Ijumaa, 9 Mei 2014

INATAKIWA NIJIIMARISHE KIIMANI (ibada ya mkesha 9-05-2014 na Mtumishi wa Mungu Bab G Power)



                                                         

  • Suala la mimi  kujiimarisha kiimani inatokana na juhudi yangu binafsi; kivipi? Jinsi ninavyokuwa ninajitoa kusoma Biblia , vilevile kusikiliza Neno la Mungu.



  • (Nirahisi kubadilika kiimani vilevile kimaisha kama nitaruhusu maarifa ya Neno la Mungu kuniongoza).



  • Mtu ambaye anaruhusu maarifa ya Neno la Mungu kumuongoza hupata faida zifuatazo:-

a.       Hupewa na Roho wa Mungu uwezo wa kupambanua sauti ya Mungu wakati wote  Mungu anapo sema na mtu huyo.


b.      Hupata muunganiko  wa kweli na Baraka za Mungu, yaani hufanikiwa kwa kila atakacho kigusa
.
(Nikiona ninahangaika sana kimaisha, sifanikiwi, ninatakiwa nirudi chini nianze kuisoma Biblia usiku na mchana , kama  jinsi Yoshua 1:8 inavyo sema , nirahisi nikafahamu wapi niliko teleza au kukosea; kwasababu Biblia inanifahamu hatakama ninaisoma, ndio maana inauwezo wa kunielezea mimi nilivyo kiroho vilevile kimwili).

Kusoma Biblia kunaimarisha imani ya mkristo kwenda sambamba na misingi ya Yesu Kristo, kwasababu kwenye kusoma Biblia ndipo  tunapo ifahamu kweli halisi ya Mungu ni ipi.

Msemo:

Kuifahamu kweli nusu kunamadhara  makubwa kuliko uongo mkamilifu, yaani nibora mtu akakunyima chakula  kuliko kukuonjesha chakula  akakuacha bado unanjaa.


Maisha bila msaada wa kiroho hayaendi ; mwanadamu bila Neno la Mungu ni sawa na kipofu anyetembea katika njia yenye mashimo, hawezi kufika safari yake akiwa salama

Hakuna maoni: