anaitwa Mtumishi wa Mungu’’.

Ø  (Inatakiwa niutunze wokovu nilio nao kwasababu ni zaidi ya dhahabu, kwasababu wokovu ni Neema inayonipa mimi mwamini kuuishi  umilele wa Mungu).

Ø  (Wokovu ni zawadi iliyotoka kwa Mungu juu ya maisha yangu).

A.      KANUNI ZA KUTEMBEA KATIKA WOKOVU
Ø  Ili niweze kutembea katika kanuni halisi za wokovu, inatakiwa nisome Biblia nione uhalisi wa maisha ya Yesu kristo alivyo ishi akiwa katika mwili wa damu na nyama.Kwa maana zaidi Yesu Kristo awe mfano wangu mimi ninaye muamini , hata maandiko matakatifu yamesisitiza juu ya jambo hili   1petro2:21-25.

Ø  Katika kutembea ndani ya uhalisia wa Yesu Kristo Biblia inafunua wazi kwamba , inatakiwa mimi ninaye muamini Mungu, nifuate kwa wazi nyayo za Yesu Kristo kama ilivyo andikwa katika 1Petro2:21-24.

Ø  Je! Nyayo za Yesu Kristo ambazo Biblia inazisema ni zipi?
A.      Yesu Kristo hakutenda dhambi , huo ndio mwenendo wa kwanza wa Yesu Kristo.
B.      Wala uongo haukuonekana kinywani mwake.
C.      Hakuwa mtu wa kulipiza kisasi.
D.      Alikuwa mtu mwenye Upendo wa kweli. ambaye tayari amekwisha kuwa Roho. 

UFAFANUZI WA KIPENGELE (A )KINACHO ZUNGUMZIA DHAMBI 
                                                 Dhambi ni nini?
Ø  Dhambi ni uasi , vilevile kila jambo lililo kinyume na mpango wa Mungu ni dhambi , jambo hili hata biblia ime lifafanua,1 Yohana5:17a  vilevile 1Yohana3:4, hapo tunapata ufafanuzi kuhusu dhambi yaani matendo ya giza.

Ø  (Dhambi haina heshima)

Ø  Kazi ya dhambi ni kudhalilisha utu wa mtu, vilevile huondoa uthamani alionao mtu katika jamii

Ø  Nini kinacho fanya wokovu wa mtu udhalilike?
·         Ni kwasababu ya kukosa maarifa ya ufahamu wa Neno la Mungu, yaani Maandiko matakatifu(Biblia).

Ø  Wokovu wa mkristo mwamini utaimarika iwapo mkristo huyo ataruhusu Neno la Mungu kuielimisha roho yake, kitakacho tokea kwa mkristo aliye elimishwa roho yake na  Neno la Mungu ni kina cha maarifa ya rohoni kuongezeka, yaani kuwa na kina zaidi cha kumjua  Mungu hapo ndipo wokovu wa mkristo utakuwa salama.

Ø  Nikitaka kuishinda dhambi inatakiwa mimi na Neno la Mungu tuwe wa moja, hapo nitakuwa na asili moja na Mungu kwaasababu Mungu ni Neno Yohana1:1,2

Hakuna maoni: