Jumatatu, 21 Julai 2014

NAITAMANI SANA KARAMA YA UVUMILIVU.


20-07-2014
NAITAMANI SANA KARAMA YA UVUMILIVU.
Katika ujumbe wa leo kuna maneno makuu matatu yaliyo ubeba ujumbe, kabla ya kuendelea ,inatakiwa nipate ufafanuzi wa maneno haya ,ili ufahamu wangu upate upeo wa kuelewa yatakayozaliwa katika ujumbe wa leo
.
Neno la kwanza ni KUTAMANI
Neno la pili ni KARAMA
Neno laa tatu ni UVUMILIVU


UFAFANUZI WA NENO LA KWANZA: KUTAMANI
Kutamani ni hali fulani inayo andaa maandalizi ya jambo fulani kuthibitika, kwa lugha nyingine kutamani ni kunia ndani ya moyo, na inafahamika wazi jambo ambalo mtu amelinia ndani ya moyo  wake nilazima atalitenda tu.

UFAFANUZI WA NENO KARAMA
Karama ni zawadi au ni kipawa anacho kiachilia Mungu juu ya mtu, kwa lugha nyingine karama ni Neema inayo toka kwa  Mungu na kuyavaa maisha ya mtu bila kutazama mazingira ya huyo mtu yalivyo.

TAFSIRI YA NENO UVUMILIVU
Uvumilivu ni hali fulani ya kungojea au kusubiria  vilevile ni subira.

Uvumilivu ni karama yenye msingi wa Imani kubwa ndani yake.

Imani za wakristo waamini zimejeruhika kwasababu ya kukosa hali ya uvumilivu katika maisha yao, hii ni picha wazi mtu wa aina hii hawezi kumcha Mungu katika roho na kweli.

Mkristo aliyekosa hali ya uvumilivu hata kuabudu kwake sio sahihi, kwasababu uvumilivu ni tendo la Imani, vilevile jambo hili Mungu aliliweka wazi hata kimaandiko
Mathayo 24:9-13

(Msingi wamaisha yangu ya ushindi upo ndani ya tendo la uvumilivu)

Nitabarikiwa kulingana  na kiwango cha Imani yangu inavyo kua, ili mfanikio yakija yasije yakanitoa nje   ya uwepo wa Mungu.

Mwamini akikosa uvumilivu ndani ya moyo  wake hawezi kutoa maamuzi sahihi katika kile ambacho anakinia kukifanya ,bali atakuwa mtu anaye jikatisha tamaa mwenyewe , ndiomaana  Biblia jambo hili imelifunua pia kwa undani
Warumi 14:23

Mkristo aliyekosa uvumilivu kamwe hawezi fanikiwa katika maisha yake yote atakuwa ni mtu anayeishi kwa taabu mwanzo wa maisha yake mpaka mwisho wa safari yake,hapa inabidi nifahamu nililokusudiwa na Mungu kulipitia nitalipitia tu  ili maandiko yatimizwe katika maisha yangu.

Uvumulivu niliona mimi ndio unao andaa historia ya mafanikio kwa kizazi changu kinacho kuja nyuma yangu, juu ya hili inategemea kama nimekuwa mvumilivu katika kusubiri baraka za Mungu pamoja na hukumu zake,kizazi changu mimi hakitatoka katika misingi hiyo kamwe ,zaidi kitakuwa ni kizazi chenye kutoa msaada kwa wengine ‘‘ee Mungu nisaidie’’.

Nikiwa mwamini niliyekosa hali ya uvumilivu kizazi changu nitakiandalia hali ya kushindwa.

Haitakiwi niangalie mazingira ninayoyapitia hata kama yana maumivu kiasi gani bali inatakiwa nivumilie ili niendane sambamba na Baraka za Mungu alizoziahidi kupitia maandiko Matakatifu,hata Biblia kuna kitu imegusia katika
Waebrania 11:8-10.

Mkristo yoyote ambaye hajatambua makusudi ya Mungu katika maisha yake hawezi kuwa mvumilivu, na hii inasababishwa na upofu wa kiroho alio nao makristo huyo.

Mimi niliye okoka inatakiwa nifuate nyayo za Yesu Kristo kwa asilimia zote,kwasababu Yesu Kristo hakushindwa katika mazingira yote ingawa alijaribiwa na kupata maumivu,kwasababu alikuwa ameuvaa mwili wa damu na nyama,hili jambo ni sahihi kabisa,ndiyo maana hata katika Zaburi 23:4 inathibitisha.

(Haitakiwi niogope changamoto yoyote ninayoipitia ,kwasababu hapo ndipo ulipo mpenyo wa Baraka zangu,cha msingi ni kuwa mvumilivu).

Hakuna maoni: